kende
JF-Expert Member
- Dec 2, 2013
- 3,527
- 1,669
Hawa ni watu ambao kwa mtazamo wangu wana impact kubwa sana kwenye huu mziki wa kizazi kipya "Bongofleva", yaani wameacha alama ambayo haitakuja kufutika vizazi na vizazi, wametoa hamasa kubwa kwa wasanii wengine wa miaka ya kuanzia 2000 na kuendelea;
1. JOSEPH MBILINYI (SUGU)---Huyu ndo msanii aliyeanza kurap siriaz kwa kutumia Lugha ya kiswahili na kukubalika na vijana wengi katikati ya miaka ya 90, akafanikiwa kurelease albam nyingi na kuwafanya wasanii kibao kupata confidence ya kufanya alichokuwa anafanya.
2. JOSEPH HAULE (PROF JAY)----Huyu aliendeleza alipoishia Sugu, kupitia huyu Bongofleva ilitanua fanbase kwa kiasi kikubwa, alifanikiwa kuondoa ile zana kwamba mziki (esp Hiphop) ni uhuni, watu wa rika tofauti wakaanza kusikiliza Bongofleva na kuachana na muziki wa kikongo na taarabu vilivyokuwa vimetawala sana enzi hizo.Wasanii pia walistuka, wakaanza kutunga vitu vya maana. Wimbo wake wa alioufanya akiwa na HBC "CHEMSHA BONGO" ulileta mapinduzi makubwa kwenye muziki huu
3. JUDITH WAMBURA 'LADY JAYDEE'----Alianza game kwa kusuasua, alitoa nyimbo mbili tatu ambazo hazikupata attention ya kutosha kabla ya kuachia 'BOMU' wimbo unaoitwa MACHOZI ambao ulikuwa kama wimbo wa taifa enzi hizo, ukiukosa redioni unaukuta kideoni. Naweza kusema video ya MACHOZI ndio video bora ya kwanza kuachiwa na msanii wa bongofleva, kwa wakati huo ilikuwa inaonekana video babkubwa na ndipo wasanii wakaanza kustuka kwamba na Bongo tunaweza kufanya video kali.Wimbo huo ulimpa mafanikio makubwa ndio maana neno 'Machozi' hadi leo hii bado analitumia kwenye biznes zake. Hata hivyo Jide hauishia hapo, aliendelea kutoa nyimbo n' album nyingi zilizofanya vizuri sokoni. Hadi leo hii haijatokea msanii wa kike aliyeweza kuwa consistent kwenye game kama yeye, ndio maana hadi leo hii zikiandaliwa tuzo, msanii bora wa kike anakuwa yeye hata asipokuwa na single inayobamba hewani.
# Tupia jina la msanii ambaye sijamtaja hapa ambaye unadhan anastahili kuitwa LEGEND
1. JOSEPH MBILINYI (SUGU)---Huyu ndo msanii aliyeanza kurap siriaz kwa kutumia Lugha ya kiswahili na kukubalika na vijana wengi katikati ya miaka ya 90, akafanikiwa kurelease albam nyingi na kuwafanya wasanii kibao kupata confidence ya kufanya alichokuwa anafanya.
2. JOSEPH HAULE (PROF JAY)----Huyu aliendeleza alipoishia Sugu, kupitia huyu Bongofleva ilitanua fanbase kwa kiasi kikubwa, alifanikiwa kuondoa ile zana kwamba mziki (esp Hiphop) ni uhuni, watu wa rika tofauti wakaanza kusikiliza Bongofleva na kuachana na muziki wa kikongo na taarabu vilivyokuwa vimetawala sana enzi hizo.Wasanii pia walistuka, wakaanza kutunga vitu vya maana. Wimbo wake wa alioufanya akiwa na HBC "CHEMSHA BONGO" ulileta mapinduzi makubwa kwenye muziki huu
3. JUDITH WAMBURA 'LADY JAYDEE'----Alianza game kwa kusuasua, alitoa nyimbo mbili tatu ambazo hazikupata attention ya kutosha kabla ya kuachia 'BOMU' wimbo unaoitwa MACHOZI ambao ulikuwa kama wimbo wa taifa enzi hizo, ukiukosa redioni unaukuta kideoni. Naweza kusema video ya MACHOZI ndio video bora ya kwanza kuachiwa na msanii wa bongofleva, kwa wakati huo ilikuwa inaonekana video babkubwa na ndipo wasanii wakaanza kustuka kwamba na Bongo tunaweza kufanya video kali.Wimbo huo ulimpa mafanikio makubwa ndio maana neno 'Machozi' hadi leo hii bado analitumia kwenye biznes zake. Hata hivyo Jide hauishia hapo, aliendelea kutoa nyimbo n' album nyingi zilizofanya vizuri sokoni. Hadi leo hii haijatokea msanii wa kike aliyeweza kuwa consistent kwenye game kama yeye, ndio maana hadi leo hii zikiandaliwa tuzo, msanii bora wa kike anakuwa yeye hata asipokuwa na single inayobamba hewani.
# Tupia jina la msanii ambaye sijamtaja hapa ambaye unadhan anastahili kuitwa LEGEND