Bujibuji Simba Nyamaume
JF-Expert Member
- Feb 4, 2009
- 74,834
- 155,781
Mamilioni ya watu duniani hutegemea samaki na mazao yatokanayo na samaki kwa chakula chao na uchumi wao.
Kuna zaidi ya jamii 30,000 za aina tofauti ya samaki huko baharini na kwenye maji ya mito, maziwa mabwawa nk wakicheza na kukimbizana kwa mawindo na kujilinda.
Kunanaina za samaki ambazo NI wazuri Sana na wenye kupendeza kama maua ya bustanini, utawakuta wakiuzwa madukani kwenye viota vya kioo na pia kwenye majumba ya matajiri na mahoteli ya kifahari.
Likini pia kwa upande wa pili Kuna samaki wa kuogopesha Sana, wenye sumu, wenye meno makali waliopo hodari na mahiri kwenye kuondoa uhai wa mwanadamu na kiumbe chochote wanachohisi chaweza kuhatarisha maisha yao.
Kuna samaki wenye kushambulia binadamu, wapo wawezao kuachilia sumu Kali wasipo shikwa au kuandaluwa kwa umakini kabla ya chakula.
Pia wapo samaki wenye kuzalisha umeme mkali sana wenye uwezo wa kuua watu wengi kwa mkupuo.
10. Puffer Fish (Bunju)
Puffer fish au Bunju kwa Kiswahili ni aina ya samaki MWENYE kujitunisha na kujivimbisha. Kuna zaidi aina 90 ya Bunju baharini.
Samaki Hawa wenye uwezo wa kujitunisha na kutengeza umbo la duara wanapokasirishwa, huoatikana kwenye maji ya bahari kwenye maeneo yenye joto duniani kote.
Wana ngozi ngumu yenye miiba, na wana meno makali na kabla hajajitunisha anakuwa na umbo Kama la gari.
Bunju mkubwa hufikia ukubwa wa sentimeta 90 au futi tatu lakini wengi wao huwa ni wadogo wadogo.
Bunju wana sumu kali sana iliyopo ndani ya miili yao ambayo inaweza ikakuua ndani ya muda mfupi ukimla, lakini samaki huyu Japan huliwa na anatajwa kwamba ni samaki mtamu Sana, huandaliwa na mtaalamu aliyepata mafunzo ya miaka mitatu. Na kwa Kijpani Bunju huitwa FUGU.
9.Red Lionfish