Walaaniwe wote wanaoupotosha umma wa Tanzania - Mhariri, Mwananchi

M TZ 1

Member
Oct 12, 2010
34
3
Ndugu watanzania wenzangu,katika kupitia magazeti mbalimbali yanyoaminika na kuheshimika mbele ya umma wa tanzania nimekutana na makala katika gazeti la mwananchi,nimeona niwaonjeshe utamu wa hii mada,sasa nimeanza kugundua kwanini serikali inalikandamiza hili gazeti.nawasilisha

 
Ni wahariri wachache sana Tanzani wenye uhuru na uwezo wa Kupembua mambo kama huyu wa Mwananchi na ningewaomba kampuni yao ianzishe Televishion kama walivyofanya Kenya, nigefurahi yule Mhariri wa Nipashe Jumapili aje hapa asome huu uchambuzi na aombe radhi kwa uharo aliotuandikia Jumapili.
 
Hata mimi nimeshangaa jinsi watu tulivyoupokea mgomo wa CHADEMA, yaani kuna watu wameapiza na kuapiza. Nafikiri kufuatana na kanuni za bunge, ni kitu ambacho kipo na hakina adhabu kama Mh Sitta alivyosema, na kwa wanaofuatilia mabunge ya wenzetu hii sio ajabu. Kuna ambao wanatamani kumbeba mheshimiwa rais kwenye mbeleko (mgongoni) kwa jinsi wanavyoona kama kaonewa mno kwa kitendo hiki.
 
Gazeti la mwananchi liko very independent. Wao kijiko wanakiita kijiko na siyo chuma kilichokunjwa. Tatizo la waandishi wetu wengi wa habari ni kusumbuliwa ama na uoga au njaa. Wanaamuliwa na wanasiasa waandike kitu gani. Ni utumwa wa aina fulani hivi unaowadhalilisha sana (ingawa wao hawajui). Hebu fikiria gazeti kama la Habari leo ambalo limepoteza heshima yake na kuwa kama magazeti ya udaku ya Shigongo. Wamesahau kuwa linaendeshwa kwa kodi zetu na si michango ya wanachama wa CCM.
Big up mwananchi, mwanahalisi na raia mwema. Ole wenu waandishi wanafiki
 
Sio tu wananchi wa kawaida wamepotoshwa, pia baadhi ya wabunge wa upinzani hawakuwaelewa Chadema, sijui ni shule ndogo?
 
Tuna media house chache sana zenye kusema hali halisi kama Mwananchi Communications. Nakereka na Habari Leo kuandika habari kishabiki zaidi kuliko mantiki. Hata hivyo watanzania tunazidi kuimarika kifikra, sasa si tu kwamba tunasoma na kuangalia taarifa mbali mbali bali tuna uwezo wa kupembua taarifa.
 
Na ulaaniwe mwenyewe na uzao wako. Chadema walipoingia kwenye uchaguzi hawakujua kuwa katiba iliyopo ina mapungufu hayo???? Baada ya kushindwa urais ndipo wanatukosea heshima tuliowatuma bungeni. Kudadadeki, walichemsha wapende, wasipende na wote mnaoshabikia upuuzi huo, ...................... ah, bora ninyamaze tu.
 

Naamini wewe mzee kibiongo ni mmoja wa wale wenye macho lakini hawaoni. Kutoka nje ya bunge ni kitendo halali na cha kistaarabu kabisa cha kuonyesha msimamo wao. Chadema hawajavunja sheria yeyote kama 6 alivyosema. Katika nchi yeyote yenye demokrasia lazima uwepo uhuru wa mtu au kikundi cha watu kutoa maoni yao, hiyo ndiyo ilikuwa njia sahihi kabisa kwa chadema kumweleza jk kuwa hayupo pale kwa ridhaa ya wananchi na wao hwatambui ushindi wake ingwa ameshaapishwa
 

Ee wanajamvi msameheni maana hajui alitendalo.
 

How old are you???
 

