Wahenga tu: Katika awamu 5 za serikali ya JMT zilizopita ipi unaikubali zaidi kwa Utendaji uliotukuka?

Awamu ya Nne ya Dr. JK.
Ni katika awamu hii nilipanda madaraja mara mbili, mwanangu aliajiriwa, Mdogo wangu aliajiriwa, Ulikuwa ndo mwanzo wa kaka yangu kuwa tajiri kabla ya kuyumba ktk awamu ya Magu.
Pia vijana wengi mtaani kwetu waliajiriwa au kujiajiri na mzunguko wa pesa ukawa mzuri.
Kaka yako alikuwa tajiri halafu akayumba kipindi cha Magu?

Basi huyo hakuwa tajiri kwa maana ya tajir bali alikuwa " ananyonya" sehemu fulani
 
Enzi za mkoloni ndio naikubali zaidi maana nakumbuka maisha yalikuwa mazuri mno
Ingawa nilikuwa mdogo ila wacheni tu
Hizo awamu zote siwezi kusema nazikubali

Train tu zilikuwa kama oriental express
 
Namkumbuka Chaudry (RIP) ndo alianzisha uvaaji wa pajama mpaka leo ndo uniform ya wasichana
Wakati ule tuliona kama anatupotosha leo ukiona shule zinatumia kiwango kilekile Cha uniform,,Mimi niliona anatunyima burudani ya kuona miguu ya bia ya toto's za miaka Ile miguu ya kina Trancy Tralumba nadhani unamkumbuka alikuwa anakaa frelimo,na Mademu wa highland ndiyo waliofanya ubunifu wa kuvaa viimin sketi. shuleni
 
Back
Top Bottom