Meridah Tough
Senior Member
- Nov 27, 2017
- 136
- 365
Dah!
Hapa duniani kuna mengi sana.
Kwa heshima naomba nitangulize salamu kwa jukwaa hili pendwa. Kwa kweli mkasa ambao umenipata, nitapenda kuuongelea ili iwe funzo kwa wadada wengine wadogo ambao wanapata changamoto hizi ndogondogo.
Hivi karibuni baada ya kuachwa na mwenzangu ambaye tulidumu muda sana katika mapenzi, tukipita changamoto mbalimbali hususan za kiuchumi, nafikiri mwenzangu alipata mtu mwingine. Nami kwa kuwa nilishachoka kuwa mpiganaji wa kulinda penzi letu, nikaona sawa tu, aende nipate pumziko kwingine, pengine hatukuandikiwa. Baada ya kama miezi 3, tukaanza mahusiano na kijana mwingine mtu mzima kidogo.
Kwa kweli, alinijali sana na kunipenda sana. Lakini katika maongezi ni kama tulikuwa watu wawili tofauti. Wakati mimi nikimwambia mategemeo yangu katika mahusiano yetu ni kutulia na kutokuwa na dramas, mwenzangu alikuwa anaongea kana kwamba tuna urafiki wa sex tu na and nothing. Sikuwa na pupa kujua nini alimaanisha.
Kwa bahati mbaya mwenzangu alipata changamoto fulani mambo ya msiba, hivyo akalazimika kubeba majukumu katika familia yao kipindi hiko cha Covid 19. Alinishirikisha nami bila hiyana nikaona nimsaidie jambo ambalo lilimshangaza sana kwani hakutegemea kama ningeweza kujitoa kiasi kile tena katika kipindi cha Covid 19.
Baada ya hapo, upendo uliongezeka ikawa too much sasa kwa uapande wake jambo ambalo mimi nikaanza kupata wasiwasi. Wasiwasi wangu ukazidi pale ambapo jamaa akaanza tabia za kuonyesha dalili zote za kutaka niwe nampatia pesa. Ingawa anafanya masihara lakini ni yale masihara ya kweli. Mara nina ndoto za kufanya hivi nitafutie pesa, mara nataka kile in the future kitatusaidia but kitakaa kwangu and so many dramas.
Kwa kweli maisha ya namna hiyo, nikaanza kupoteza interest naye. Sababu ninaamini kusaidiana kupo na ni jambo la kawaida katika maisha either ya mapenzi ama la, lakini mtu anapomchukulia mwenzake aliyemsaidia kama kitega uchumi, kwa kweli, kwanza inasikitisha lakini pili itakufanya upoteze trust kwa mtu. Hii ni kwa ke na me.
Mpaka sasa nina mwezi sina interest kabisa ya kumtafuta mwenzangu. Sina interest naye kabisa naona hata yeye amegundua hivyo na ndio maana hanitafuti.
Mwenye kuona funzo na aone.
Hapa duniani kuna mengi sana.
Kwa heshima naomba nitangulize salamu kwa jukwaa hili pendwa. Kwa kweli mkasa ambao umenipata, nitapenda kuuongelea ili iwe funzo kwa wadada wengine wadogo ambao wanapata changamoto hizi ndogondogo.
Hivi karibuni baada ya kuachwa na mwenzangu ambaye tulidumu muda sana katika mapenzi, tukipita changamoto mbalimbali hususan za kiuchumi, nafikiri mwenzangu alipata mtu mwingine. Nami kwa kuwa nilishachoka kuwa mpiganaji wa kulinda penzi letu, nikaona sawa tu, aende nipate pumziko kwingine, pengine hatukuandikiwa. Baada ya kama miezi 3, tukaanza mahusiano na kijana mwingine mtu mzima kidogo.
Kwa kweli, alinijali sana na kunipenda sana. Lakini katika maongezi ni kama tulikuwa watu wawili tofauti. Wakati mimi nikimwambia mategemeo yangu katika mahusiano yetu ni kutulia na kutokuwa na dramas, mwenzangu alikuwa anaongea kana kwamba tuna urafiki wa sex tu na and nothing. Sikuwa na pupa kujua nini alimaanisha.
Kwa bahati mbaya mwenzangu alipata changamoto fulani mambo ya msiba, hivyo akalazimika kubeba majukumu katika familia yao kipindi hiko cha Covid 19. Alinishirikisha nami bila hiyana nikaona nimsaidie jambo ambalo lilimshangaza sana kwani hakutegemea kama ningeweza kujitoa kiasi kile tena katika kipindi cha Covid 19.
Baada ya hapo, upendo uliongezeka ikawa too much sasa kwa uapande wake jambo ambalo mimi nikaanza kupata wasiwasi. Wasiwasi wangu ukazidi pale ambapo jamaa akaanza tabia za kuonyesha dalili zote za kutaka niwe nampatia pesa. Ingawa anafanya masihara lakini ni yale masihara ya kweli. Mara nina ndoto za kufanya hivi nitafutie pesa, mara nataka kile in the future kitatusaidia but kitakaa kwangu and so many dramas.
Kwa kweli maisha ya namna hiyo, nikaanza kupoteza interest naye. Sababu ninaamini kusaidiana kupo na ni jambo la kawaida katika maisha either ya mapenzi ama la, lakini mtu anapomchukulia mwenzake aliyemsaidia kama kitega uchumi, kwa kweli, kwanza inasikitisha lakini pili itakufanya upoteze trust kwa mtu. Hii ni kwa ke na me.
Mpaka sasa nina mwezi sina interest kabisa ya kumtafuta mwenzangu. Sina interest naye kabisa naona hata yeye amegundua hivyo na ndio maana hanitafuti.
Mwenye kuona funzo na aone.