Dogo uwe na heshima!
CHADEMA walipoingia kwenye uchaguzi walijua kuwa KATIBA inamapungufu ndiyo maana walilielezea hilo kinagaubaga katika ILANI yao, na mgombea wa kiti cha Urais toka CHADEMA Dr.(wa ukweli) W. P. Slaa alisema mara nyingi kuwa ataanza kulishughulikia hilo katika siku 100 za kwanza atakapokuwa madarakani.

Ulikuwa unasikiliza nini wakati wa kampeni, Radio uhuru? mipasho?....

Wewe mwenyewe ndiwe unajukisea/jivunjia heshima (japokuwa sina uhakika unayo kwa kiasi gani) kwa kuwa ni mvivu wa kukumbuka na hodari wa kuropoka.

Naomba uendelee kunyamaza,
Invisible said:
Ficha upumbavu wako, usifiche hekima yako
 
Bila ushabiki wa kisiasa madai ya katiba mpya na tume huru ya uchaguzi ni ya msingi kabisa na ni kwa faida ya kila mtanzania mpenda taifa lake na kwa kizazi hiki na vizazi vijavyo. Kwa maana hiyo basi kila mtanzania mzalendo hana budi kuunga mkono madai haya.
 
Yawezekana ni upuuzi. Kila mtu ana namna yake ya kupima mambo. Waweza ona upuuzi lakini umefikiria huo upuuzi unavyoweza okoa shari tuendako? Unadhani watu wataendelea kuwa watulivu siku zote huku wakiamini kuwa wanadhulumiwa? Umesikia yaliyotokea Shinyanga, Karagwe, Mwanza na kwingine, je, watu wale walichochewa na nani? Kama watu wataendelea kukandamizwa amani lazima itatoweka.
Hii ni kanuni ya maisha ya mwanadamu duniani pote, rejea yaliyotokea Philipines, China, Marekani na kwingi duniani. Kunapotokea ukandamizaji, hatua ya pili ni kupingwa kwa ukandamizaji, tatu ni namna ya upingaji na mwisho ni vita. Congo wanapigana mpaka leo sababu ya Marehemu Mobutu, Burundi uasi unaendelea, na Tanzania haipo peponi. Mwaka huu 2010, mmeshuhudia watu wakipigana na kuuana na polishi kupiga mabomu ya machozi kila sehemu. Kwa mfumo huu wa kukibeba chama kilicho madarakani, naiona vita kuu siku si nyingi.
Mlio vipofu mtadhani CHADEMA wataanzisha vita, amini nawaambia vita itatokana na mfumo unaowalinda watawala. Na itakuwa vita kati ya watawala na vibaraka wao dhidi ya wananchi waliochoshwa na ukandamizwaji. Kwa taarifa tu, kuna jeshi kubwa la vijana wenye umri wa kuanzia miaka 13 ambao miaka 5 ijayo watapenda kuona mabadiliko. Kama 2005 waliandikishwa milioni 9, 2010 milioni 20, mwaka 2015 je? Wapenda amani na si madaraka tafakari, chukua hatua!!!!!!!!!
 
Nakubaliana na mhariri hapo

Wana Chadema naona mmemfagilia sana huyo mhariri lakini kesho akija na issue ya kukosoa Chadema wote mtasema amenunuliwa na mafisadi!
 

for sure.
 
Mod (Invisible), wawekee watu wapige kura za maoni kama watu wana support au kuto support KITENDO CHA WABUNGE WA CHADEMA KUTOKA NJE YA UKUMBI WA BUNGE WAKATI RAIS AKIHUTUBIA. Hapo tutajua mwelekeo wa wana JF
 

MK CHADEMA walilisema hilo toka mwanzo, kuwa endapo wangepewa ridhaa ya kuiongoza hii nchi, hivyo vingekuwa vipzumbele vyao. Naamini kabisa kama Dr. Slaa angetangazwa kuwa mshindi wa kiti cha urais, basi kwenye hotuba yake ya kufungua bunge angeyagusia yote hayo. Kwahiyo punguza jazba Mzee
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…