Waislam msiende liliondo- redio kheir

Kwa kweli swala la imani ni gumu sana kuliangalia katika mioyo ya watu...waweza kataza watu wakakukubalia machoni ili kukufurahisha lakini wakatenda watakavyo!
Sioni kama ni vema kuwakataza watu kwenda kujaribu tiba, maana sijasikia kama Babu amewashawishi watu kubadili dini au kuihusisha dawa na swala la kubadili watu itikadi na imani zao....! Waacheni waende jamani wanaumwa hao!
 

kati ya radio makini ni kheir na immaan redio. Wapo wazi juu ya dawa babu loliondo kuwa ni uvumi[DECI] usiache watu wapoteze fedha kwa kuuza mali zao ili waende kwa babu ? Watu wameuza mashamba kwenda kudanganywa na babu ? Tiba gani haina anayejitokeza hadharani kuwa amepona bäada ya miezi sita walau. Mtu anakunywa dawa muda huohuo anasema kapona huku bado hajapimwa ? Utapeli mkubwa huo. Babu anastahili akamatwe kwa kudanganya umma.
 
Kuna watu wanaongea tu bila kujua kwanini UISLAM unampinga Babu wa loliondo,kwanza napenda kuwaambia ndugu zetu ktk Adam waislam wanamkubali Yesu kama mtume/nabii,hakuuwawa na ndo maana yupo hai;Na mtume Mohammad s.a.w ni mtume na nabii wa mwisho so wanapomuona mtu anaamka na kusema yeye ni nabii kama Babu inakuwa ni kinyume cha mafundisho ya uislam thatz y wanazuia.Na Yahya ni mchawi mkubwa kama kakobe,lwakatare,mwalusako,nk
 

Well said Manyanza...!
Need we say more....?
 
sasa mbona hawawakatazi kula kitimotto ambayo inawasaidia kumezea ARVs........Hao ni Waslamu na sio Waislam
 

Shida iko wapi...? Maradhi ni na tiba ni mambo binafsi...
Kama una mtu ana ugua maradhi yanayotibiwa na babu au kama wewe mwenyewe una maradhi hayo nenda kwa babau ukapate kikombe na ninakuhakikishia utapona...!

Swali ni: Je.., ukitibiwa na kupona utampokea Yesu kama mwokozi wa maisha yako au ndio yatabaki yale ya Baniani mbaya.....?
 

Kama una UKIMWI., sukari., pumu au presha nenda kwa babu wewe utakuwa shahidi msikitini kuwa dawa ya babu inafanya kazi..!
 
Naafikiana na kutokwenda kwao ili sisi tuliowapenda Yesu tupate kupona kwa msaada wa Mungu, waendelee na ngono zao sisi tunaenda kwa Babu akatupe kikombe cha uzima.
 
Uko dunia ipi mwenzetu watu wamejitokeza kwenye magazeti tena viongozi katika ngazi mbalimbali za kijamii wote wakitoa shuhuda wamepona au ulitaka mtu atoke ndani ya ukoo wako ndio uamini,acheni watu waende wakaponywe kwa imani
 

Congratulations LordJustice.., ahsante kwa kutujuza..!
 
Ukitaka kujua mshauri wa kweli, umpate anae umwa hasa HIV au Kisukari ndo atakwambia uende Loliondo au la! Ila hawa wanaopiga kelele hawana shida...
 


Muulize Omary Mahita....
 

Hata ikiajathibitika kuwa ni uongo huyo Babu hana kosa maana hajawatangazia watu, bali wanjitangazia wenyewe na kumimika kama mvua, waache watu wajaribu tiba mbadala, wewe unasema tu kwa kuwa hujawahi ugua au uguliwa siku yakikufika utaenda mwenyewe bila kuomba ushauri.
 


Humuamini YESU utaaminije Miujiza??? EM tuambie muujiza gani aliowahi kuufanya mtume .s.a.w katika maisha yake duniani...manake ya yesu yapo kibao....tuanzie hapo mkuu
 
wengine mbona wanandoa na MAJINI, lakini hatusemi!:hug:dawa lazima tunywe, wasiotaka wasiende!
 
wanasema mbona hawajitokezi na kupimwa hospital?
Hata huko hospitali tunapoenda bado ugonjwa wa mtu huwa ni siri kati ya daktari na mgonjwa hivyo sioni mantiki ya kutaka watu wakapime na kuonesha hadharani kama wameponywa au vipi,kuna mambo mengine yanashangaza sana hapa duniani babu hajaita mtu yeyote kwenda kule na wanaenda kwa dhamira ya kupona.
Hao wanaosema kuwa wenzao wasiende ni wazima na kama wangekuwa wanaumwa basi ndio wangekuwa wa kwanza kwenda katika kutafuta suluhisho la matatizo yao,katika ugonjwa hakuna binadamu asiyehangaika kutafuta tiba hata kama atabadilisha madaktari tofauti tofauti ili mradi tu aweze kupona.
 
Mimi nimeenda na nimekunywa dawa na kupona! Nimepima inshaalah sina virusi tena! Watu wa Mungu nendeni mtapona,,,hakuna cha muislam wala mkristo wooote wamejaa mle. Hao wanaosema waislam wasiende....nadhani its too late maana hata mashekhe wamejaa kule kwa Babu!
 


Hakika sasa ndio naelewa kwanini Salman Rushdie alikuja na 'THE SATANIC VERSES' - 'AYA ZA SHETANI'.
 
sasa watu kwenda loliondo wao inawauma nini? kwani quran inakataza mitishamba?
shida sio mitishamba bali utajwa wa JINA LIPITAYO MAJINA YOTE yaan YESU. kwa maana hawakubali wala hawathubutu kukaa kimya maana wanajua watu wakishaenda huko watamtukuza na hapo ndipo panapogomba
 
Mimi sioni tatizo hapa cha msingi ni uamuzi wa mtu binafsi bana wewe unaumwa, wenzio au umati wa watu wanapata tiba na wanapona chagua umauti au udini
 

Similar Discussions

Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…