Ngurubhe
JF-Expert Member
- Jul 26, 2014
- 1,840
- 1,049
Nimejarbu kupita karibu shule zaidi ya 300, nikitembeza vi-handouts kwa masomo mbalimbali. Awamu ya kwanza nilitembeza mkoa wa Dar es salaam, kisha Iringa, Moro, dom, singinda na Tabora. Nilikutana na walimu kadhaa maofisini wakiwa na ari ya kufany kazi sana. Hata wengine walininyima kabisa muda wa kuwashawishi wanafunzi kununua handout zangu, kuwa hawana muda.
Nimepita awamu hii hasa kwa mikoa hii hasa wakati huu yaani baada ya mwezi JULY kuja bila ongezeko WALIMU WALIO WENGI WAMEKATA TAMAA. WANAFANYA TU KWA SABABU HAWANA NAMNA NYINGINE.
LAKINI KUNA KITU NIMEGUNDUA JAPO KINAWEZA ONEKANA KIDOGO, KUWA mkoa wa dar es salaam unawalimu wa kike wengi sana ukilinganisha na shule za huko mikoani.
Madhara yake walimu walio wengi wakipata mimba, au akijifungua ndo hafanyi kazi tena effectively. Na watoto wanakuwa hawana mwl japo anahesabika yupo!
Kwa utashi wangu mdogo walimu wa kike pia wanashindwa kupambana na aina ya wanafunzi watukutu wa dar hii inapelekea Dar kufanya vibaya kitaluuma kitaifa. Puuzeni lakini nimeyaona hayo...
Sent using Jamii Forums mobile app