fishseller
Member
- Jun 13, 2012
- 30
- 19
Kwa kipindi kirefu sasa, wakazi wa Mbweni Mpiji iliyoko manispaa ya Kinondoni tumekuwa na matatizo mbalimbali ambayo serikali ya wilaya na mkoa wameshindwa kushirikiana na wananchi ili kusaidia kutatua matatizo hayo.
Mojawapo ya matatizo matatu tuliyonayo yaliyodumu kwa kipindi kirefu ni magari makubwa yanayotumika kusomba mchanga kutoka mto Mpiji na kupita kwa kasi kwenye makazi ya watu na kusababisha ajali.
Pia magari hayo yamepelekea kwa mmonyoko mkubwa wa ardhi na uharibifu wa miundombinu kwenye maeneo mengi ya Mbweni Mpiji. Miundombinu hiyo inajengwa kwa kutumia pesa za walipa kodi wan chi hii.
Baada ya tangazo la kuzuia magari hayo kusomba mchanga kutolewa na serikali mapema mwaka jana, magari ya polisi yalianza kufanya doria usiku na mchana ili kuzuia magari hayo yasiendelea kusomba mchanga huyo.
Hata hivyo, wakazi wa Mpiji tunasikitika kuwa polisi hao wametumia mwanya huo kuomba rushwa kutoka kwa madreva na wamaili wa malori na kuwaruhusu kuendelea na shughuli za uharibifu wa mazingira.
Baadhi ya madreva wamesikika wakitamba kuwa hakuna mtu wa kuwafanya chochote kwakuwa malori mengi yanamilikiwa na watu wenye nafasi kubwa serikalini na hakuna mtu yoyote anayeweza kuwagusa.
Tatizo la pili ni magendo kutoka Zanzibar kupitia bandari bubu ya Mbweni Maputo.
Kambi ya jeshi iliweka kizuizi ili magendo isipitie lakini wanaofanya biashara hiyo walibadilisha njia na kutumia njia nyingine ambayo polisi wanaofanya doria wamekuwa wakiwasubiri, kupokea rushwa na kuyaruhusu magari hayo kuendelea na safari.
Baadhi ya maafisa kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania wamekuwa wakishirikiana na askari polisi kupokea rushwa kutoka kwa wafanyabiashara hao.
Jambo lingine linalowasikitisha wakazi wa Maputo ni kwamba bandari inayotumika kupitisha magendo ipo mita chache kutoka chuo cha Usalama wa Taifa ambako wanafunzi na wakufunzi wanaiona biashara haramu ikiendelea bila wao kufanya chochote.
Tunasikitika kuona kuwa katika zama hizi za rais Magufuli ambaye alitoa ahadi kwa wapiga kura kwamba mambo haya hayawezi kuendelea kutokea nchi lakini yanaendelea kufanyika wakati watu wenye mamlaka ya kuzuia uharifu huu wakishirikiana na waarifu.
Mheshimiwa Makonda alipata sifa kubwa wakati akiwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni kutokana na utendaji wake mzuri lakini matatizo haya aliyafumbia macho mbali na ukweli kwamba alikuwa na taarifa.
Tatu, Mbweni Mpiji ni eneo la mji mpya ambapo viwanja vyote waligawiwa kwa wananchi baada ya kupimwa na serikali. Hata hivyo, maeneo mengi bado hayajaunganishwa na maji ya Dawasco. Baadhi ya watu waliounganishiwa maji walilazimika kuchanga mpaka milioni 10 ili Dawasco iweze kuwapelekea maji kwenye maeneo yao.
Eneo hili lina kaya za kutosha kwa Dawasco kuwekeza fedha kwa kuunganisha maji bila kuwachangisha wananchi kwani kuna uhakika wa wateja. Ni aibu kwa shirika ambalo linatakiwa kujiendesha kibiashara kuwachangisha watu ili kuwapatia huduma ya msingi kama maji.
