Wakili Jebra Kambole adai Erick Kabendera hajawahi kuhojiwa kuhusu utakatishaji fedha na kukwepa Kodi

Beatrice Kamugisha

JF-Expert Member
May 18, 2019
762
6,980
Hi kidogo inatia mashaka na inaleta sintofahamu hasa kwa mahakama zetu na ofisi ya DPP, mtuhumiwa alihojiwa mbele ya wakili wake kuhusu makosa ya mtandao na kufungwa kwa maelezo. Lakini anatikishwa mahakamani kwa makosa ya kukwepa Kodi na kutakatisha fedha, je hizo fedha ametakatisha lini na kwanini hakuhojiwa kuhusu tuhuma hizo?

DPP Hadi anaandika hizi charge alisoma Nini Kama siyo maelezo ya mtuhumiwa? Kama maelezo ya mtuhumiwa hayana kipengele Cha kukwepa Kodi wala kutakatisha fedha kuna umuhimu gani wa watuhumiwa kuendelea kuhojiwa? Kwanini wasiwe wanakamatwa na DPP anawafungulia mashtaka anayohisi yanampendeza?

Kwa upande wa mahakama, watu wamejazwa magerezani kwa kunyimwa dhamana lakini bado tu mahakama haitaki kushtuka kutoka usingizini, watu wanateseka bila hata hatia huko magerezani kisa tu yupo mtu mmoja ambaye ofisi yake imeshindwa kusimamia haki na kuwalaza watu ndani huku yeye akilipwa mshahara na Kodi za wananchi.

Ifike mahali wasomi wetu mtambue kiwango kilekile mnachotumia kuwatesa waliowasomesha ndicho mtakachoteswa nacho ninyi na vizazi vyenu.

Mnamweka mtoto wa watu ndani huku mama yake mgonjwa akiwa anaangaika mkiamini kwamba mtafanikiwa ila mnachuma laana. Ipo siku damu na machozi ya Hawa mnaowatesa zitasimama Kati yetu ndipo mtatambua Bora kuishi bila kazi kuliko kutumia kazi yako kuwanyanyasa wengine.

Unahojiwa uraia unafunguliwa mashtaka ya uhujumu uchumi sijui utakatishaji fedha kweli? Kwamba utakatishaji fedha mliuona kwenye pasipoti yake au kwenye cheti chake Cha kuzaliwa?

No no no no no no no no, kuna watu wanatumika sivyo.
 
Hovyo kabisa hawa watu!!!

EBOG5IpWwAA6737.png
 
Hovyo kabisa hawa watu!!!
Kabisa Mkuu Salary Slip

Tulimsikiliza wenyewe Kamanda Mambosasa, akiongea kwenye Press. Conference, akielezea Umma wa watanzania kuwa wanamshikilia Kabendera wakimhoji kuhusu utata wa.uraia wake, na hizo tuhuma nyingine hakuzitaja

Iweje wamfikitishe mahakamani na kumsomea mashitaka mapya ya kujihusisha na magenge ya kihalifu, utakatishaji pesa na ukwepaji kodi??

Hakika dunia hivi sasa inajua namna ambavyo Polisi wa nchi hii wanavyowabambikia kesi raia wasio na hatia!

Tunapolalamika watanzania kuwa Jeshi la Polisi nchini linatumika na watawala, ushahidi "beyond reasonable doubt" ni huu wa kesi ya mwandishi Kabendera!
 
Aisee! Haya mambo ya raia ya kupakaziwa mikesi ya ajabu ajabu na kuwekewa vikwazo kutokana na kutofautiana na utawala kifikra nilizoea kuyasikia sikia tu kwenye vyombo vya habari vya kimataifa yakiwakumba wanaharakati wa huko ughaibuni, sasa Tanzania yangu ni nini tena kimeisibu!!

Tunakoelekea itakuwa vigumu kuimba ule wimbo wa kizalendo..."Taanzaniaa, Tanzaniaaa...Nakupenda kwa moyo..."

Pole kwa mama Erick Kabendera, maana lazima anapitia magumu kwa sasa...
 
Asante sana kwa kuleta hii andiko, nakumbuka mambo sasa alipokuwa anaongea kwanini wanamusikiria huyu mwandishi alisema issue ni uraia wake, na akaulizwa si hio ni kazi ya uhamiaji akofoka kwa ukali na kusema jeshi la polisi liko na uwaja pana wa kufanya kazi, hakutaja hii issue ya kukwepa kodi, kuwa na mangenge na kuhujumu uchumi, swali kuu ni hli, je DPP KATOA WAPI HAO MASHITAKA???????lakini pale unapomutesa binadamu wenzako, kumbuka kuna aliye juu ya yote na siku yaja wakati mungu atasema, ENOUGH IS ENOUGH
 
Kwa utaratibu huu polisi watawaburuza sana ata kwa uelewa wangu wa sheria 101 polisi awezi kumuhoji mtu bila ya mwanasheria wake kuwepo unless mtuhumiwa achague yeye mwenyewe, let alone kumuwekea charges ambazo ajamsomea na wala mwanasheria wake kuzijua

Haki ya kuweko kwa mwanasheria kwenye interrogation sio favour eti polisi waamue wampe au wamnyime mtu that is a client ‘claim right’ ni yalazima katika kulinda maslahi yake.

