Wakristu tupunguze mbwembwe na majivuno jamani

Nsimbi

JF-Expert Member
Sep 27, 2014
1,091
1,202
Vitabu vya dini vinatutaka kuwa wanyenyekevu. Sio kuwa na kiburi na mbwembwe kama walivyo baadhi ya viongozi wa dini wa kizazi hiki. Ni hodari wa kushiriki misiba ya matajiri lakini ya masikini wanaikwepa.

Nafarijika kwamba Wakristo na Waislamu wote wanamuabudu Mungu mmoja. Ndiyo kwa namna tofauti lakini hilo halipaswi kuwa tatizo kubwa.

Nafurahia zaidi namna Waislamu wengi wanavyofanya mambo yao kwa unyenyekevu mkubwa. Waislamu wapo simple katika mambo yao na hivyo ndivyo dini na mitume wanavyotaka.

Wako simple kwenye kuzika, ndoa, tohara na namna nzima ya maisha yao. Pengine ni kwa sababu wanafahamu zaidi kwamba dunia hii tunapita tu.

Ndani ya Ukristu na baadhi ya Wakristo wengi kuna mbwembwe nyingi. Viongozi wengi wa makanisa wanajikweza sana.
Msingi mkuu wa Ukristu ni kujinyenyekeza kwa Mungu na wanadamu. Lakini sasa Ukristu umeingiwa na kirusi. Mbwembwe za wanaojiita maaskofu, manabii, wachungaji nk nk zinatisha. Badala ya kuwa wachungaji hivi sasa watu hawa wamekuwa walaji wa kondoo ...yaani waumini wao!

Kuna 'maaskofu' wanalindwa kama wafalme. Wanaishi katika nyumba za kifahari mno. Wana mimali ya kutisha. Baadhi wanamiliki ndege na magari ya kifahari mno. Pesa imewekwa mbele sana katika makanisa hasa revival churches na visingizio mbalimbali hutumika hususani Biblia kuhalalisha uovu.
Kifupi viongozi wengi wa revival churches hutumia sadaka za waumini kujinufaisha wao binafsi, wake na au hawara zao na marafiki zao.

Yesu na mitume wanaojifanya kuwahubiri waliishi maisha humble sana. Bwana alihimiza humbleness. Kitu ambacho sikioni kwenye maisha ya hawa viongozi wa makanisa. Viongozi wengi wa dini wamejaa unafiki, majivuno, dharau na wengi hujitenga kabisa na masikini.

Najiuliza hawa 'maaskofu' wanamhubiri Yesu gani? Kwa kweli ni kufuru kufanya biashara kupitia jina hili Takatifu. Wala si haki kuwapumbaza waumini kwa mahubiri yao uongo ili watoe pesa nyingi za sadaka. Viongozi uchwara wa dini huwakumbatia wenye fedha.

Utitiri wa makanisa si jambo la fahari. Watu hawa wajiitao manabii nk, wanafanya biashara. Period! Wanatumia advantage ya matatizo ya watu walio desperate kupata suluhisho la matatizo yao. Shame on them.

Hawa jamaa hawana chembe ya huruma kwani wanawanyonya hata waumini masikini. Wanakula mali za wajane na huwa convince wafuasi wao kutoa hata akiba zao kuwajengea 'maaskofu' nyumba na kujaza mafuta katika gaaa riii zao!! Ama kweli wajinga ndio waliwao!!
Tanzania na Watanzania wengi ni malofa. Lakini bila aibu baadhi ya 'maaskofu' hao wanaishi kama wako Ulaya na Marekani.

Nadhani kimoyomoyo huwa wanawacheka waumini wanaitumia akiba zao kutoa sadaka huku wakijua pesa hiyo inaenda kutumika kwenye maamuzi.

Kuna 'maaskofu' na 'manabii' wanadai kuwa na suluhisho la kila tatizo la waumini. Waongo. Wanachotaka ni fedha tu. Inasikitisha kuona waumini wengi wako too naïve and probably stupid kugundua kutapeli huu.

Kuna sababu kwa nini makanisa yanachipua kama uyoga. Watu wanaona dini ya kikristo ni kama fursa ya kufanyia biashara. Wanahimiza watu wafanye kazi lakini wao hawawezi kushika hata jembe la mkono.
Wanacheza na maandiko to their advantage hasa kiuchumi na kujikweza katika jamii. Nasema revival churches ni mafarisayo wa kizazi kipya. Hawataki kubeba misalaba bali magumu yote wamewaachia waumini wao. Waliopumbazwa!

