Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 15,997
Ndugu zangu,
Jambo linalompa JPM nguvu ni mbinu yake ya kujiambatanisha na matatizo ya wananchi. Na wananchi wakimuangalia wanaamini bila shaka huyu ni kiongozi wetu, wanaamini wapo naye kwenye mvua na jua, njaa na shibe.
JPM amejitahidi kuwa karibu na wananchi akifuatilia kila tukio siku kwa siku. Tabia hii imempa fursa ya kutatua changamoto inayojitokeza kwa wakati bila kuchelewa. Hii ndio imempa nguvu ya umma. Nguvu ya umma ni muhimu katika utawala wowote. JPM hachoki kudadisi taarifa zozote zinazohusu nchi iwe kiutamaduni, kijamii, kiuchumi nk. na mara kwa mara amekuwa akichomekea pale anapopata fursa ya kuhutubia.
Mara nyingi akihutubia amewaasa wananchi ya kwamba hakuna mtu wa nje atakayetusaidia matatizo yetu, hivyo ni lazima tufanye kazi. Hapa amekuwa tofauti, huku wapinzani wake wakihubiri kukumbatia wazungu na mtindo wao wa maisha, JPM amejikita katika siasa za ukweli zenye kumpa ujasiri mwananchi wa kawaida.
Miaka mitano hadi kumi iliyopita Chadema ilijikita kwenye nguvu ya umma na lolote lililotokea iwe Bungeni au nje ya Bunge viongozi Chadema walisikika wakisema ''tunashtaki kwenye mahakama ya umma''
Ajizi nyumba ya njaa, katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2015 walidanganywa wakaajiri mzungu ili awasaidie kwenye propaganda huku viongozi wakieneza propaganda kwamba wamefungua kesi ICC ili Kikwete ashitakiwe. Wananchi waliona na wakaanza kuwapuuza.
Baada ya hapo walijikita katika kueneza habari hasi dhidi ya nchi kwa kupitia media za nje mkakati ambao umeshafeli. Wananchi hawakufurahi na mkakati huu kwani matokeo yake yangeathiri maisha ya wananchi na si wanasiasa.
Kwa wenye kumbukumbu, Mbowe aliwahi kufika mahala kila linalotokea anampiga JK mkwara kuwa ''nchi haitatawalika''. Maneno haya yalikuwa ni dalili ya nguvu ya wananchi ambao kwa sasa hawapo nao.
Nimalize tu kwa kusema kinachombeba JPM ni kujiambatanisha na wananchi huku wapinzani wanakosa nguvu kwa sababu ya kukumbatia wazungu.
Wakongomani husema ''nguvu ya mamba ku mayi''
Jambo linalompa JPM nguvu ni mbinu yake ya kujiambatanisha na matatizo ya wananchi. Na wananchi wakimuangalia wanaamini bila shaka huyu ni kiongozi wetu, wanaamini wapo naye kwenye mvua na jua, njaa na shibe.
JPM amejitahidi kuwa karibu na wananchi akifuatilia kila tukio siku kwa siku. Tabia hii imempa fursa ya kutatua changamoto inayojitokeza kwa wakati bila kuchelewa. Hii ndio imempa nguvu ya umma. Nguvu ya umma ni muhimu katika utawala wowote. JPM hachoki kudadisi taarifa zozote zinazohusu nchi iwe kiutamaduni, kijamii, kiuchumi nk. na mara kwa mara amekuwa akichomekea pale anapopata fursa ya kuhutubia.
Mara nyingi akihutubia amewaasa wananchi ya kwamba hakuna mtu wa nje atakayetusaidia matatizo yetu, hivyo ni lazima tufanye kazi. Hapa amekuwa tofauti, huku wapinzani wake wakihubiri kukumbatia wazungu na mtindo wao wa maisha, JPM amejikita katika siasa za ukweli zenye kumpa ujasiri mwananchi wa kawaida.
Miaka mitano hadi kumi iliyopita Chadema ilijikita kwenye nguvu ya umma na lolote lililotokea iwe Bungeni au nje ya Bunge viongozi Chadema walisikika wakisema ''tunashtaki kwenye mahakama ya umma''
Ajizi nyumba ya njaa, katika kipindi cha kuelekea uchaguzi mkuu mwaka 2015 walidanganywa wakaajiri mzungu ili awasaidie kwenye propaganda huku viongozi wakieneza propaganda kwamba wamefungua kesi ICC ili Kikwete ashitakiwe. Wananchi waliona na wakaanza kuwapuuza.
Baada ya hapo walijikita katika kueneza habari hasi dhidi ya nchi kwa kupitia media za nje mkakati ambao umeshafeli. Wananchi hawakufurahi na mkakati huu kwani matokeo yake yangeathiri maisha ya wananchi na si wanasiasa.
Kwa wenye kumbukumbu, Mbowe aliwahi kufika mahala kila linalotokea anampiga JK mkwara kuwa ''nchi haitatawalika''. Maneno haya yalikuwa ni dalili ya nguvu ya wananchi ambao kwa sasa hawapo nao.
Nimalize tu kwa kusema kinachombeba JPM ni kujiambatanisha na wananchi huku wapinzani wanakosa nguvu kwa sababu ya kukumbatia wazungu.
Wakongomani husema ''nguvu ya mamba ku mayi''