Wakati Nasoma Stashahada Yangu Ya Kwanza

Ambiele Kiviele

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2014
Posts
15,271
Reaction score
29,937
Wakati nasoma Stashahada yangu ya kwanza, tulitumia diski tepetevu, kicharazio, kirudufu, kinukuzi na kiteuzi.

Ilikuwa nadra sana kukuta mwanafunzi anatumia nywila kwenye kipakatalishi. Hata vitu kama mdaki, diski mweko, mtaliga, kadi sakima na kadiwia/mkamimo havikuwepo kabisa.

Ila kwa sasa mambo yamebadilika. Wanafunzi wanakula vibanzi na sharubati, wanapata mishiko haraka kutoka kiotomotela...wanatumia kadihela, Aaah mambo Saaaafi!

Shughuli ni pale unapogundua hujui kingereza wala kiswahili

[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Harafu tunajitapa tunakijua kiswahili..,umekopi wapi mkuu?,nilishaiona hii mahali lakini nimepasahau.
 
Hapo kwenye Stashahada ya kwanza ndo sijaelewa kabisa.
kwani Stashahada ya pili huwa ni ipi mkuu?
 
Ngoja nijaribu baadhi ya maneno
kicharazio - keybord
nywila - password
kiteuzi - pointer
kipakatalishi - laptop

kWa kweli kiswahil ni kigumu
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…