Wakinga wote mapembelo vavene!

Wakinga wote mapembelo vavene!

Tuacheni wakinga tupumue jamani kwani tumewakosea mini aaaagrr tukijituma kutafuta fedha na tukafanikiwa mnasema wachawi tunaua ndugu zetu end endeleeni kubwabwaja sisi ni kazi tu nani kakwambia lazima uwe na elimu ili ufanikiwe? acheni mawazo mgando
 
Huwezi amini ushirikina kama wewe siyo mshirikina. Great thinker una-conclude kiwango cha ushirikina wa kabila kwa kulinganisha makabila kutoka wilaya mbili tu???. Makete vs Handeni. you must be joking!!!!.

Hilo la USHIRIKINA @eastafrican eagle ame declare interest mapema, inawezekana anaongea kitu ambacho ana uhakika nacho.
 
Unashangaa nini Tajiri kama Wanyama aliyekuwa na wanyama Hotel Kariakoo na magorofa kibao kako pamoja na utajiri woooote alikuwa hajajenga kwao maana hakukuwa na mtu anayeishi huko maana ndugu karibuni wooote alishawamaliza,alipokufa ilibidi kwanza wavute mda ikajengwa nyumba faster ndani ya wiki 2 ndio akaenda kuzikwa kwao
watoto wa mwakipande na mseketwa utawaweza?
 
Ukiachana na umaarufu wa CHUO CHA UALIMU TANDALA,HOSPITALI MAARUFU YA IKONDA labda labda na umaarufu wa mganga wa kienyeji dr.MWAKIPANDE na nyumbani kwa kina Deo Filikunjombe Wakinga wa MAKETE wapo taabani kwa umaskini ulio kidhiri,'KILA KITU WAO NI MWALIMI TU HATA KAMA UNAWADANGANYA,watu hawa wa makete ambao asilimia kubwa ni akina SANGA na MBILINYI hawajui cha kufanya ili umaskini angalau upungue kwao,Ukipita maeneo ya Masisiwe,Ikete,Maliwa,Sunji,LUPILA,Tandala,Lupalilo,Mago,Kasinga,Ndulamo,Iwawa,Idanganya,Makete Junction,Ivalalila ,BULONGWA na kwengineko MAKETE Unaweza ukadhani Watanzania Maskini ZAidi wanapatikana huku,Baada ya sekeseke la ukimwi kuwanyanyasa kwa muda mrefu sasa angalau Presure imepungua ila vijana wanapakimbia kabisa MAKETE hawapa taki kabisa kwasababu huwezi kuwa na hela na ukaishi MAKETE HALI NI MBAYA.
Arthi ya MAKETE inarutuba inayo kosekana sehemu kubwa hapa Duniani lakini Serekali ipo ipo tu,kule Mahindi,NGANO,SHAIRI,MTAMA,ALIZETI VIAZI,na mazao ya MIti yanakubali ile mbaya lakini mpaka leo tarehe 27/11/2013 MAKETE hawajapata Mbolea ya RUZUKU.Madini kila kona kule lakini WAKINGA ni maskini asikuambie mtu.HUku UKINGANI maji si ya tabu kabisa lakini kilimo cha umwagiliaji hakijafika huku kabisa ninahisi haya ni maajabu,Na watu wa huku wanakijua zaidi kilimo cha jembe la mkono katika karne hii ya 21.

MY TAKE:RAFIKI YANGU NAPE HEBU TUAMBIE KWANINI WAKINGA NI MASKINI!
MMELIONGOZA JIMBO HILO KWA MIAKA 50 SASA JE MNAJIPYA LA KUTUFANYIA WATANZANIA WA MAKETE!

