Wakuu wa Wilaya kubadilishwa

Wakuu wa Wilaya kubadilishwa

wakati wa chama chashika hatamu, ukuu wa wilaya ulikuwa ni cheo cha mtu wa dalasa la saba waliohitimu Hombolo au handeni. sijui siku hizi kigezo ni kipi!
halafu chuo cha mzumbe, mkoloni alikuwa nakitumia kuwafunza watumishi wa serikali na wanafunzi wengine, kuja kuwa wakuu wa mikoa na wilaya, ndio maana kilikuwa kinaitwa chuo cha uongozi-Mzumbe. sasa leo watu wanateuliwa kuwa wakuu wa wilaya bila ya hata , ujuzi wa how to spend, development and recurrent fund, wewe unategemea nini hapo? ukuu wa wilaya ni vyeo nyeti sana kuliko hata ukuu wa mikoa. kwa sababu huko wilayani ndiko kwenye vijiji vingi sana na wakazi walio wengi ni masikini. sasa mkuu wa wilaya sifa zake kubwa ni mojawapo ya kujua , how to eradicate povety(kupambana na umasikini), how to create jobs, how to improve infrastuctures and peoples' wellbeing. kama serikali haitazingatia sifa hizo inapoteua wakuu wa wilaya, basi itakuwa inawafukuza wakuu wa wilaya kila mwezi!

MY take: ukuu wa wilaya kiwe cheo cha kufanyiwa interview mtu na sio okotaokota tuu bora kasoma!!!

Acha Urongo,ilikuwa sifa ni kuwa Kada,siku hizi imeongezeka,
1..ukubali kuvua ch**i,(mke).
2..uwe unacheka cheka kama kibonde(Ubwabwa)m/ume.
 
Kuna tetesi za ndani nimesikia kutakuwa na mabadiriko ya wakuu wa wilaya nchi nzima wengine watatoka na wengine watapangiwa sehemu zingine hii ni kutokana na wengine kushindwa kumudu nafasi walizoteuliwa......

Mambo no yale yale. Kukarimiana kwa zamu. Si mnajua nafasi zenyewe za uongozi ni chache, hivyo lazima kupeana muda wa kulamba kidogo kisha unamuachia na mwenzako naye alambe. Hivyo hivyo hadi woooooote walio ahidiwa neema na malipo walambe lambe kidogo.
 
Mwenye Job discpription ya wakuu wa wilaya na mkoa tafadhari, hadi sasa sijajua hua wanaenda ofisini kufanya nini, ni kama makamu wa kwanza wa rais, nae pia hua sielewi hasa ofisini hua anafanya nini though huyu akitoka ofisini atleast hua anamkasi wa kukatia utepe.
 
Kuna tetesi za ndani nimesikia kutakuwa na mabadiriko ya wakuu wa wilaya nchi nzima wengine watatoka na wengine watapangiwa sehemu zingine hii ni kutokana na wengine kushindwa kumudu nafasi walizoteuliwa......

Ni kuhamisha ufisadi kuutoa Dodoma kuupeleka Musoma......!
 
Na ukiona hivyo ujue Mh Dhaifu Kuna Mrembo kamuopoa hivyo anataka kumzawadia "zawadi maalum" ambayo ni ukuu wa wilaya!!
 
Hii tunaita kuyatembea maneno..."walk the talk"....wakuu wa wilaya watarudishwa wanajeshi (makapten na usalama wa taifa) ili ku'monitor' wahamiaji haramu! Hizi ni jitihata za kawaida hasa nchi inapokuwa katika mazingira ya kuwa vitani muda wowote kama ilivyo hivi sasa! Mnaweza nikosoa kama nimepotoka! Unapokaa mwingine tu wala hujua mbinu za adui hata namna ya ku'mobilise watu inakuwa ni shida! Nipo pamoja nawe raisi wangu! MAwifi na mashemeji waliopo wilayani kwa sasa hawatufai kwa hili!

Mi sitaki bhana , kumbe kuna mashemeji na mawifi !
 
kuna jamaa mmoja anaitwa JACLINE liana.ni DC katika mkoa mmoja lake zone,huyu jamaa ni kilaza hakuna mfano,yeye anafanya kazi ya NAPE ,anafungua matawi ya CCM,kuimarisha chma nk.na nasikia alikuwa mwandishi wa gazeti la uhuru,nafikikiri JK angeanza na huyu
 
Nitatuma jina langu liwepo
"Vox populi,Vox populi"
 
Hii hamisha hamisha ya mara kwa mara ni matumizi mabovu tu ya pesa zetu za kodi!

Serikali kila siku wanalalamika hakuna pesa; lakini hapo hapo hata zile kidogo zilizopo zinatumika kwa matumizi ambayo hayana umuhimu.

Kwa nini uajiri kiholela halafu uje kufanya mabadiliko kabla hata mwaka mmoja haujapita?!

Kama huu si uendawazimu ni kitu gani?!
 
Mwenye Job discpription ya wakuu wa wilaya na mkoa tafadhari, hadi sasa sijajua hua wanaenda ofisini kufanya nini, ni kama makamu wa kwanza wa rais, nae pia hua sielewi hasa ofisini hua anafanya nini though huyu akitoka ofisini atleast hua anamkasi wa kukatia utepe.

