Uchaguzi 2020 Wagombea Urais 2020 wasiendelee kujichosha

Mtukudzi

Senior Member
Nov 14, 2013
103
408
Inaweza kuonekana kama mzaha lakini amini nawaambieni mpaka leo tarehe 28 September 2020 watanzania wameishaamua ni nani awe Rais wao. Kwa hiyo mizengwe vitisho na maneno matamu ya wagombea wetu hayabadilishi maamuzi ya wapiga kura wa mwaka huu.

Taja makundi yote katika nchi hii, yote yaliamua nani wanaenda kumchagua siku ile NEC na ZEC walipotangaza wagombea wa vyama vyote. Kwa hiyo wanaolalamika kutopewa nafasi TBC na media wako sawa tu na wanaofurahi kupewa fursa kwenye vyombo hivyo.

Kwa chama tawala zile live coverage za mgombea wao wakati wote wa miaka 5 iliyopita inatosha kuwapa confidence na kuwaondolea unyonge wa nini kitatokea kwenye sanduku la kura. Kwa wapinzani watanzania wameishamchagua yule ambaye wanaona ni mpinzani halisi na hivyo wapo naye bila kujali itikadi zao ( tumeona Chadema ACT na baadhi ya makada wa CCM, NCCR na CUF).

Kampeni za mwaka huu zimeanza wakati watu wameishachagua upande. Kwa ajili hiyo wagombea Urais punguzeni presha zinazopelekea kuvunja sheria na maadili ya uchaguzi kwa sababu hamtabadilisha maamuzi ya wapiga kura wa safari hii. Kwa taarifa ni kuwa wapiga kura wanatamini iwe hata kesho wawafurahishe.
 
Kama hujui,kuna kundi kubwa la wapiga kura ambao huwa "undecided"!Hawa ndio huwa walengwa wa kampeni za uchaguzi!
Achana na makada ambao ije mvua lishuke jua wao huchagua chama chao!

So uzi wako ni upotoshaji mkubwa na hauna back up ya kiutafiti! Jipangeni kuandika mada za maana na zenye ukweli JF iwe na hadhi na heshima kama zamani!
 
Amini nakuambia nakuambia pattern ya mwaka huu haitafuata patterns za 'undecided' zilizo kichwani mwako. Makundi yote yameishaamua mpaka leo hii.
Kama hujui,kuna kundi kubwa la wapiga kura ambao huwa "undecided"!Hawa ndio huwa walengwa wa kampeni za uchaguzi!
Achana na makada ambao ije mvua lishuke jua wao huchagua chama chao!
So uzi wako ni upotoshaji mkubwa na hauna back up ya kiutafiti!
Jipangeni kuandika mada za maana na zenye ukweli JF iwe na hadhi na heshima kama zamani!
 
Ningependa sana Rais awe Tundu Lissu halafu waziri mkuu wake awe Magufuli Ila haiwezekani kabisa
 
Kuna watu/makundi ambayo kabla ya kampeni yalikuwa yanaunga mkono upande fulani na kufuatia kipindi hiki cha kampeni wamebadili uelekeo wa kura zao.

Pia kuna watu/makundi yaliyokuwa yamekata tamaa kushiriki uchaguzi na kupitia kampeni sasa wamehamasika kupiga kura.

Kuna wale walio jiaminisha wameshinda kabla ya uchaguzi na sasa baada ya hizi kampeni hawaamini wanachokiona.
 
Amini nakuambia nakuambia pattern ya mwaka huu haitafuata patterns za 'undecided' zilizo kichwani mwako. Makundi yote yameishaamua mpaka leo hii.
Unataka uaminiwe kama nani labda au kwa fact na data zipi ama kwa tafiti gani uliyofanya?

We mwenyewe hujiamini na Id yako feki afu unaongea kizembe tu uaminiwe.
 
D
Unataka uaminiwe kama nani labda au kwa fact na data zipi ama kwa tafiti gani uliyofanya?

We mwenyewe hujiamini na Id yako feki afu unaongea kizembe tu uaminiwe.
[/QUOTE
Ewe mwenye verified ID, dhambi yangu ni ipi hapo? Jenga hoja na data zako usilete povu
 
Amini nakuambia nakuambia pattern ya mwaka huu haitafuata patterns za 'undecided' zilizo kichwani mwako. Makundi yote yameishaamua mpaka leo hii.
Kwa utafiti upi uliofanya?Umewezaje kujua behaviour za wapiga kura?Msijitoe ufahamu kwa kiwango hiki!Huna utafiti unapataje ujasiri wa kutoa majibu ambayo hutolewa kwa tafiti?
 
Imenikumbusha Rombo Mramba aligeukwa siku 3 tu kabla ya uchaguzi
Mleta uzi alikuwa anapima kina cha maji kwa pua! Ukiona wakati wa kampeni mgombea anafokea wapiga kura na mengi mengine tunayoyaona, elewa fika ushindi wake hautegemei kura zao. Anazunguka tu kama zuga. Mkurugenzi wa NEC anampigia kampeni. Anamwita mshindani wake kwa jambo lisilo na tija. Amtoe kwenye reli. Amtafute ubaya kwa kumtekenya. Akicheka nongwa. Akishindwa kucheka muhali. Yote tisa, kumi TAL anaitwa na Mkurugenzi lakini ole ya kutoitikia wito inatamkwa na Polepole. Uchawi huwa kwa kificho ukijulikana hauna madhara tena.
 
Kama hujui,kuna kundi kubwa la wapiga kura ambao huwa "undecided"!Hawa ndio huwa walengwa wa kampeni za uchaguzi!
Achana na makada ambao ije mvua lishuke jua wao huchagua chama chao!
So uzi wako ni upotoshaji mkubwa na hauna back up ya kiutafiti!
Jipangeni kuandika mada za maana na zenye ukweli JF iwe na hadhi na heshima kama zamani!
Makada wa ccm ni wengi kuliko chama cha Mbowe. Wale undecided, tukiongeza kidogo biashara inakwisha asubuhi na mapema. Magufuli kiboko yao.
 
Back
Top Bottom