Precious Diamond
JF-Expert Member
- Jun 9, 2023
- 710
- 1,610
Wakuu,
Msemaji wa Mbezi Beach leo nimeenda kuboresha taarifa zangu kwenye daftari kudumu la wapiga kura katika Ofisi ya Serikali ya Mtaa Mbezi Beach B. Wakati niko nasubiri kuandikishwa ilikuwa zamu ya dada fulani kuandikishwa. Sasa wakati anaandikishwa huyo kaka kwenye picha hapo pembeni alikuwa nje, akamwambia huyo dada muandike na huyo kwenye daftari.
Huyo dada akauliza hilo daftari ni la nini, mwandikishaji akasema ni la wakala, akauliza wakala wa chama gani, akaambiwa CCM, akauliza kwanini wanaandikisha mwandikishaji wa Tume akasema sijui, mimi kaniambia wameambiwa waandike. Yule dada akamuuliza tena kwanini hujauliza kujua kama ni utaratibu? Dada hakuwa na majibu, akaambiwa aulize sababu wanacheza na taarifa za watu.
Wakati anamalizia kujaza taarifa zake huyo wakala wa CCM akarudi kwenye kiti chake, alipoulizwa akasema kuna awamu ya pili ambayo watakuja kuhakikisha majina. Dada akamuuliza unahakikisha majina kama nani wakati wewe siyo mfanyakazi wa Tume? Na kwanini uandikishe majina wakati kazi hii inafanywa na tume? Yule wakala akasema hapo sina majibu sisi ndiyo tulivyoambiwa kwenye chama, kama unataka maelezo zaidi inabidi ukaulize huko!
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Hapo ikafanya nijiulize, kwanini huyu wakala anaandika haya majina? Wanaenda kuyafanyia nini? kwanini yaandikwe pembeni kwenye kidaftari. Kidaftari wanachoandikia ni hiko hapo nimekizungushia duara, kama mamlaka itataka jina la wakala naweza kuwapatia.
Baada ya yeye kusema ni wakala wa CCM ndio nikagundua wakala wa vyama vingine hawapo. Na ndio maana hii figisu inaendelea, sidhani kama kungekuwa na mawakala wa vyama vingine hili lingeendelea.
Nataka Tume ituambie huu ndio utaratibu kwamba Wakala anatakiwa kuchukua majina ya wanaojiandikisha na jinsia zao? Je, taarifa hizo zinachukuliwa kwa matumizi gani kama wafanyakazi watume wanarekodi majina hayo? Na mawakala wanatoa ushirikiano kutoa majina hayo, maana kaka huyo alikuwa nje wakati dada anaandikisha akamwambia mwandikishaji aandike hilo jina mwandikishaji akasema utakuja kulichukua huku (kwenye fomu), lakini anafanya hivyo bila kujua majina hayo yanaenda wapi!
Pia soma ~ Mratibu wa Uandikishaji Dar: Wakala wa Chama kazi yake ni kutazama sio kunakili majina ya wanaojiandikisha kwenye Daftari la Wapiga Kura
Wadau wengine waliyokutana na hali kama hii;
===
Msemaji wa Mbezi Beach leo nimeenda kuboresha taarifa zangu kwenye daftari kudumu la wapiga kura katika Ofisi ya Serikali ya Mtaa Mbezi Beach B. Wakati niko nasubiri kuandikishwa ilikuwa zamu ya dada fulani kuandikishwa. Sasa wakati anaandikishwa huyo kaka kwenye picha hapo pembeni alikuwa nje, akamwambia huyo dada muandike na huyo kwenye daftari.
Huyo dada akauliza hilo daftari ni la nini, mwandikishaji akasema ni la wakala, akauliza wakala wa chama gani, akaambiwa CCM, akauliza kwanini wanaandikisha mwandikishaji wa Tume akasema sijui, mimi kaniambia wameambiwa waandike. Yule dada akamuuliza tena kwanini hujauliza kujua kama ni utaratibu? Dada hakuwa na majibu, akaambiwa aulize sababu wanacheza na taarifa za watu.
Wakati anamalizia kujaza taarifa zake huyo wakala wa CCM akarudi kwenye kiti chake, alipoulizwa akasema kuna awamu ya pili ambayo watakuja kuhakikisha majina. Dada akamuuliza unahakikisha majina kama nani wakati wewe siyo mfanyakazi wa Tume? Na kwanini uandikishe majina wakati kazi hii inafanywa na tume? Yule wakala akasema hapo sina majibu sisi ndiyo tulivyoambiwa kwenye chama, kama unataka maelezo zaidi inabidi ukaulize huko!
Kupata matukio na taarifa zote kwa kila mkoa kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025 ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
Hapo ikafanya nijiulize, kwanini huyu wakala anaandika haya majina? Wanaenda kuyafanyia nini? kwanini yaandikwe pembeni kwenye kidaftari. Kidaftari wanachoandikia ni hiko hapo nimekizungushia duara, kama mamlaka itataka jina la wakala naweza kuwapatia.
Baada ya yeye kusema ni wakala wa CCM ndio nikagundua wakala wa vyama vingine hawapo. Na ndio maana hii figisu inaendelea, sidhani kama kungekuwa na mawakala wa vyama vingine hili lingeendelea.
Nataka Tume ituambie huu ndio utaratibu kwamba Wakala anatakiwa kuchukua majina ya wanaojiandikisha na jinsia zao? Je, taarifa hizo zinachukuliwa kwa matumizi gani kama wafanyakazi watume wanarekodi majina hayo? Na mawakala wanatoa ushirikiano kutoa majina hayo, maana kaka huyo alikuwa nje wakati dada anaandikisha akamwambia mwandikishaji aandike hilo jina mwandikishaji akasema utakuja kulichukua huku (kwenye fomu), lakini anafanya hivyo bila kujua majina hayo yanaenda wapi!
==================
Wadau wengine waliyokutana na hali kama hii;
===
View attachment 3277637
Huku (Dar-Kinondoni) hilo daftari alikuwa anaandika mwandikishaji wa tume huyo dada mwenye uniform ya Tume! Basi atakuwa ni CCM
halafu wazee wa Tone Tone wanategemea kutoboa na hiyo kampeni yao ya kufikirika!![]()