Ebu tuanze na majukumu yaliyomo ndani ya serikali za mitaa kama sheria zinavyoanisha and then tutakwenda katika serikali kuu.Sababu,kwa utendaji wa serikali za mitaa na ule wa serikali kuu unafanyika katika maeneo yale yale hivyo inapasa kuwa na upeo wa kutosha kuhusu mgawanyo wa majukumu kwa ngazi tatu,yaani wizara,mkoa na wilaya

MADARAKA YA WAZIRI MWENYE DHAMANA YA SERIKALI ZA MITAA

kwa mujibu wa kifungu namba 4 vya sheria namba 7 na 8 za mwaka 1982,majukumu ya waziri mwenye dhamana ya serikali za mitaa ni kuhakikisha kwamba mamlaka zote za serikali za mitaa zinajengewa uwezo wa kutekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria.Uwezo huo wa serikali za mitaa unaangaliwa katika fani mbalimbali ikiwa ni pamoja na fedha,utumishi,usimamizi wa sheria na nidhamu.

MADARAKA YA MKUU WA MKOA
Kifungu cha 5(3) cha sheria za tawala za mikoa Namba 19 ya mwaka 1997 kinaeleza wajibu wa mkuu wa mkoa kwa mamlaka ya serikali za mitaa ni kuziwezesha na kuzijengea mazingira ya kutekeleza majukumu yao ya kisheria.Dhana hii ya uhuru wa mamlaka ya serikali za mitaa inaegemea katika sharti kuwa,mamlaka hizi zitakuwa zinajiendesha kisheria.Lakini pale itakapobainika kuwa sheria haifuatwi,basi uhuru huo hautalindwa,bali serikali kuu ikiwa ni pamoja na mkuu wa mkoa itaingilia kati kuona kuwa sheria zinatekelezwa.Msingi huu wa fikra ndiyo uliosababisha kumpa mkuu wa mkoa uwezo wa kuingilia au kuwaruhusu maofisa wa serikali kuu kuchunguza nyaraka pamoja na kumbukumbu nyingine za fedha za mamlaka ya serikali za mitaa.Lengo ni kutaka kugundua endapo kuna ukiukwaji wa sheria au kanuni za fedha.Hatua hizi ni kwa mujibu wa kifungu cha 44 cha sheria ya fedha za serikali za mitaa namba 9 ya mwaka 1982.Kifungu cha 78A cha sheria namba 8 ya mwaka 1982,Kinampa mkuu wa mkoa madaraka ya kusimamia utekelezaji wa sheria za mamlaka za serikali(Mamlaka za Miji),ikiwa ni pamoja na kuchunguza uhalali wa vitendo na maamuzi ya mamlaka hizo na kumuarifu waziri ikiwa kuna ulazima wa kuingilia kati endapo vitendo na maamuzi vinakiuka misingi ya sheria.

MADARAKA ya MKUU WA WILAYA
Kifungu cha 14 cha sheria za tawala za mikoa namba 19 ya mwaka 1997,kinampa mkuu wa wilaya majukumu ya kuziwezesha na kuzijengea mazingira mazuri mamlaka za serikali za mitaa zilizomo ndani ya eneo lake ili ziweze kutekeleza majukumu yake ipasavyo.Aidha kifungu cha 78A cha sheria namba 8 ya mwaka 1982,kama ilivyo kwa mkuu wa mkoa,Vimetoa uwezo wa mkuu wa wilaya kuchunguza uhalali wa vitendo na maamuzi ya Mamlaka ya Serikali za mitaa katika eneo lake.

Mkuu huyo anatakiwa kumjulisha waziri mwenye dhamana ya serikali za Mitaa ikiwa kuna ukiukwaji na uvunjaji wa sheria na kanuni za nchi katika utekelezaji wa majukumu na maamuzi ya mamlaka za serikali za mitaa.Mkuu wa wilaya atakuwa mwenyekiti wa kamati ya ushauri ya wilaya(DCC)

NOTE: Hii ni kwa upande wa serikali za mitaa,kwa upande wa serikali kuu nitakupostia nikipata nafasi
 
Mi sitaki bhana , kumbe kuna mashemeji na mawifi !



Wengine ambao nasikia wanaweza kuupata Udc ni
Hamy-D
ZeMarcopplo
Mafililha
Habariyamujini
Chillisosi
Mafilili
Scramble bila kumsahau
Chris Lukosi mbeba mabox na
FaidhaFox ametoa pichu
 
Kuna tetesi za ndani nimesikia kutakuwa na mabadiriko ya wakuu wa wilaya nchi nzima wengine watatoka na wengine watapangiwa sehemu zingine hii ni kutokana na wengine kushindwa kumudu nafasi walizoteuliwa......
vijana wa lumumbasasa wanakesha kwa babu kuhakikisha kuwa wankuwepo kwenye orodha, dogo mwigulu nadhani atapewa wilaya walau tano peke yake kwani kafanya kazi ya kuwakenusha meno wakulu kwa kiwango kikubwa, kumbuka ishu za tindikali , mabomu , na mengineyo. wakikosa utawaona humu jf wanavyolalama ,mara ooohhh post zangu mimi zilisomwa na watu wengi ...mara oohhh mimi nilikuwa nashinda lumumba kila siku kupeleka habari za mabango na makavu tuliyopewa live bila ngache.
 
Kuna tetesi za ndani nimesikia kutakuwa na mabadiriko ya wakuu wa wilaya nchi nzima wengine watatoka na wengine watapangiwa sehemu zingine hii ni kutokana na wengine kushindwa kumudu nafasi walizoteuliwa......

Jk na mimi nione japo ni mwanachama wa ncc---m.Ni mtendaji mzuri kama mbati.nitajitolea pia kukusaidia kuondoa gwandaz tehe tehe inhi inhi.
 
Kweli wabadilishwe ili tupate taswira mrejesho wenye tija zaidi.
 
Kuna tetesi za ndani nimesikia kutakuwa na mabadiriko ya wakuu wa wilaya nchi nzima wengine watatoka na wengine watapangiwa sehemu zingine hii ni kutokana na wengine kushindwa kumudu nafasi walizoteuliwa......

Naomba hiki cheo kifutwe kabisa ni mzigo kwetu.
 
Back
Top Bottom