Keynez
JF-Expert Member
- Feb 12, 2007
- 3,635
- 6,529
Hii bank kwa kweli ina huduma mbovu sana. Juzi juzi nimejaribu kufungua account pale, kwanza wana fomu nyingi na complications zisizoisha. Siku 3 nazungushwa tu, nikaenda NMB ndani ya nusu saa nimemaliza.
Na ukishafungua account na hawa CRDB bado kuna matatizo mengi sana unakumbana nayo na account yako na huwa wanakuwa hawana msaada sana. Nasema hayo kwa sababu tayari nina account nyingine pale na ni kama nimeikacha. Hata ukiwa pale tu utaona idadi kubwa ya wateja wao wanaokuja na kuondoka bila matatizo yao kutatuliwa.
Naona hii benki inaenda au inastahili kugawanywa kama NBC ya wakati ule iliyozaa NMB. Tunaambiwa tupende vya kwetu ila inaonyesha hadi aje mzungu ndiyo huwa tunakaa sawa na kutoa huduma zinazoeleweka.
Najua hili linaweza lisitokee kwenye utawala wa Magufuli kwa sababu sera na mitazamo yake ni tofauti sana na Mkapa ila hii benki inabidi imulikwe.
Na samahani kama kuna nitakayemkwaza ila kuna element ka ukabila pia kwenye ile benki. Naona kama wafanyakazi wengi katika matawi niliyowahi kwenda ni watu wa kutoka sehemu moja!! Sijui kama hilo litakauwa linachangia matatizo waliyonayo ila niliondoka nikijiuliza maswali mengi ambayo sijapata majibu. Kwanza inawezekana wanachukua fomu za watu ambao mwisho wa siku wanaamua kutoendelea na application au hata kufanya makusudi zangu wanaweza wakawa wanakatisha tamaa watu wenye account halafu wanatumia hizo account au information za watu kuchukulia mikopo bila wateja wenyewe kujua? Je hili linawezekana? Nimefikia kujiuliza maswali kama hayo kwa sababu ufanisi wao ni wa mashaka sana.
Na ukishafungua account na hawa CRDB bado kuna matatizo mengi sana unakumbana nayo na account yako na huwa wanakuwa hawana msaada sana. Nasema hayo kwa sababu tayari nina account nyingine pale na ni kama nimeikacha. Hata ukiwa pale tu utaona idadi kubwa ya wateja wao wanaokuja na kuondoka bila matatizo yao kutatuliwa.
Naona hii benki inaenda au inastahili kugawanywa kama NBC ya wakati ule iliyozaa NMB. Tunaambiwa tupende vya kwetu ila inaonyesha hadi aje mzungu ndiyo huwa tunakaa sawa na kutoa huduma zinazoeleweka.
Najua hili linaweza lisitokee kwenye utawala wa Magufuli kwa sababu sera na mitazamo yake ni tofauti sana na Mkapa ila hii benki inabidi imulikwe.
Na samahani kama kuna nitakayemkwaza ila kuna element ka ukabila pia kwenye ile benki. Naona kama wafanyakazi wengi katika matawi niliyowahi kwenda ni watu wa kutoka sehemu moja!! Sijui kama hilo litakauwa linachangia matatizo waliyonayo ila niliondoka nikijiuliza maswali mengi ambayo sijapata majibu. Kwanza inawezekana wanachukua fomu za watu ambao mwisho wa siku wanaamua kutoendelea na application au hata kufanya makusudi zangu wanaweza wakawa wanakatisha tamaa watu wenye account halafu wanatumia hizo account au information za watu kuchukulia mikopo bila wateja wenyewe kujua? Je hili linawezekana? Nimefikia kujiuliza maswali kama hayo kwa sababu ufanisi wao ni wa mashaka sana.


