Huyu jamaa wakati alipokuwa rais wa chuo pale udsm miaka ile ya katikati mwa 2000, alikuwa smart sana kwenye kutetea maslahi ya wanachuo mfano boom lilipochelewa kutoka, aliongoza mwenyewe migomo na maandamano hadi haki ilipopatikana.
Naona tangu ameingia kwenye siasa, nguvu kubwa anaitumia kulipigania tumbo lake. Ni vyema wangerudisha ule mfumo wa kubadilishana vituo vya kazi na si kuwazuia kabisa watumishi kuhama. Madhara ya hii kitu ni kwa serikali maana hao watumishi kimwili watakuwa kwenye vituo vyao vya kazi ila kiakili watakuwa wanaziwazia familia zao tu na hivyo kudhorotesha utendaji wa kazi.