Si vibaya kuchukua mfano wa Rwanda walioanza kudhibiti upuuzi huu. Kuna ukanjanja sana kwenye huu uongozi wa dini. lazima kuwe na mipaka. Serikali iweke sheria kali kudhibiti makanisa kuenea kama uyoga. Gvt iache kuwadekeza waanzisha makanisa mapya. Haiewezekani kila kukicha linaanzishwa kanisa jipya. Kama kweli nia ni kumwabudu Mungu basi makanisa tunayo ya kumwaga.

Utitiri wa vijikanisa ni kero kubwa mitaani kwa makelele na isitoshe imedhihirika kuwa mengi ni kichaka cha matapeli, wazinzi, walevi, losers, majambazi na hata wauza dawa za kulevya.

Eti akina Mwingira Lusekelo Kakobe Rwakatare, Mwamposa nk nk nao ni viongozi wa dini!!!! Very funny indeed. Kwa nje wanajidai wanahubiri Injili lakini deep inside ni matapeli wanaotumia umaamuma wa waumini kujipatia fedha. Tena nyingi.

Hivi kila muumini akiasi kanisa mama na kuamua kuanzisha kanisa lake binafsi tutakuja tunaipeleka wapi nchi hii. Serikali amkeni. Makanisa sasa yanatosha. Msisajili mengine. Kangi, acha kusajili hivyo vijikanisa bwana. Inatosha.
 
Nataka tuwekane clear simplicity ya kuzika kwa hao wenzetu kwa mtizamo wangu haizingatii dignity ya mtu maana jamaa wanakufunga kwenye mkeka wanakuweka hata kwenye double cabin kama umeshawahifiwa na mtu wa karibu hilo swala la kumkosea dignity marehemu hua linakwaza wafiwa wa karibu sana..sio kila kitu cha watu wengine lazima kiigwe pia wanamkimbiza sana marehemu kwenda kuzika, kutokana na muingiliano wa watu kwenye jamii unakuta hawa ndugu zetu wakija kujumuika kuwazika wakristo wanaleta itikadi za kukimbiza marehemu kaburini rejea mazishi ya pancho latino na Godzilla inakuaga full vurugu...
 
Wagalatia 6:17, Paulo anasema,

Tangu sasa mtu asinitaabishe; kwa maana ninachukua mwilini mwangu chapa zake Yesu.


Luka 13:24Luke 13:24

Jitahidini kuingia katika mlango ulio mwembamba, kwa maana nawaambia ya kwamba wengi watataka kuingia, wasiweze.

Luka 13:25Luke 13:25

Wakati mwenye nyumba atakaposimama na kuufunga mlango, nanyi mkaanza kusimama nje na kuubisha mlango, mkisema, Ee Bwana, tufungulie; yeye atajibu na kuwaambia, Siwajui mtokako;

Luka 13:26Luke 13:26

ndipo mtakapoanza kusema, Tulikula na kunywa mbele yako, nawe ulifundisha katika njia zetu.

Luka 13:27Luke 13:27

Naye atasema, Nawaambia, Siwajui mtokako; ondokeni kwangu ninyi nyote mlio wafanyaji wa udhalimu.

Luka 13:28Luke 13:28

Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje.

Ukristo umevamiwa sana ila mwisho wa siku Mungu atachuja ngano na makapi

HAWA MANABII NA MITUME NDIO WANAOUCHAFUA UKRISTO KWA MIUJIZA FEKI


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sheria ya Dini ya Uislam kuhusu kuzika

Tumefunzwa kumkimbiza Maiti na kumuwahisha katika makazi yake

Hujui kilichokuwa katika bega lako,je umembeba aliebora mbele ya Mola,na ikiwa ni mbora,basi muwahisheni katika makazi yake mazuri,
Na Ikiwa ni muovu mbele ya Mola,Ubaya ulioje kwa nyinyi kumbeba aliekasirikiwa na Mola kwa muda mrefu


