Wakulima watekeleza mashamba ya nyanya kwa kukosa wanunuzi wilayani Kilosa

RUCCI

JF-Expert Member
Oct 6, 2011
1,701
1,714
Baadhi ya wakulima wa Nyanya wa kijiji cha Dumila wilayani Kilosa wametelekeza mashamba ya nyanya na kuziacha bila kuvunwa huku zaidi ya tani moja ya nyanya hizo zikiharibika na kutupwa kila siku kutokana na kukosa wanunuzi.

Wakiongea kijijini hapo baadhi ya wakulima ambao wamekutwa katika gulio la nguzo mbili wakiuza nyanya wamesema hali yao kiuchumi inazidi kuwa mbaya kwasababu zao ambalo walitegemea liwakomboe kiuchumi limekosa soko na wanunuzi.

Wakulima wengine wamesema wamekata tamaa na kuacha kuendelea kuvuna nyanya shambani kwasababu gharama za pembejeo walizotumia katika uzalishaji wa zao hilo ni kubwa kuliko bei ya kati ya shilingi mia tano na elfu moja kwa ndoo moja ya nyanya.

Katibu tawala msaidizi sekta ya uchumi na uzalishaji ofisi ya mkuu wa mkoa wa Morogoro Bwana Ernest Mkongo amesema changamoto ya soko la nyanya msimu huu limesababishwa na kuwepo kwa uzalishaji mkubwa na kwamba mkoa umeandaa kongamano la uwekezaji ili kupata wawekezaji wa viwanda vya kusindika nyanya na mazao mengine ya mbogamboga.

Chanzo: ITV
 
Nyanya ni nyanyue nyanya ni nyanyase!!! Nyanya imenyanyasa haswaa! !!!
============
Bahati mbaya serikali haioni umuhimu wa hata kutoa pole ama kuomba radhi kwa kuwatelekeza wakulima wa nyanya. Wakati ni serikali iliyohimiza watu wafanye kazi kwa bidii! !!
 
[HASHTAG]#KILIMO[/HASHTAG] NI UTI WA MGONGO#

[HASHTAG]#KILIMO[/HASHTAG] KWANZA#

.......................
 
Na msimu huu nyanya zimekubali mbaya,home nina kibustani kadogo lakini zimekubali mno,ni changamoto kwa serikali,ile kauli mbiu ya Tanzania ya Viwanda ipo wapi?,vijana wametumia nguvu kuwekeza nguvu zao huko matokeo yake ndo hayo,inavunja moya mno...
 
Pamoja na kuongezeka uzalishaji wa zao hilo la nyanya, sina uhakika kama hao walikuwa wanalijua soko lao ni lipi! Je, wakulima walitambua kuwa soko la zao lao la nyanya lingeathirika kutokana na Serikali kupiga marufuku safari za watumishi wake zisizo na tija.

Nina maana kuwa soko kuu la wakulima wengi wa mazao kama nyanya, vitunguu, maharage na mbogamboga ni kando kando ya barabara kuu, hasa wasafiri. Wenye uwezo wa kununua wengi walikuwa wenye magari binafsi katika safari zao, mara nyingi za kikazi. Wengi wakinunua kwa ajili ya matumizi ya nyumbani na wengine pia kwa biashara (walanguzi).

Ni muhimu Maafisa Biashara, maeneo husika, wasaidie wakulima kuwatafutia soko ikiwa ni pamoja na mbinu za kuongeza thamani.

Yawezekana pia kutafuta njia mbadala ya kuzihifadhi zao la nyanya, kama vile kuzikausha na kutengeza unga wake.
 
SEREKALI YETU KWA HARAKA SANA IWAITE WANUNUZI WA NYANYA KUTOKA KENYA WAJE WANASURU WAKULIMA WETU,HATUNA VIWANDA HATUNA JINSI NI AIBU ZAO HILI LILILOTUMIA NGUVU NYINGI KUOZEA MASHAMBANI
•serekali active tutaijua tu.
•waziri wa kilimo unalionaje suala hili?
•Are fit or not?
 
Back
Top Bottom