Nimetoka kuhangaika na mishemishe za maisha, nimechoka na nimejaa mawazo.
Nafika nyumbani nategemea amani, badala yake nakutana na matusi na dharau zisizo na sababu.
Yeye mwenyewe kachukua simu, kapiga kwao eti anarudi na abaki huko huko!
Kuanzia kesho mimi ni single rasmi, na hili liwe fundisho kwake na kwa wengine wote: mwanaume naye ana mipaka ya kuvumilia.
Kipigo cha leo sio hasira tu, bali ni somo atakalolikumbuka maisha yake yote.
Wewe ni mwanaume DHAIFU na unatuaibisha wanaume wenzako
Mwanaume wa kweli mwanamke hawezi kukusumbua kizembe
Kulingana na MFUMO DUME tulionao Afrika mwanaume kwa asilimia 90+ ndio KISABABISHI cha matatizo kwenye mahusiano/ndoa nyingi
(Ingawaje pia wapo wanawake wasumbufu)
Hakuna mwanamke bila SABABU eti ataanza tu kukutukana na kuindoa amani ndani ya nyumba ukirudi nyumbani........ usiangaike na ulipo angukia rekebisha ulipo jikwalia
Wanaume wengi wa mfumo dume they don’t care about woman’s feelings or whatever as long as wana provide matumizi
Mkeo ni life partner wako na sio some kind of house girl wa kukuzalia kulea kupika kufua nk nk......
Jali hisia zake, msirikishe mipango yenu, mpe muda wako nk nk
Hakikisha anajiona ni sehemu ya maisha yenu na sio mkeo wa kukupa uroda unapo jisikia na kulea watoto wako
Mara nyingi ukihisi labda mkeo anakukarahisha ujue hiyo ni dalili kwamba kuna kitu kwa upande wako hakiko sawa...... labda huyo mwanamke awe mkorofi by nature
Na kikubwa zaidi tutafute hela..... zinasaidia sana kuwatuliza hawa viumbe