Wako wapi wagunduzi wa teknolojia za Kitanzania?

Lucas

JF-Expert Member
Dec 3, 2011
2,457
1,108
Nimeangalia TBC na kumuona Mtanzania mmoja Emmanuel Bukuku ambaye amebuni mashine yenye uwezo wa kuita samaki, hongera kwake na vizuri.

Ila huyu jamaa amenifanya nikakumbuka watanzania kadhaa ambao sijui ujuzi wao na ubunifu viliishia wapi? serikali iliwasapoti vipi??

Namkubuka kaka mmoja Rogers Sifelani huyu alitengeneza helcopter na kuruka nayo kutoka arusha hadi Babati miaka ya 90, aliishia wapi?i

Kuna kijana mmoja miaka ile alitengeneza kituo cha redio sijui aliishia wapi?

Nyumbu na magari yao waliishia wapi?

wale na wanafunzi wa Veta BUguruni walitengeneza Gari sijui wako wapi?


hebu tukumbushe na wengine na kama unajua wako wapi hawa kwa sasa utujulishe.
 
Nimeangalia TBC na kumuona Mtanzania mmoja Emmanuel Bukuku ambaye amebuni mashine yenye uwezo wa kuita samaki, hongera kwake na vizuri.

Ila huyu jamaa amenifanya nikakumbuka watanzania kadhaa ambao sijui ujuzi wao na ubunifu viliishia wapi? serikali iliwasapoti vipi??

Namkubuka kaka mmoja Rogers Sifelani huyu alitengeneza helcopter na kuruka nayo kutoka arusha hadi Babati miaka ya 90, aliishia wapi?i

Kuna kijana mmoja miaka ile alitengeneza kituo cha redio sijui aliishia wapi?

Nyumbu na magari yao waliishia wapi?

wale na wanafunzi wa Veta BUguruni walitengeneza Gari sijui wako wapi?


hebu tukumbushe na wengine na kama unajua wako wapi hawa kwa sasa utujulishe.

Yote kweli ndugu. Bahati mbaya sana viongozi wetu hawajui kulea maendeleo pale yanapoanza kuchipua. Mie nakumbuka gunduzi mbili.
1, Bwana mmoja (nimemsahau jina) katika miaka ya 70 hivi alibuni na kutumia mabomba ya mianzi. Sijui aliishia wapi na ugunduzi wake ambao ungesaidia sana kilimo cha umwagiliaji.
2. Juzijuzi tu miaka ya 90 kikundi cha wanachuo wa DIT(Chuo cha Ufundi dsm) walibuni kifaa cha kutambua uchakachuaji wa transfoma za umeme pindi mtu anapoanza kuondoa mafuta kwenye transfoma na habari kupelekwa makao makuu TANESCO muda huohuo uingiliaji wa transfoma unapofanyika. Hii ingesaidia sana kuokoa kuungua kwa transfoma.Cha ajabu TANESCO haikushangilia ugunduzi huu walikaa kimya mpaka leo.

Viongozi wa nchi hii wamebaki kushabikia teknolojia za watu wa nje na kusahau kwamba hata hapa kwetu teknolojia zinaanza kuchipuka. Pamoja na hayo kwa bahati nzuri tunayo COSTECH, ambayo inajitahidi kulea vipaji vya ubunifukupitia DTBI (Dar Teknohama Business Incubator). Taasisi hii imemlea mgunduzi wa mashine ya kutengeneza sabuni, kijana mbunifu wa teknolojia ya habari ambaye anabuni kitu huyu kijana anachokiita TOVS(Tanzania On-line Voting System)

Yetu macho!
 
Nimeangalia TBC na kumuona Mtanzania mmoja Emmanuel Bukuku ambaye amebuni mashine yenye uwezo wa kuita samaki, hongera kwake na vizuri.

Ila huyu jamaa amenifanya nikakumbuka watanzania kadhaa ambao sijui ujuzi wao na ubunifu viliishia wapi? serikali iliwasapoti vipi??

Namkubuka kaka mmoja Rogers Sifelani huyu alitengeneza helcopter na kuruka nayo kutoka arusha hadi Babati miaka ya 90, aliishia wapi?i

Kuna kijana mmoja miaka ile alitengeneza kituo cha redio sijui aliishia wapi?

Nyumbu na magari yao waliishia wapi?

wale na wanafunzi wa Veta BUguruni walitengeneza Gari sijui wako wapi?


hebu tukumbushe na wengine na kama unajua wako wapi hawa kwa sasa utujulishe.
Wameshaongezeka wengine kama:
Transistor:
Mbunifu wa vifaa mbalimbali vya electronics

Wicalumtata:
Bingwa wa kuunda subwoofer
 
mgunduzi wa gari pekee "kapalata"
yule wa helikopta
na kuna gunduzi nyingi sana zingine zimelala wanasiasa wanazika hizi gunduzi na kuziabudu za wazungu
 
Tatizo kuu ni hiki chama kilichopo madarakan...kuendeleza uwezo wa watu kwao nikujipalia makaa ya mawe kuondolewa madarakan...wewe angalia tu sehemu wanapotawala utapata majibu...
Hilo ndio tatizo kuu
 
Back
Top Bottom