tatizo lao ni barabara mbovu
 
Ukiachana na umaarufu wa CHUO CHA UALIMU TANDALA,HOSPITALI MAARUFU YA IKONDA labda labda na umaarufu wa mganga wa kienyeji dr.MWAKIPANDE na nyumbani kwa kina Deo Filikunjombe Wakinga wa MAKETE wapo taabani kwa umaskini ulio kidhiri,'KILA KITU WAO NI MWALIMI TU HATA KAMA UNAWADANGANYA,watu hawa wa makete ambao asilimia kubwa ni akina SANGA na MBILINYI hawajui cha kufanya ili umaskini angalau upungue kwao,Ukipita maeneo ya Masisiwe,Ikete,Maliwa,Sunji,LUPILA,Tandala,Lupalilo,Mago,Kasinga,Ndulamo,Iwawa,Idanganya,Makete Junction,Ivalalila ,BULONGWA na kwengineko MAKETE Unaweza ukadhani Watanzania Maskini ZAidi wanapatikana huku,Baada ya sekeseke la ukimwi kuwanyanyasa kwa muda mrefu sasa angalau Presure imepungua ila vijana wanapakimbia kabisa MAKETE hawapa taki kabisa kwasababu huwezi kuwa na hela na ukaishi MAKETE HALI NI MBAYA.
Arthi ya MAKETE inarutuba inayo kosekana sehemu kubwa hapa Duniani lakini Serekali ipo ipo tu,kule Mahindi,NGANO,SHAIRI,MTAMA,ALIZETI VIAZI,na mazao ya MIti yanakubali ile mbaya lakini mpaka leo tarehe 27/11/2013 MAKETE hawajapata Mbolea ya RUZUKU.Madini kila kona kule lakini WAKINGA ni maskini asikuambie mtu.HUku UKINGANI maji si ya tabu kabisa lakini kilimo cha umwagiliaji hakijafika huku kabisa ninahisi haya ni maajabu,Na watu wa huku wanakijua zaidi kilimo cha jembe la mkono katika karne hii ya 21.

MY TAKE:RAFIKI YANGU NAPE HEBU TUAMBIE KWANINI WAKINGA NI MASKINI!
MMELIONGOZA JIMBO HILO KWA MIAKA 50 SASA JE MNAJIPYA LA KUTUFANYIA WATANZANIA WA MAKETE!

Uko Subjective Mkuu na Sijui vigezo vp umetumia kuja na hitimisho dhalilishi kama hilo kwa wanamakete pamoja na changamoto ulizoziainisha lkn yapo mengi mazuri unapotembelea vijiji husika kwa mfano kijiji cha Bulongwa Kina Umeme, Nyumba za Kisasa na maisha kwa ujumla ya wakazi wa hapo ni mazuri tu......Je umewahi muona wapi mkinga kawa ombaomba pamoja na umasikini wake? Ni lini umesikia Makete tunaomba msaada wa chakula serikalini kisa tumepatwa na njaa? UMETUMWA WEWE NA KWA KIFUPI TEMBELEA NA MIKOA MINGINE KAMA DODOMA, SINGIDA, MANYARA, SHINYANGA, RUKWA NDO UJE NA HITIMISHO HILO
 
Mkuu sijui umetumia kigezo gani kuzungumzia umaskini wa wakinga waishio makete. Generally huwa tunaangalia malazi, chakula na mavazi. Umeangalia nyumba za makete zilivyojengwa kwa tofari za kuchumwa na kuezekwa bati? Ulishaona mbavu za mbwa makete? Ulishasikia makete wanaomba msaada? Tumetembea sehemu mbali mbali tanzania hii makete ni moja ya wilaya zenye security kubwa ya chakula na nyumba bora na za kudumu. Msiende makete kipindi cha vumbi mkaona watu wamechafuka mkaanza kusema watu ni maskini! Kama kweli umepita huko umeona nyumba za miaka ile zilizopo ikonda, lupalilo, mago, na bulongwa? Unaweza kulinganisha na zile za handeni au dodoma?? Tena huko imepita lami kabisa, hawana shida ya usafiri. Vijana wengi wanaondoka kule kwa sababu population ya wilaya ni ndogo hivyo mzunguko wa hela unakuwa mdogo na kila mtu ana asili ya biashara. Atamuuzia nani? Msag'hag'he khavele isyomwiveg'ha!
 
