Wagombea udiwani wa CHADEMA waporwa fomu

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,305
33,924
Kwa taarifa za uhakika nilizonazo ni kwamba Wagombea wawili wa udiwani kupitia CHADEMA Bw. Andwear Palaiga wa Kata ya Gangilonga na Bw. Godfrey Lufyagila wa Kata ya Kwakilosa wameporwa fomu zao kwa nyakati tofauti na toka maeneo tofauti na watu wasiojulikana.

Inadaiwa kwamba wa kwanza kuporwa fomu hizo ni Godfrey Lufyagile wa Kata ya Kwakilosa ambaye aliingiliwa nyumbani kwake na mtu aliyefunika uso wake jana saa tatu usiku na kumtaka atoe fomu yake ya ugombea kwa usalama wa maisha yake.

Mtu huyo alivyochukua hiyo fomu aliondoka kwa Pikipiki aliyokuja nayo na mtu mwingine.Baada ya tukio hilo Mwenyekiti wa mtaa aliitwa na kupewa taarifa na Lufyagile tayari keshatoa taarifa kituo Kikuu cha Polisi mjini Iringa.

Tukio la pili limetokea leo Asubuhi wakati Mgombea wa Kata ya Gangilonga Bw. Palaiga alipokuwa anatafuta wadhamini kwenye mitaa ya Kata hiyo alipokutana na mtu aliyemnyang'anya begi lililokuwa na fomu hizo za ugombea. Inadaiwa unyang'anyi huo ulitumia silaha aina ya Bastola. Palaiga naye keshatoa ripoti kwenye kituo Kikuu cha Polisi mjini Iringa kwa msaada zaidi.

Uchaguzi kwenye Kata tano zilizo kwenye Manispaa ya Iringa Jimbo la Iringa Mjini unarudiwa baada ya Madiwani waliokuwepo hapo awalil kujiuzulu na kujiunga na CCM.
 
Huu uchaguzi ni lini? Nina wasiwasi na hawa wagombea wanacheza michezo. hizi form wasiachwe wakae nazo majumbani.
 
Ukitegemea msaada kutoka policcm kwa masuala yenye kuinufaisha ccm unakuwa unapoteza muda. Hapo wafanye initiatives nyingine kama kuna uwezekano. Lakini kuna uzembe kwa wagombea wengi ndani ya huu upande wetu. Sitashangaa ikiwa hata wagombea watakuwa sehemu ya waporaji.
 
Sasa Chadema kama mnafanyiana hayo maovu kwa kweli inaonyesha chama chenu hakina uongozi unaoheshimika..

Mmekuwa chama cha majanga.. mnatendeana na kutaka kusingizia wasiojulikana huku mnajuana na mipango ya kupanga kutafuta kiki za kura za huruma.. mnatia aibu taifa letu kwa upande wa upinzani. Kama hamjiamini na kulilia huruma kila mara muache tu siasa hamuziwezi.. kwanza hakuna mnalofanyia wananchi zaidi ya porojo zenu za kiki mbovu zisizoingia tena wananchi..

Kweli mnakimbizwa na awamu hii ya 5

Na bado mtapata tabu sana sanaaaaa
 
FB_IMG_1531499032556.jpg
Kwa ufupi ccm inachokifanya kwa jeahi la polisi ni kuhakikisha figisu wanafanyiwa upinzani na kumbuka jana mwenyekiti wa taifa wa uchaguzi alisema wataangalia taratibu za ujazaji fomu na urejeshaji kwa wakati kama kigezo cha kuwekwa kwenye list ya wagombea.

Sasa kinachofanyika ni kuwateka au kuwafunga wagombea ili wasirejeshe fomu, kingine wanabambikiza kesi kwa wagombea, wakikukosa wanakuita mezani, ikishinfikana unapotezwa.
 
CCM Bila polisi ni wepesi kuliko pamba , Baada ya Magufuli kuiua ccm kifo cha kikatiri sana , tegemeo pekee ni polisi , ikumbukwe kwamba ccm haiungwi mkono hata na wanachama wake
 
Sasa Chadema kama mnafanyiana hayo maovu kwa kweli inaonyesha chama chenu hakina uongozi unaoheshimika..

Mmekuwa chama cha majanga.. mnatendeana na kutaka kusingizia wasiojulikana huku mnajuana na mipango ya kupanga kutafuta kiki za kura za huruma.. mnatia aibu taifa letu kwa upande wa upinzani. Kama hamjiamini na kulilia huruma kila mara muache tu siasa hamuziwezi.. kwanza hakuna mnalofanyia wananchi zaidi ya porojo zenu za kiki mbovu zisizoingia tena wananchi..

Kweli mnakimbizwa na awamu hii ya 5

Na bado mtapata tabu sana sanaaaaa
Mawazo ya kuzamia meli big up.
 
Back
Top Bottom