Wafanyabiashara wagoma nchi nzima

Wafanyabiashara wagoma nchi nzima

Waailete za kuleta, janja ya kutaka kwepa kodi hakuna sasa. Hela inahitajika, uchaguzi umekaribia
Mkuu majebere, umesema pesa hiyo ya kodi inahitajika sana na serikali ya Sisiem, kwa kuwa uchaguzi umekaribia, unataka kutuambia mnazihitaji sana pesa hizo ili mkanunulie fulana, khanga na kofia, ili muwahonge wananchi, na kuwafanya wapiga kura hao kuwa mabango yenu ya matangazo, kwa kuvalia sare hizo za chama chenu cha magamba?

Kama lengo la serikali hii ni kuzisaka kwa udi na uvumba, pesa hizo za kodi ili waxipeleke kwenye kampeni kwa ajili ya kukinufaisha chama kimoja, ni vyema wafanyibiashara hao wakaendelea kukomaa na msimamo wao huo huo.
 
Wafanyabiashara leo tarehe 27 wamegoma nchi nzima kwa madai ya kutaka kukutana na serikali TRA kujadiliana njia bora zaidi ya kulipa kodi tofauti na ilivyo sasa ambapo wafanyabiashara wanakandamizwa na sheria mpya ya kodi ilipitishwa na Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kulipa kodi siyo tatizo, tatizo ni hizo kodi zinaliwa na wachache. Kwanza ccm iondoke ndiyo watu watakuwa na imani na kulipa kodi
 
Taarifa nilizonazo ni kwamba mgomo umestishwa, nimepita Kariakoo asubuhi hii naona baadhi ya maduka yanafunguliwa
 
Ngoja ifike mwezi July utaona yote yataisha na serikali itadai kuwa tayari kuwasikiliza wafanyabiashara na hata mwenyekiti wao kesi itafutwa tu.
UCHAGUZI HUU!!
 
Anzeni ushawishi "lobbying" ili ifanyiwe marekebisho. Lakini lendila biashara ya kuuza kuku zilizookwa pale Nairobi na Mtu mwenye duka Kariako nani mfanya biashara mkubwa? kwa nini yule muuza kuku na kababu pale Nairobi atumia machine ya kodi ya kutolea risiti ninyi wenye maduka ya Jumla kariakoo msitumie machine za TRA?

Mkuu kwanza TRA hawathamini taarifa za mashine za EFD.

Binafsi natumia hii mashine. Juzi nilienda TRA nikakadiriwa kulipa kodi mara 2 ya niliyolipa mwaka jana.

Nilipouliza kwa nini wasikadirie kutokana na taarifa za mashine ya EFD nikaambiwa hawana hakika kama inatumika kama inavyotakiwa!!

Nilishangaa sana, nikajiuliza kwa nini watu walazimishwe kutumia EFD machines wakati TRA wenyewe hawaamini watumiaji?!
 
Last edited by a moderator:
Jamani ninavyo juua sisi wafanyabiashara hatuna maslahi na nchi yetu bali pale mambo m,agumu yanapo tukuta.

Niseme tu asilimia kubwa ya wafanyabiashara hawajitokezi kukemea maovu ya serikali na hata mara nyingi huponda wale wanao kuwa najicho la kuikosoa serikali.Sheria hizi zilipitishwa bungeni kwa kura ya ndiooo na waliowengi wakafurahia chama cha ndiooo kufanikiwa.Ushauri wangu vaeni uzalendo kwanza na ujasiri wa kuona nyanja zote zinatendewa haki nasisi tutajikuta tukipona kwa ujumla wake.

Wafanyabiashara leo tarehe 27 wamegoma nchi nzima kwa madai ya kutaka kukutana na serikali TRA kujadiliana njia bora zaidi ya kulipa kodi tofauti na ilivyo sasa ambapo wafanyabiashara wanakandamizwa na sheria mpya ya kodi ilipitishwa na Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania.
 
Ss wafanyabiashara nia yetu ni kukaa na serekali meza moja tupange njia nzuri zaidi ya ulipaji kodi wa haki sasa kuna ubaya gani kama nia ni kukaa na wafanyakazi wetu tuliyowajiri wenyewe

Wafanyabiashara wengi hamtumii akili....hauwezi kuipangia serikali ila serikali ndo inayopanga KODI....mlizoea kukwepa KODI....mbona wafanyakazi wanakatwa Direct kwenye mishahara yao siku zote.....mshahara mil 2 kwa mwezi kodi karibu laki 3....
....sasa nyie kwa mwezi wengine mnaingiza zaidi ya million 200 unataka kodi iwe laki 3 kwa mwezi kama mfanyakazi aliyeingiza mil 2......Elimu inasaidia kujitambua.....Lipeni Kodi ndo mtakuwa na Akili kuchagua viongozi wanaofaa....hiki kilio cha kodi kwa wafanyakazi ni cha siku nyingi nyie mlikuwa MNAKENUA MENO TU
 
Sipati picha siku ambayo itatoka mgomo wa makini haya kwa siku moja, Wafanyabiashara(Kodi kandamizi) , Walimu(Mishahara duni), Madaktari(Mishahara na Mazingira ya ovyo kaka hospital zetu) , Wanafunzi wa vya vikuu(Mikopo), Machinga na Mamalishe (Manyanyaso toka Halmashauri zetu), Bodaboda(Manyanyaso toka Polisi na Fire Extinguisher) Daladala(kubadilishiwa vituo bila kushiriki sawa kama ilivyotokea hivi karibuuni jijini Mza)
 
Waailete za kuleta, janja ya kutaka kwepa kodi hakuna sasa. Hela inahitajika, uchaguzi umekaribia

Wasiotaka kununua mashine za efd wanyang'anywe leseni za biashara. Kodi ni lazima ilipwe kutokana na mapato na efd ndiyo itaonyesha mapato halisi. Wafanyabiashara ni wakwepaji wakubwa wa kodi. Wafanyakazi ndiyo wanalipa kodi kulingana na mapato yao. Tra iwaorodhesha wote waliogoma na kuhakikisha wanafutiwa leseni zao za biashara.
 