Uko Subjective Mkuu na Sijui vigezo vp umetumia kuja na hitimisho dhalilishi kama hilo kwa wanamakete pamoja na changamoto ulizoziainisha lkn yapo mengi mazuri unapotembelea vijiji husika kwa mfano kijiji cha Bulongwa Kina Umeme, Nyumba za Kisasa na maisha kwa ujumla ya wakazi wa hapo ni mazuri tu......Je umewahi muona wapi mkinga kawa ombaomba pamoja na umasikini wake? Ni lini umesikia Makete tunaomba msaada wa chakula serikalini kisa tumepatwa na njaa? UMETUMWA WEWE NA KWA KIFUPI TEMBELEA NA MIKOA MINGINE KAMA DODOMA, SINGIDA, MANYARA, SHINYANGA, RUKWA NDO UJE NA HITIMISHO HILO

Mapembelo binamu! Obwana ojo ajag'hile enzela, ingie mukhesotu. Makete sasa hivi kukuta nyumba ya nyasi ni nadra sana, sasa hivi hata umeme wa tanesco usipofika watu wanavuta solar tena vijijini kabisa! Ikipita lami kule watu wakawa na uhakika wa kusafiri mwaka mzima wakinga wote watahamishia nyumba zao makete. Eti kilimo cha umwagiliaji, sasa mle lwamadovela utamwagiliaje?
 
Unashangaa nini Tajiri kama Wanyama aliyekuwa na wanyama Hotel Kariakoo na magorofa kibao kako pamoja na utajiri woooote alikuwa hajajenga kwao maana hakukuwa na mtu anayeishi huko maana ndugu karibuni wooote alishawamaliza,alipokufa ilibidi kwanza wavute mda ikajengwa nyumba faster ndani ya wiki 2 ndio akaenda kuzikwa kwao
watoto wa mwakipande na mseketwa utawaweza?

Kwa mwakipande na useketwa hata makabila mengine yanaenda sana tu! Si huwa mnatuulizi tukiwa kwenye mabasi njia panda ya lupila? We unadhani nikikutana na mchaga, basi ya makete anauliza njia panda ya useketwa sitajua anaenda kujikoki? Huyo wanyama unayesema ndiye aliyejenga daraja la kwenda kijijini kwao kutokea bulongwa kwa hela yake. Ulitaka akajenge ghorofa luwumbu?
 
Ndeeti nye Vakheenga vajiango, mtoa mada watoto wa mjini tunamuita KAVAUKA! Kataja saaana vijiji vya makete lakini haeleweki hoja yake nini!
Anataka kuzungumzia umaskini wa Makete au Umaskini wa WAKINGA!?
Kama ni umaskini wa Makete sijui ametumia vigezo gani kulinganisha na wilaya zote za Nchi hii, lakini kama ni ishu ya kabila letu hakuna wakinga maskini.

Watangulizi wametangulia kukuuliza, umewahi wapi kumwona Mkinga ombaomba? Ok labda huyu bado, je tangia uhuru au hata kabla imewahi au kusoma makete wameshawahi kuomba chakula cha msaada?
Hapo wanamakete tunajiuliza hasa vigezo ulivyotumia kupata umaskini wetu, kinyume na hapo unakosa tofauti na wenye dhana kuwa Wakinga ni wachawi!!

Kila mtu sasa anafahamu kuwa kati ya makabila tajiri kabisa hapa Tanzania Wakinga wanahesabiwa pia, sasa sijui ni siasa, wivu au kitu gani kinakusukuma kusema Makete au Wakinga ni maskini!!

Kihusu jembe la mkono, labda mwandishi utakuwa huifahamu kabisa Makete na vijiji ulovyovitaja umesomewa tu, kwa jiografia ya Makete huwezi kulima na trekta, Makete 90% mi milima mikali tu, sasa hapo unalimaje na trekta, sehemu ambazo hata ng'ombe mwenyewe anataabika kulima!!?