Vitu vitatu ni muhimu sana kufanywa haraka kisheria

1)Mtu akitaka kuingia katika Uislam,Basi jambo lifanywe haraka

2)Harusi
3)Mazishi


Uislam hauna makuu Chief

Ila watu wana makuu
Nataka tuwekane clear simplicity ya kuzika kwa hao wenzetu kwa mtizamo wangu haizingatii dignity ya mtu maana jamaa wanakufunga kwenye mkeka wanakuweka hata kwenye double cabin kama umeshawahifiwa na mtu wa karibu hilo swala la kumkosea dignity marehemu hua linakwaza wafiwa wa karibu sana..sio kila kitu cha watu wengine lazima kiigwe pia wanamkimbiza sana marehemu kwenda kuzika, kutokana na muingiliano wa watu kwenye jamii unakuta hawa ndugu zetu wakija kujumuika kuwazika wakristo wanaleta itikadi za kukimbiza marehemu kaburini rejea mazishi ya pancho latino na Godzilla inakuaga full vurugu...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
I concure. ...
Madhehebu mengi mno ya kikristo yame kuwa too commercialized kias kwamba mtu inabidi uwe na uelewa wa Hali ya juu sana kutofautisha ukwel na uongo pamoja na muda wenyewe.....
Fact kwamba dunia tunapita and it's not all about the Benjamins ni wachache sana wa naelewa. .....(the haves with humility)
Pole mkuu kama yamekukuta . .. but it really doesn't matter with time.....
 
Vitabu vya dini vinatutaka kuwa wanyenyekevu. Sio kuwa na kiburi na mbwembwe kama walivyo baadhi ya viongozi wa dini wa kizazi hiki. Ni hodari wa kushiriki misiba ya matajiri lakini ya masikini wanaikwepa.

Nafarijika kwamba Wakristo na Waislamu wote wanamuabudu Mungu mmoja. Ndiyo kwa namna tofauti lakini hilo halipaswi kuwa tatizo kubwa.

Nafurahia zaidi namna Waislamu wengi wanavyofanya mambo yao kwa unyenyekevu mkubwa. Waislamu wapo simple katika mambo yao na hivyo ndivyo dini na mitume wanavyotaka.

Wako simple kwenye kuzika, ndoa, tohara na namna nzima ya maisha yao. Pengine ni kwa sababu wanafahamu zaidi kwamba dunia hii tunapita tu.

Ndani ya Ukristu na baadhi ya Wakristo wengi kuna mbwembwe nyingi. Viongozi wengi wa makanisa wanajikweza sana.
Msingi mkuu wa Ukristu ni kujinyenyekeza kwa Mungu na wanadamu. Lakini sasa Ukristu umeingiwa na kirusi. Mbwembwe za wanaojiita maaskofu, manabii, wachungaji nk nk zinatisha. Badala ya kuwa wachungaji hivi sasa watu hawa wamekuwa walaji wa kondoo ...yaani waumini wao!

Kuna 'maaskofu' wanalindwa kama wafalme. Wanaishi katika nyumba za kifahari mno. Wana mimali ya kutisha. Baadhi wanamiliki ndege na magari ya kifahari mno. Pesa imewekwa mbele sana katika makanisa hasa revival churches na visingizio mbalimbali hutumika hususani Biblia kuhalalisha uovu.
Kifupi viongozi wengi wa revival churches hutumia sadaka za waumini kujinufaisha wao binafsi, wake na au hawara zao na marafiki zao.

Yesu na mitume wanaojifanya kuwahubiri waliishi maisha humble sana. Bwana alihimiza humbleness. Kitu ambacho sikioni kwenye maisha ya hawa viongozi wa makanisa. Viongozi wengi wa dini wamejaa unafiki, majivuno, dharau na wengi hujitenga kabisa na masikini.

Najiuliza hawa 'maaskofu' wanamhubiri Yesu gani? Kwa kweli ni kufuru kufanya biashara kupitia jina hili Takatifu. Wala si haki kuwapumbaza waumini kwa mahubiri yao uongo ili watoe pesa nyingi za sadaka. Viongozi uchwara wa dini huwakumbatia wenye fedha.

Utitiri wa makanisa si jambo la fahari. Watu hawa wajiitao manabii nk, wanafanya biashara. Period! Wanatumia advantage ya matatizo ya watu walio desperate kupata suluhisho la matatizo yao. Shame on them.

Hawa jamaa hawana chembe ya huruma kwani wanawanyonya hata waumini masikini. Wanakula mali za wajane na huwa convince wafuasi wao kutoa hata akiba zao kuwajengea 'maaskofu' nyumba na kujaza mafuta katika gaaa riii zao!! Ama kweli wajinga ndio waliwao!!
Tanzania na Watanzania wengi ni malofa. Lakini bila aibu baadhi ya 'maaskofu' hao wanaishi kama wako Ulaya na Marekani.

Nadhani kimoyomoyo huwa wanawacheka waumini wanaitumia akiba zao kutoa sadaka huku wakijua pesa hiyo inaenda kutumika kwenye maamuzi.

Kuna 'maaskofu' na 'manabii' wanadai kuwa na suluhisho la kila tatizo la waumini. Waongo. Wanachotaka ni fedha tu. Inasikitisha kuona waumini wengi wako too naïve and probably stupid kugundua kutapeli huu.

