tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
Wasanii Diamond Platinum, Rayvany na Ommy Dimpoz wamekuwa kivutio katika mkutano wa kampeni za chama cha Mapinduzi (CCM) zinazofanyika mkoani Mbeya.
Soma pia: Rais Samia kugawa bahasha kwa watumbuizaji ni sawa na kununua watu, anatuonesha hakubaliki bila 'zawadi'?
Hata hivyo, wakati mastaa hao wa muziki nchini wakiingia jukwaani leo Alhamisi, Septemba 4, 2025 wananchi waliwashangilia wanamuziki hao katika viwanja vya Old Airport jijini japa, huku askari Polisi na maofisa itifaki wa CCM wakionesha shughuli ya kuwapanga ili kuwa salama.
Wasanii hao na wengine wapo katika msafara wa ziara ya mgombea Urais wa CCM, Samia Suluhu Hassan mkoani Mbeya kwa ajili ya kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Ommy Dimpoz ndiye alitangulia kabla ya wawili hao kufuata jukwaani akipiga baadhi ya ngoma zake, kisha Rayvany na baadaye Diamond kuhitimisha.
Wakati wakipanda na kufanya shoo zao, wananchi ambao wamejitokeza kwenye viwanja hivyo, mizuka ilionekana kupanda kwa wakazi hao kufuatia ngoma za wasanii hao zilizobamba zamani na sasa. Hadi sasa bado shughuli zinazoendelea kwa wasanii kuendelea kutoa burudani kwa wananchi wakati wakimsubiri mgombea huyo aliyetua tangu jana Septemba 3.
Soma pia: Rais Samia kugawa bahasha kwa watumbuizaji ni sawa na kununua watu, anatuonesha hakubaliki bila 'zawadi'?
Hata hivyo, wakati mastaa hao wa muziki nchini wakiingia jukwaani leo Alhamisi, Septemba 4, 2025 wananchi waliwashangilia wanamuziki hao katika viwanja vya Old Airport jijini japa, huku askari Polisi na maofisa itifaki wa CCM wakionesha shughuli ya kuwapanga ili kuwa salama.
Wasanii hao na wengine wapo katika msafara wa ziara ya mgombea Urais wa CCM, Samia Suluhu Hassan mkoani Mbeya kwa ajili ya kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka huu. Ommy Dimpoz ndiye alitangulia kabla ya wawili hao kufuata jukwaani akipiga baadhi ya ngoma zake, kisha Rayvany na baadaye Diamond kuhitimisha.
Wakati wakipanda na kufanya shoo zao, wananchi ambao wamejitokeza kwenye viwanja hivyo, mizuka ilionekana kupanda kwa wakazi hao kufuatia ngoma za wasanii hao zilizobamba zamani na sasa. Hadi sasa bado shughuli zinazoendelea kwa wasanii kuendelea kutoa burudani kwa wananchi wakati wakimsubiri mgombea huyo aliyetua tangu jana Septemba 3.