Wakongo: Taifa Stars imejaa utoto mwingi

popiexo

JF-Expert Member
Oct 26, 2010
742
182
Baadhi ya wachezaji wa DRC wamesema Tanzania "Taifa Stars" ilistahili kucheza nusu fainali, lakini wachezaji wake wamejaa utoto mwingi na hawajali kazi yao katika michuano ya bonde la mto nile.
"Nimeona mechi ya Tanzani, wachezaji wanapoteza pasi halafu hawajali, wanafungwa goli wanatabasamu"
"Unafungwa bao tano hata kadi ya njano hupewi kwa kucheza rafu kupunguza kasi yao, vijana wenu wamejaa utoto mwingi sana, hawajui thamani ya mpira"alisema kiungo Kasongo Ngandou, anaechezea TP Mazembe.

Source: Mwananchi.

Hii ni kweli hatuna wachezaji ndio maana wanashindwa kucheza ulaya kila wakienda wanarudi, mara ooh nimekumbuka nyumbani
 
Tutafia uwanjani!Kwani wao wanamiguu mingapi?Minne?Wanacheza kumi na mbili?Ndio misemo yetu,tukiingia uwanjani hakuna kuzimia wala nini,mabao tu wanakung'utwa.Hao ndio watz na majigambo yao!
 
Bakongoman bamesema muzuri juu vile batanzania bamejaa butoto, kutomboka bure na kupenda wabibi na mafie. Mupira hawajui inabidi waifanye nguvu sana.
 
Back
Top Bottom