Kuna sababu kwa nini makanisa yanachipua kama uyoga. Watu wanaona dini ya kikristo ni kama fursa ya kufanyia biashara. Wanahimiza watu wafanye kazi lakini wao hawawezi kushika hata jembe la mkono.
Wanacheza na maandiko to their advantage hasa kiuchumi na kujikweza katika jamii. Nasema revival churches ni mafarisayo wa kizazi kipya. Hawataki kubeba misalaba bali magumu yote wamewaachia waumini wao. Waliopumbazwa!

Si vibaya kuchukua mfano wa Rwanda walioanza kudhibiti upuuzi huu. Kuna ukanjanja sana kwenye huu uongozi wa dini. lazima kuwe na mipaka. Serikali iweke sheria kali kudhibiti makanisa kuenea kama uyoga. Gvt iache kuwadekeza waanzisha makanisa mapya. Haiewezekani kila kukicha linaanzishwa kanisa jipya. Kama kweli nia ni kumwabudu Mungu basi makanisa tunayo ya kumwaga.

Utitiri wa vijikanisa ni kero kubwa mitaani kwa makelele na isitoshe imedhihirika kuwa mengi ni kichaka cha matapeli, wazinzi, walevi, losers, majambazi na hata wauza dawa za kulevya.

Eti akina Mwingira Lusekelo Kakobe Rwakatare, Mwamposa nk nk nao ni viongozi wa dini!!!! Very funny indeed. Kwa nje wanajidai wanahubiri Injili lakini deep inside ni matapeli wanaotumia umaamuma wa waumini kujipatia fedha. Tena nyingi.

Hivi kila muumini akiasi kanisa mama na kuamua kuanzisha kanisa lake binafsi tutakuja tunaipeleka wapi nchi hii. Serikali amkeni. Makanisa sasa yanatosha. Msisajili mengine. Kangi, acha kusajili hivyo vijikanisa bwana. Inatosha.
Kuwa na ukwasi na kuishi kifahari sio dhambi,tatizo linakuja pale ambapo hizo Mali zimepatikana kwa njia zisizo na utakatifu ndani yake,
Ma pastor wengi,hawa wanao weka mabango na matangazo kibao,kwamba uwafate ili upate wokovu,wengi ni wezi tu na mtaperi,dini imekuwa fulsa ya kupiga hela.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sheria ya Dini ya Uislam kuhusu kuzika

Tumefunzwa kumkimbiza Maiti na kumuwahisha katika makazi yake

Hujui kilichokuwa katika bega lako,je umembeba aliebora mbele ya Mola,na ikiwa ni mbora,basi muwahisheni katika makazi yake mazuri,
Na Ikiwa ni muovu mbele ya Mola,Ubaya ulioje kwa nyinyi kumbeba aliekasirikiwa na Mola kwa muda mrefu


Vitu vitatu ni muhimu sana kufanywa haraka kisheria

1)Mtu akitaka kuingia katika Uislam,Basi jambo lifanywe haraka

2)Harusi
3)Mazishi


Uislam hauna makuu Chief

Ila watu wana makuu

Sent using Jamii Forums mobile app
Swadakta
 
Vitabu vya dini vinatutaka kuwa wanyenyekevu. Sio kuwa na kiburi na mbwembwe kama walivyo baadhi ya viongozi wa dini wa kizazi hiki. Ni hodari wa kushiriki misiba ya matajiri lakini ya masikini wanaikwepa.

Nafarijika kwamba Wakristo na Waislamu wote wanamuabudu Mungu mmoja. Ndiyo kwa namna tofauti lakini hilo halipaswi kuwa tatizo kubwa.

Nafurahia zaidi namna Waislamu wengi wanavyofanya mambo yao kwa unyenyekevu mkubwa. Waislamu wapo simple katika mambo yao na hivyo ndivyo dini na mitume wanavyotaka.

Wako simple kwenye kuzika, ndoa, tohara na namna nzima ya maisha yao. Pengine ni kwa sababu wanafahamu zaidi kwamba dunia hii tunapita tu.

Ndani ya Ukristu na baadhi ya Wakristo wengi kuna mbwembwe nyingi. Viongozi wengi wa makanisa wanajikweza sana.
Msingi mkuu wa Ukristu ni kujinyenyekeza kwa Mungu na wanadamu. Lakini sasa Ukristu umeingiwa na kirusi. Mbwembwe za wanaojiita maaskofu, manabii, wachungaji nk nk zinatisha. Badala ya kuwa wachungaji hivi sasa watu hawa wamekuwa walaji wa kondoo ...yaani waumini wao!