Huwezi kuelewa jambo hili linawaumizaje hao wanaodai haki yao hadi uwe mfanyabiashara na unayelipa kodi.
Ndio utawaelewa hao watu, kinyume na hapo utakuwa unaongea tu kufurahisha nafsi.

Kila jambo linahitaji uelewa ndio uchangie kile unachokijua Binafsi ni mfanya biashara na kodi nalipa tena vizuri tuuu tatizo mfumo wetu hauko sawa ndio maana wafanyabiashara wanalalamika na naamini busara ingetumika wakakaa meza moja wakatoa hoja zao na Bwana mkubwa SERIKALI akajibu hoja zao ll.... Lkn hili la kutumia ubabe bila kujibu hoja mm naona kuna tatizo kama kweli mtu anaona anaumia kwa nn asiseme? Na anapolalamika kwa nn asisikilizwe? Ina maana lipo ambalo sio sahihi na ndio maana SERIKALI haitaki kujadiliana na wafanya biashara. Biashara ni ngumu kodi imeongezwa mara mbili na hawataki kusikia kuwa mauzo yameshuka wanachojua wao kila siku mauzo yanaongezeka tuuu .Hivi kweli kama hali ingekua hivyo si kila mtu angefanya biashara? Bado tuna nafasi ya kukaa chini na kujadiliana. Na huu mfumo wa kupitisha sheria bila kuwashirikisha wadau ni mbaya kwa sababu anaetunga hiyo sheria yupo kinadharia zaidi na anaetakiwa kuitekeleza yuko kivitendo zaidi hivyo ingekua busara akashirikishwa mlengwa ili achangie mawazo yake kama mtekelezaji wa hiyo sheria na sio huu utaratibu wa wanaoafiki waseme ndiiooooooooo
 
Kumbe wanaogoma ni wachuuzi maana hata kina Mengi, Manji, Barharesa, Mimi ni wafanyabishara lakini hatuko kwenye mgomo. Manaposema wafanyabishara wote wamegoma mnakuwa hamjatenda haki kwa wengineo ambao hatuna tatizo na mashine za TRA kwa sababu hatuna cha kuficha.


Tukana uwezavyo lakini kodi ni lazima kwa maendeleo na ustawi wa taifa letu la Tanzania. Ni suala la wakati tuu lazima sheria za Nchi zifuatwe. Umoja wenu ungekuwa na maana kama mngepenyeza ushawishi wakati ule sheria ya EFD Machine inatungwa lakini siyo sasa

Nchi hii inaendeshwa kwa sheria, kanuni na taratibu! Kulipa kodi ni wajibu wa kila mtanzania na hata katika maandiko hilo lipo jamani. Hatuwezi kuendelea kuwaachia wafanyakazi mzigo huu wa kulipa kodi. Kila mtu kwa kazi na nafasi yake atimize wajibu wake. Wafanya biashara lipeni kodi, wafanyakazi hasa wa serikali hakuna mjadala juu ya kodi wanakata hukohuko, wachuuzi lipeni kodi.
Lakini na ninyi serikali timizeni wajibu wenu mnaokusanya hizo kodi mtumie fedha hizo kwa linalokusudiwa na walipa kodi tuone zinavyotumika kama ni hiduma tuzipate inavyostahili sio muzihamishie mifukoni mwenu na kujifungulia akainti uswis. Matendo yeni Kibinadamu Mnatufanya tusione sababu ya kulipa kodi.
Tusimame tujenge nchi yetu kwa uaminifu upendo na mshikamano.
 
Wasiotaka kununua mashine za efd wanyang'anywe leseni za biashara. Kodi ni lazima ilipwe kutokana na mapato na efd ndiyo itaonyesha mapato halisi. Wafanyabiashara ni wakwepaji wakubwa wa kodi. Wafanyakazi ndiyo wanalipa kodi kulingana na mapato yao. Tra iwaorodhesha wote waliogoma na kuhakikisha wanafutiwa leseni zao za biashara.

Efd ni tatizo kuna jamaa yangu anatumia hiyo mashine ameenda kukadiliwa kaambiwa alipe Mara 2 ya mwakajana. Alipohoji kwa nn wasitumie taarifa za efd wakamwambia hawaamini kama taarifa zimeingizwa sahihi. Hakuna umuhimu wa kununua mashine hizo
 
Efd ni tatizo kuna jamaa yangu anatumia hiyo mashine ameenda kukadiliwa kaambiwa alipe Mara 2 ya mwakajana. Alipohoji kwa nn wasitumie taarifa za efd wakamwambia hawaamini kama taarifa zimeingizwa sahihi. Hakuna umuhimu wa kununua mashine hizo

Kamishina Mkuu wa mamlaka ya mapato acha siasa we siyo waziri wa fedha. Waache wanasiasa wapige kelele ww fuata sheria kusanya kodi halali na usionee mtu. Ondoa wala rushwa wote na usiheshimu vimemo hata vya ikulu kuhusu misamaha ya kodi isiyo ya kisheria. Wakikufukuza kazi sisi tutawashughulikia kwenye sanduku la kura na tutakurudishia cheo chako. Tumechoka kuomba budget support wakati uwezo tunao.
 
Back
Top Bottom