Wengi wetu tuna matumaini makubwa na uongozi mpya wa mkoa wa Dar es Salaam na kasi ya Mheshimiwa Makonda lakini wasiwasi wetu ni kwamba kama alishindwa kutatua matatizo haya akiwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, ataweza kufanya nini kipya kwenye nafasi yake ya sasa?
Mojawapo ya matatizo matatu tuliyonayo yaliyodumu kwa kipindi kirefu ni magari makubwa yanayotumika kusomba mchanga kutoka mto Mpiji na kupita kwa kasi kwenye makazi ya watu na kusababisha ajali.
Pia magari hayo yamepelekea kwa mmonyoko mkubwa wa ardhi na uharibifu wa miundombinu kwenye maeneo mengi ya Mbweni Mpiji. Miundombinu hiyo inajengwa kwa kutumia pesa za walipa kodi wan chi hii.
Baada ya tangazo la kuzuia magari hayo kusomba mchanga kutolewa na serikali mapema mwaka jana, magari ya polisi yalianza kufanya doria usiku na mchana ili kuzuia magari hayo yasiendelea kusomba mchanga huyo.
Hata hivyo, wakazi wa Mpiji tunasikitika kuwa polisi hao wametumia mwanya huo kuomba rushwa kutoka kwa madreva na wamaili wa malori na kuwaruhusu kuendelea na shughuli za uharibifu wa mazingira.
Baadhi ya madreva wamesikika wakitamba kuwa hakuna mtu wa kuwafanya chochote kwakuwa malori mengi yanamilikiwa na watu wenye nafasi kubwa serikalini na hakuna mtu yoyote anayeweza kuwagusa.
Tatizo la pili ni magendo kutoka Zanzibar kupitia bandari bubu ya Mbweni Maputo.
Kambi ya jeshi iliweka kizuizi ili magendo isipitie lakini wanaofanya biashara hiyo walibadilisha njia na kutumia njia nyingine ambayo polisi wanaofanya doria wamekuwa wakiwasubiri, kupokea rushwa na kuyaruhusu magari hayo kuendelea na safari.
Baadhi ya maafisa kutoka Mamlaka ya Mapato Tanzania wamekuwa wakishirikiana na askari polisi kupokea rushwa kutoka kwa wafanyabiashara hao.
Jambo lingine linalowasikitisha wakazi wa Maputo ni kwamba bandari inayotumika kupitisha magendo ipo mita chache kutoka chuo cha Usalama wa Taifa ambako wanafunzi na wakufunzi wanaiona biashara haramu ikiendelea bila wao kufanya chochote.
Tunasikitika kuona kuwa katika zama hizi za rais Magufuli ambaye alitoa ahadi kwa wapiga kura kwamba mambo haya hayawezi kuendelea kutokea nchi lakini yanaendelea kufanyika wakati watu wenye mamlaka ya kuzuia uharifu huu wakishirikiana na waarifu.
Mheshimiwa Makonda alipata sifa kubwa wakati akiwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni kutokana na utendaji wake mzuri lakini matatizo haya aliyafumbia macho mbali na ukweli kwamba alikuwa na taarifa.
Tatu, Mbweni Mpiji ni eneo la mji mpya ambapo viwanja vyote waligawiwa kwa wananchi baada ya kupimwa na serikali. Hata hivyo, maeneo mengi bado hayajaunganishwa na maji ya Dawasco. Baadhi ya watu waliounganishiwa maji walilazimika kuchanga mpaka milioni 10 ili Dawasco iweze kuwapelekea maji kwenye maeneo yao.
Eneo hili lina kaya za kutosha kwa Dawasco kuwekeza fedha kwa kuunganisha maji bila kuwachangisha wananchi kwani kuna uhakika wa wateja. Ni aibu kwa shirika ambalo linatakiwa kujiendesha kibiashara kuwachangisha watu ili kuwapatia huduma ya msingi kama maji.
Wengi wetu tuna matumaini makubwa na uongozi mpya wa mkoa wa Dar es Salaam na kasi ya Mheshimiwa Makonda lakini wasiwasi wetu ni kwamba kama alishindwa kutatua matatizo haya akiwa mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, ataweza kufanya nini kipya kwenye nafasi yake ya sasa?