Wewe unamteja ambae hajawahi ata hojiwa kuhusu hizo charges, wewe mwenyewe hujui ata details za hizo charges za mteja wako. Lakini unaenda mahakamani unaafiki tu kisa charges zenyewe hazina bail.

Ingekuwa nchi za wenzetu hell will break loose, siku hiyo hiyo ungeona mwanasheria keshafungua kesi ya police misconduct etc na mambo ya kunajisi sheria.

Wanafanya hivi because they get away easily kama ile ndio respond ya nwanasheria wake.
 
Aisee! Haya mambo ya raia ya kupakaziwa mikesi ya ajabu ajabu na kuwekewa vikwazo kutokana na kutofautiana na utawala kifikra nilizoea kuyasikia sikia tu kwenye vyombo vya habari vya kimataifa yakiwakumba wanaharakati wa huko ughaibuni, sasa Tanzania yangu ni nini tena kimeisibu!!

Tunakoelekea itakuwa vigumu kuimba ule wimbo wa kizalendo..."Taanzaniaa, Tanzaniaaa...Nakupenda kwa moyo..."

Pole kwa mama Erick Kabendera, maana lazima anapitia magumu kwa sasa...
Hivi tatizo liko wapi? kama DCI kakusanya ushahidi wa kutosha na kaupeleka kwa DPP ambaye naye kajiridhisha kwamba mtuhumiwa amefanya makosa hayo na hivyo kumpeleka mahakamani kujibu tuhuma hizo tatizo liko wapi? kwa nini tusingojee kuona ushahidi ukiwekwa mezani na mahakama aimue?
 
JPM wanted him dead period
Hata mimi, huwezi mtukana mkuu wa nchi tena nje ya mipaka ya nchi afu watu wakuchekeechekee tu, kwa mujibu wa katiba, Rais kama mkuu wa nchi ndiye nembo au alama ya Taifa nje ya mipaka ya Tanzania hivyo kumtukana Rais nje ya mipaka ni kulituka Taifa, wamemstahi sana aisee.
 
Hivi tatizo liko wapi? kama DCI kakusanya ushahidi wa kutosha na kaupeleka kwa DPP ambaye naye kajiridhisha kwamba mtuhumiwa amefanya makosa hayo na hivyo kumpeleka mahakamani kujibu tuhuma hizo tatizo liko wapi? kwa nini tusingojee kuona ushahidi ukiwekwa mezani na mahakama aimue?
Alafu Jumapili kama sio Ijumaa uko katika nyumba za ibada eti unasali na si ajabu wewe ukawa ndio wale wa kusema,"bwana Yesu asifiwe".
 
Hata mimi, huwezi mtukana mkuu wa nchi tena nje ya mipaka ya nchi afu watu wakuchekeechekee tu, kwa mujibu wa katiba, Rais kama mkuu wa nchi ndiye nembo au alama ya Taifa nje ya mipaka ya Tanzania hivyo kumtukana Rais nje ya mipaka ni kulituka Taifa, wamemstahi sana aisee.
Eleza tusi lipi alilotukana na utueleze kama kuna shitaka la kumtukana Raisi aliloshitakiwa nalo.

Nyie mtu akiwa Raisi kwenu mnamuona kama Mungu mtu!!

Acha kujipendekeza hata kama anakupa ulaji!!
 
Hata mimi, huwezi mtukana mkuu wa nchi tena nje ya mipaka ya nchi afu watu wakuchekeechekee tu, kwa mujibu wa katiba, Rais kama mkuu wa nchi ndiye nembo au alama ya Taifa nje ya mipaka ya Tanzania hivyo kumtukana Rais nje ya mipaka ni kulituka Taifa, wamemstahi sana aisee.
Kama ni kosa " kutukana" (japo mie silioni) adhabu yake ni kifo bila kupitia mahakamani?......
😂😂😂😂..wauaji wenzio wanamtuhumu kwa makosa ya KUTAKATISHA nguo zake kila anapo amua kufua.
 
Kama ni kosa " kutukana" (japo mie silioni) adhabu yake ni kifo bila kupitia mahakamani?......
..wauaji wenzio wanamtuhumu kwa makosa ya KUTAKATISHA nguo zake kila anapo amua kufua.
Kama yuko mahakamani basi tuache mahakama etende haki, kama jamaa alivyosema hapo juu.
 
Back
Top Bottom