Waislamu watangaziwa mfungo wa siku tatu ili kujiepusha na COVID19

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,011
9,879
Katibu wa Baraza la Maulamaa, Sheikh Hassan Chizenga ametaka waumini wa dini ya Kiislamu nchini Tanzania kufunga kwa siku tatu kuanzia Machi 8 ili kumuomba Mungu aepushe janga la CoronaVirus.

Pamoja na Mfungo Baraza Kuu la Waislamu Tanzania limeona haja ya kurejesha dua za Kunuti katika swala zote tano hadi COVID-19 itakapotokomea.

Serikali ilisema Tanzania inachukua tahadhari dhidi ya COVID19 ambazo ni kujifukiza na kumtegemea Mungu.

1613447362782.png

Akizungumza na waandishi wa habari kwa niaba ya Mufti wa Tanzania, Katibu Mkuu wa Baraza la ulamaa na Msemaji wa Mufti wa Tanzania Sheikh Hassan Said Chizenga ametoa agizo hilo kwa misikiti yote nchini kurejesha tena dua ya kunuti katika swala zote tano pamoja na kuchukua tahadhari zote zinazotolewa na Wizara ya afya kwa ajili ya kujingika na maambukizi ya ugonjwa wa Corona

"Baada ya kuonekana kwamba baadhi ya mashambulizi tuliyoyapata mwaka jana kana kwamba yanataka yatokee tena basi kilichokuwa sahihi ni kuzungumza na Mungu nakutumia utaalamu wa kisayansi unaotakiwa na Mungu tumweke mbele tukifanya hivyo tutafanikiwa" amesema Sheikh Hassan

Aidha watanzania wameshauriwa kutokutetereshwa kiimani na mtu yeyeote kuhusiana na silaha waliyoitumia na kuwapatia ushindi mwaka jana ambayo ili leta utofauti kati ya Tanzania na nchi nyingine badala yake wazidi kumtegemea mwenyezi Mungu.

"Tusiyumbishwe kwa namna yeyote kuiacha silaha yetu iliyotupa ushindi mwaka jana kwa kushawishiwa kutumia silaha iliyothibitishwa kuwa aina uwezo wa kupambana na korona," amesema amesema Sheikh Hassan

Sheikh Hassan Said Chizenga ametoa maagizo na tamko la Baraza la ulamaa BAKWATA kwa watanzania hii leo kwa niaba ya Mufti wa Tanzania Sheikh Abubakar Zubeir Ally aliyeshindwa kuhudhuria katika mkutano huo kutokanana sababu za kibinadamu.

Chanzo: EATV
 
Kumbe Covid19 ipo? Au hawa nao wanaanza kutumiwa na mabeberu?

Hata hivyo baina kama pana maneno mawili umeyaruka mkuu kwenye taarifa yako. Yako hapo kwenye bold tafadhali:

"Serikali ilisema Tanzania inachukua tahadhari "kali kabisa" dhidi ya COVID19 ambazo ni kujifukiza na kumtegemea Mungu."

Hatua kama hizi zingetufaa sana zikitumika hata dhidi ya magonjwa yote, majambazi, pia vita vya uchumi na hasa kwenye yale mambo yetu ya ulinzi na usalama.

Kwa mwendelezo huu hatuhitaji tena mahospitali wala watumishi wa afya.
 
... Machi 8 mbona mbali sana! Zaidi ya wiki 3 ni mbali mno; all possible measures zilitakiwa ziwe zimechukuliwa long time ago; hali sio shwari mitaani kwetu huku. Hii sio harusi (inayohitaji maandalizi) bali ni disaster; measures zinatakiwa zichukuliwe papo kwa papo bila kusubiri.
 
Hivyo huu uzi umekosewa au mimi nimesoma vibaya! Ni kuanzia wiki3 zijazo!!! Tarehe 8? Kizengha, upo serious kweli!!!
 
Hakuna kitu kibaya kama ujinga!Imagine mnatangaza mfungo wa siku tatu wa kukusanyika pamoja kwa kile kinachoitwa ni maombi, wakati mikusanyiko ndiyo njia mbaya sana ya kueneza Corona!
 
Kufunga huku kusiendane na watu kushinda njaa (tunaambiwa immunity ni muhimu inayoendana na lishe)

By the way maisha ya majority ya watu kitaa ni mfungo tosha (yaani zile wants zote hawazipati) sio kwa kupenda, bali inabidi
 
Corona hakuna anataka kufunga nini tena? Kama kufunga wafunge wao bakwata sisi waislamu hatufungi.hatuwatambui masheikh wa bakwata
 
Huku kwetu **** msemo wanasemaga "Yasini ni dawa lakini na mbio uwe nazo"

Kufunga na kuomba ni jambo sahihi sana lakini kama huchukui tahadhari kitaalamu utakufa kwa corona na huko mbnguni utachomwa kama nguruwe, yani utatiwa jiti mdomoni litokee kwa nyuma afu utakua unazungushwa zungushwa
 
Katibu wa Baraza la Maulamaa, Sheikh Hassan Chizenga ametaka waumini wa dini ya Kiislamu nchini Tanzania kufunga kwa siku tatu kuanzia Machi 8 ili kumuomba Mungu aepushe janga la CoronaVirus.

Pamoja na Mfungo Baraza Kuu la Waislamu Tanzania limeona haja ya kurejesha dua za Kunuti katika swala zote tano hadi COVID19 itakapotokomea.

Serikali ilisema Tanzania inachukua tahadhari dhidi ya COVID19 ambazo ni kujifukiza na kumtegemea Mungu.

Baraza la Maulamaa na Bakwata ni vitu viwili tofauti.
Maulamaa ndio nini
Usifikiri wote tunajua hayo madude yenu
 
Back
Top Bottom