Wafanyabiashara kudaiwa pesa za Mwenge

Wafanyabiashara kudaiwa pesa za Mwenge

Huo mwenge na kuchangia pesa za mafuta ya mwenge ilianzia wakati wa Nyerere.

Ni wakati muafaka tukaachana na hayo makosa ya Nyerere, yeye mwenyewe alishasema yeye si malaika na kuna makosa katika aliyoyafanya, basi tuyaache.

Nyerere mwenyewe baada ya kung'ang'ania sana, akaamuwa kung'atuka na kuwacha wengine walete mapya, sisi tunang'ang'ania tu.

Kwani kuna ubaya gani tukitengeneza Mwenge unaotumia nishati ya Jua?
 
Habari,

Jamani naomba msaada wetu, mitaa ya home tuna kitigo pesa kidogo, na nmekianzisha baada ya kukosa ajira juzi wamekuja watu wa serikali za mitaa wanadai pesa za mwenge eti 10000, daa mimi sina na tangu nikue hii ni mara ya kwanza kusikia hili.

Naomba mnijuze hii ni nini na kwa nini wanatuchangisha, na usipochanga nini kinatokea?

Usiwape hata senti moja waambie wakachukue ikulu
 
Back
Top Bottom