Wakazi wa Mikumi katika mkoa wa Morogoro wametishiwa kukamatwa wasipochangia Tsh.5000/= kwa ajili ya ujenzi wa madarasa

BVR 2015

JF-Expert Member
Jul 29, 2015
229
413
Wakazi wa mji mdogo wa Mikumi katika mkoa wa Morogoro,wametishwa na uongozi wa Serikali ya mji huo kuwa watakamatwa pale watakapobainika kuwa hawajachangia kiasi cha Tsh. 5,000/= kwa ajili ya ujenzi wa madarasa.

Uongozi wa mji kupitia gari la matangazo walikuwa wanawatangazia wananchi popote wanapotembea waakikishe wawe wamebeba risiti walizolipia ili wasikamatwe na jeshi la akiba.

Katika kikao walichoketi viongozi, wakiwepo madiwani na mbunge wa jimbo la mikumi ndugu Londa,wananchi walihoji huo uhalali wa kutoa michango wakati kipindi cha kampeni walinadi sera kuwa elimu itakuwa ni bure, pia wananchi waliwauliza hao madiwani na mbunge je wao tayari wameshachangia huo ujenzi? na wamechangia kiasi gani? Jibu alilotoa mbunge ni kwamba hataki maswali ya kelele kelele.
 
Hili si jambo jema!

Tulisema yale makusanyo ya 2t ni uongo wa mchana kweupe, kama wangekuwa wamekusanya hela hiyo wangetoa wakajenge madarasa. Na wale watendaji wa mitaa hawathubutu kuitisha mikutano ya wananchi maana wananchi hawa kuwachagua, ndio maana wanataka michango kwa shuruti. Kwa jinsi TRA walivyopanick baada ya ile taarifa, utajua fika kisemwacho sio. Mficha maradhi kifo humuumbua.
 
Tulisema yale makusanyo ya 2t ni uongo wa mchana kweupe, kama wangekuwa wamekusanya hela hiyo wangetoa wakajenge madarasa. Na wale watendaji wa mitaa hawathubutu kuitisha mikutano ya wananchi maana wananchi hawa kuwachagua, ndio maana wanataka michango kwa shuruti. Kwa jinsi TRA walivyopanick baada ya ile taarifa, utajua fika kisemwacho sio. Mficha maradhi kifo humuumbua.
Yake ni maigizo sasa hivi mtalii analipa entrance fee za kwenda mbugani kupitia TRA zamani ilikua TANAPA, jamaa kaweka vyanzo vyote vya mapato kuwa centralized kwa hiyo ni kuhadaa wananchii
 
Wakazi wa mji mdogo wa mikumi katika mkoa wa morogoro,wametishwa na uongozi wa serikali ya mji huo ,kuwa watakamatwa pale watakapobainika kuwa hawajachangia kiasi cha Tsh. 5000/= kwa ajili ya ujenzi wa madarasa. Uongozi wa mji kupitia gari la matangazo walikua wanawatangazia wananchi popote wanapotembea waakikishe wawe wamebeba listi walizolipia iliwasikamatwe na jeshi la akiba.
Katika kikao walichoketi viongozi,wakiwepo madiwani na mbunge wa jimbo la mikumi ndugu londa,wananchi walihoji huo uhalali wa kutoa michango wakati kipindi cha kampeni walinadi sera kuwa elimu itakuwa ni bure ,pia wananchi waliwauliza hao madiwani na mbunge je wao tayari wamesha changia huo ujenzi ? na wamechangia kiasi gani? Jibu alilotoa mbunge ni kwamba hataki maswali ya kelele kelele
Jeshi la akiba ndio jeshi gani !?
Atajichanganya tuu huyo jeshi la akiba halafu kipigo atapata kutoka kwa raia mwenye hasira kali ndio tutaelewana
 
Kila unywele utaguswa! Tuliwaambia mataga wakazidi kutuimbia kuwa tutaisoma namba.

Hizi ndio namba zenyewe ambazo tunazisoma pamoja
 
Back
Top Bottom