Hawa watu wako serious sana. Jana alikuja mjumbe nyumbani kwangu akataka nimpe taarifa zangu vikiwemo vitambulisho vyangu (Kura au NIDA)
Nilimuuliza, kwanini unataka taarifa zangu? Akajibu “Ni kwa ajili ya uboreshaji wa taarifa zako kwenye daftari la wapiga kura” Nikamwambia zoezi hilo linafanyika kituoni, nitaenda huko kurekebisha taarifa zangu.
Akaondoka, lakini alikuwa na taarifa za wakazi wengine pamoja na vitambulisho kadhaa.
Elimu zaidi inahitajika, viongozi wa vyama vya upinzani waamke katika usingizi mzito. Wananchi wengi wataingia kwenye huu mtego wa kuchukuliwa taarifa zao.
Binafsi nikienda kurekebisha taarifa zangu kituoni nikikutana na huo ujinga wa wakala wa CCM kuorodhesha majina nitaondoka na kuachana na zoezi zima.