Mwandishi kama ni Mambo ya kisiasa basi acha kuwasema Wakinga kabisa maana nomeona umehoji kitu kwa Nape, binafsi ni mwenyeji wa Unenamwa Bulongwa Makete, na ki ukweli sipendi na sitaki utawala wa Ccm Makete, lakini tukiacha unafki Wakinga ni wataftaji wa kiwango cha juu sana, na wasioweza kufuata nyayo huja na lawama nyiiingi kama zako!!

Ongolove alenoowe twe vakheenga!! Erasto Tweve.
 
karibu numbu mkuu, unapenda mbichi au za kuchemsha

Khwawe twilya amajavo. Huyu jamaa yako naôna amekimbia. Tulitaka atueleze ni kijiji gani alichopita makete akaona anaweza kulima kwa trekta? Ni wapi alipokosa miti ya mbao akiwa makete? Karibu milima yote sasa hivi ina miti isipokuwa kwenye vyanzo vya maji. Ni mkinga gani ambaye ni omba omba mjini? Kule tunatumia subsistence farming na kila mtu anatafuta kwa hali na mali ndio maana wakiingia mjini huwa hawakubali kuishiwa kirahisi kwani wanajua kilimo cha kule kilivyo. Ukikutana na mwanamke wa kikinga ukamkabidhi biashara wewe subiri kuhesabu faida tu!
 
Mapembelo binamu! Obwana ojo ajag'hile enzela, ingie mukhesotu. Makete sasa hivi kukuta nyumba ya nyasi ni nadra sana, sasa hivi hata umeme wa tanesco usipofika watu wanavuta solar tena vijijini kabisa! Ikipita lami kule watu wakawa na uhakika wa kusafiri mwaka mzima wakinga wote watahamishia nyumba zao makete. Eti kilimo cha umwagiliaji, sasa mle lwamadovela utamwagiliaje?

Jamaa hakufanya utafiti wa kutosha,au hajafika sehemu tofauti tofauti za nchi yetu. Makete inapata mvua kufuata kalenda ya Mungu, sasa umwagiliaji wa nini? Wanamwagilia wasio na mvua. Makete kuna chakula cha kuwatosha mwaka mzima ndani ya wilaya yao.Karibu 98% ya nyumba za vijijini ni za bati,kama ni elimu,naamini mtoa mada angeangalia Wizara ya elimu wanasema nini. Makete iko juu vizuri sana,wakinga/wawanji/wamagoma/wamahanji wanasoma kwa bidii kweli.

Matatizo yapo, jogorafia ya Makete inafanya Makete kuwa na outlet/inlet zaidi ya moja. Ndio maana watu wakipita Njombe mpaka Makete wanadhani wamefika Makete yote,kumbe kuna njia ya Uyole Makete au Chimala Matamba Makete,au Ruaha ikuwo Makete,au Kipengere Lupila na hii inayojulikana ya Njombe Makete.

Ukimwi upo kila mahali Tanzania,ila Ukimwi wa Makete watu waliufanyia biashara ndio maana ikaonekana hata miti ina ukimwi. Kama ni huduma za afya, Makete kuna hospitali kubwa tatu za kiwango cha Kitaifa sio vituo vya afya, ipo Ikonda (RC), ipo ya Wilaya na ipo Bulongwa(KKKT), zipo shule za sekondari za kutosha,vyuo vya kati vipo kama VETA,NURSING,UALIMU viwili,DENTIST BULONGWA, usafiri wa mabasi/malori upo kila siku. Umeme wa tanesco na watu binafsi upo.

Barabara ya lami haipo,kama ambavyo LindiKigoma/Bukoba/Rukwa ilikuwa haijaunganishwa na lami kwa miaka dahali,uwanja wa ndege haupo.

Umeme ukienea wilaya nzima yafuatayo yatatokea, Makete itaweza kuwa na viwanda vya fenicha kila kata,inaweza kusindika maziwa kwa sababu hali ya hewa inaruhusu kufuga,inaweza kulima maua. Inaweza kufungua kiwanda cha karatasi,matunda yatasindikwa kule,hata maji ya kunywa tutasafirisha kuja kwenu. Makete kutajengwa recreation camps sababu hali ya hewa ni bomba.

