Hapo ndipo wengi walipo. Wanawake wengi wanadhani hiyo sanaa ni kuviringisha tu hicho kiuno; No baby, Jifunze kitu kingine. Ujasiri wa kumwomba asije bila weye kumwambia. Pia weka mawazo kwenye huo mtanange. Muwazie huyu aliepo sasa hivi sio yule wa miaka ileeee.
Mpende kweli kweli, mweleze unavyomfurahia sio kuwaza ya kale. Kama sijakufikisha, mbona huniambii unaenda kuwaeleza dada zako? Huu ni ujinga tu. Nieleze mime niliye nawe, ukiniambia vizuri si kesho nitajirekebisha na kufanya vizuri zaidi?
Tujitahidi kujitambua kuwa tunahitajiana sote. Mambo ya saloon ni baadaye. Pia wanaume nanyi, jitahidini. Nenda kwa mkeo kabla ya kulewa. Ati bila pombe hiyo kitu siwezi. Poor me!
Nilewe nimwendee mke wangu au hawara wa ukwelii? Mbona maajanga haya! Usipomtosheleza nakuambia hawa hawana simile. The first man to cut her way, anajichukulia kiulainiii. Weye unaenda kwa hawara, umelewe halafu kwa sababu ulichelewa bar, unataka cha haraka ukimbilie home wife asijue. Weye babu jinga tu. Unamwacha mwenzio akiwa very very hot. Anatafuta kipoozeo. Nyumbani huwezi tena, naye anabakia very hot, anatafuta kipoozeo. Hayo ni majanga.