Kuna 'maaskofu' wanalindwa kama wafalme. Wanaishi katika nyumba za kifahari mno. Wana mimali ya kutisha. Baadhi wanamiliki ndege na magari ya kifahari mno. Pesa imewekwa mbele sana katika makanisa hasa revival churches na visingizio mbalimbali hutumika hususani Biblia kuhalalisha uovu.
Kifupi viongozi wengi wa revival churches hutumia sadaka za waumini kujinufaisha wao binafsi, wake na au hawara zao na marafiki zao.

Yesu na mitume wanaojifanya kuwahubiri waliishi maisha humble sana. Bwana alihimiza humbleness. Kitu ambacho sikioni kwenye maisha ya hawa viongozi wa makanisa. Viongozi wengi wa dini wamejaa unafiki, majivuno, dharau na wengi hujitenga kabisa na masikini.

Najiuliza hawa 'maaskofu' wanamhubiri Yesu gani? Kwa kweli ni kufuru kufanya biashara kupitia jina hili Takatifu. Wala si haki kuwapumbaza waumini kwa mahubiri yao uongo ili watoe pesa nyingi za sadaka. Viongozi uchwara wa dini huwakumbatia wenye fedha.

Utitiri wa makanisa si jambo la fahari. Watu hawa wajiitao manabii nk, wanafanya biashara. Period! Wanatumia advantage ya matatizo ya watu walio desperate kupata suluhisho la matatizo yao. Shame on them.

Hawa jamaa hawana chembe ya huruma kwani wanawanyonya hata waumini masikini. Wanakula mali za wajane na huwa convince wafuasi wao kutoa hata akiba zao kuwajengea 'maaskofu' nyumba na kujaza mafuta katika gaaa riii zao!! Ama kweli wajinga ndio waliwao!!
Tanzania na Watanzania wengi ni malofa. Lakini bila aibu baadhi ya 'maaskofu' hao wanaishi kama wako Ulaya na Marekani.

Nadhani kimoyomoyo huwa wanawacheka waumini wanaitumia akiba zao kutoa sadaka huku wakijua pesa hiyo inaenda kutumika kwenye maamuzi.

Kuna 'maaskofu' na 'manabii' wanadai kuwa na suluhisho la kila tatizo la waumini. Waongo. Wanachotaka ni fedha tu. Inasikitisha kuona waumini wengi wako too naïve and probably stupid kugundua kutapeli huu.

Kuna sababu kwa nini makanisa yanachipua kama uyoga. Watu wanaona dini ya kikristo ni kama fursa ya kufanyia biashara. Wanahimiza watu wafanye kazi lakini wao hawawezi kushika hata jembe la mkono.
Wanacheza na maandiko to their advantage hasa kiuchumi na kujikweza katika jamii. Nasema revival churches ni mafarisayo wa kizazi kipya. Hawataki kubeba misalaba bali magumu yote wamewaachia waumini wao. Waliopumbazwa!

Si vibaya kuchukua mfano wa Rwanda walioanza kudhibiti upuuzi huu. Kuna ukanjanja sana kwenye huu uongozi wa dini. lazima kuwe na mipaka. Serikali iweke sheria kali kudhibiti makanisa kuenea kama uyoga. Gvt iache kuwadekeza waanzisha makanisa mapya. Haiewezekani kila kukicha linaanzishwa kanisa jipya. Kama kweli nia ni kumwabudu Mungu basi makanisa tunayo ya kumwaga.

Utitiri wa vijikanisa ni kero kubwa mitaani kwa makelele na isitoshe imedhihirika kuwa mengi ni kichaka cha matapeli, wazinzi, walevi, losers, majambazi na hata wauza dawa za kulevya.

Eti akina Mwingira Lusekelo Kakobe Rwakatare, Mwamposa nk nk nao ni viongozi wa dini!!!! Very funny indeed. Kwa nje wanajidai wanahubiri Injili lakini deep inside ni matapeli wanaotumia umaamuma wa waumini kujipatia fedha. Tena nyingi.

Hivi kila muumini akiasi kanisa mama na kuamua kuanzisha kanisa lake binafsi tutakuja tunaipeleka wapi nchi hii. Serikali amkeni. Makanisa sasa yanatosha. Msisajili mengine. Kangi, acha kusajili hivyo vijikanisa bwana. Inatosha.
Umemsahau Gamanywa tapeli mkubwa,
Naunga mkono hoja haya makanisa yafutwe
 
Back
Top Bottom