Ushirikina/umaskini/ukosefu wa elimu hata hapa Ilala/Kinondoni/Temeke upo bila kujali umbali toka Ikulu. kuna watu hawajui kusoma hapa hapa Ubungo,kuna watu hawapati chakula hata kama wapo Tandale kwenye soko la vyakula,pale Kigamboni kuna watu hawana maji hata kama wako beach.

Inaonekana wakinga walikubamiza ww mtoa mada.
 
aah nyee bela hege ipa,wabena kiki
muse uku vakuboma mumuone huyu
 
umaskini ni kwa Tanzania nzima,ebu tueleze kwa evidence ni jimbo gani ambalo halina maskini hata mmoja?,halaf kusema kabila la watu pia hapo umeteleza,kama ungekuwa great thinker ungeongelea tatizo la umaskin kwenye eneo na sio kutaja kabila manake nna iman hapo makete na makabila mengine pia yapo!,kwa kutaja kabila umeonyesha ni jinsi gan ulivyo na simple mind!
DONT panic nimeizungumzia makete tu huko kwingineko nitakuzungumzia siku nyingine any way kama unajua umaskini ni tanzania nzima kwanini unaendelea kuishabikia CCM chanzo cha umaskini wako
 
Jamaa hakufanya utafiti wa kutosha,au hajafika sehemu tofauti tofauti za nchi yetu. Makete inapata mvua kufuata kalenda ya Mungu, sasa umwagiliaji wa nini? Wanamwagilia wasio na mvua. Makete kuna chakula cha kuwatosha mwaka mzima ndani ya wilaya yao.Karibu 98% ya nyumba za vijijini ni za bati,kama ni elimu,naamini mtoa mada angeangalia Wizara ya elimu wanasema nini. Makete iko juu vizuri sana,wakinga/wawanji/wamagoma/wamahanji wanasoma kwa bidii kweli.

Matatizo yapo, jogorafia ya Makete inafanya Makete kuwa na outlet/inlet zaidi ya moja. Ndio maana watu wakipita Njombe mpaka Makete wanadhani wamefika Makete yote,kumbe kuna njia ya Uyole Makete au Chimala Matamba Makete,au Ruaha ikuwo Makete,au Kipengere Lupila na hii inayojulikana ya Njombe Makete.

Ukimwi upo kila mahali Tanzania,ila Ukimwi wa Makete watu waliufanyia biashara ndio maana ikaonekana hata miti ina ukimwi. Kama ni huduma za afya, Makete kuna hospitali kubwa tatu za kiwango cha Kitaifa sio vituo vya afya, ipo Ikonda (RC), ipo ya Wilaya na ipo Bulongwa(KKKT), zipo shule za sekondari za kutosha,vyuo vya kati vipo kama VETA,NURSING,UALIMU viwili,DENTIST BULONGWA, usafiri wa mabasi/malori upo kila siku. Umeme wa tanesco na watu binafsi upo.

Barabara ya lami haipo,kama ambavyo LindiKigoma/Bukoba/Rukwa ilikuwa haijaunganishwa na lami kwa miaka dahali,uwanja wa ndege haupo.

Umeme ukienea wilaya nzima yafuatayo yatatokea, Makete itaweza kuwa na viwanda vya fenicha kila kata,inaweza kusindika maziwa kwa sababu hali ya hewa inaruhusu kufuga,inaweza kulima maua. Inaweza kufungua kiwanda cha karatasi,matunda yatasindikwa kule,hata maji ya kunywa tutasafirisha kuja kwenu. Makete kutajengwa recreation camps sababu hali ya hewa ni bomba.

Ushirikina/umaskini/ukosefu wa elimu hata hapa Ilala/Kinondoni/Temeke upo bila kujali umbali toka Ikulu. kuna watu hawajui kusoma hapa hapa Ubungo,kuna watu hawapati chakula hata kama wapo Tandale kwenye soko la vyakula,pale Kigamboni kuna watu hawana maji hata kama wako beach.

Inaonekana wakinga walikubamiza ww mtoa mada.
Barabara ya lami sasa ipo
 
Back
Top Bottom