Waepuke wapenda drama

Waepuke wapenda drama

Matunzo 02

JF-Expert Member
Joined
Jul 7, 2026
Posts
1,006
Reaction score
2,041
Hawa ni watu ambao kwenye utoto wao hawakuwa na watu waliowajali hivyo walijifunza drama ili kuwateka watu wawajali

Huwa hawana chochote kinachoweza kuwafanya watu wawajali na kuwafuatilia zaidi ya drama zao.
Hawa huwa wazuri sana kwenye kutengeneza mambo na kuigiza kwa namna ambayo wataonekana wanaonewa na wanahakikisha wanategeneza huruma.

Hakikisha unasi maana kujinasua ni ngumu ukitaka kujinasua wanakufanya ujione unahatia
Utawajua kwa mapito yao ya nyuma.
 
Pia watu wenye tamaa ni hatari kwelikweli
FB_IMG_17875745299930669.jpg
FB_IMG_17875745273180744.jpg
FB_IMG_17875745334288524.jpg
FB_IMG_17875745363207697.jpg
FB_IMG_17875745387110743.jpg
 
Wapenda drama ni wale watu wanaotumia maigizo ili wapate huruma mfano anasema anaumwa ili apate pesa mara kuna msiba yeye anapata jambo mbaya tu waogope sana
Weng wao ni wanawake
 
Manipulators, ukijua namna ya kuishi na hawa watu hautateseka sana.

Mtu unaishi nae ghetto moja ila sasa unaona kabisa anayoyafanya ni mambo ya hovyo, uwezo wa kumfukuza unao ila kila ukitaka kumfukuza unashindwa ni kama anakusoma mapema sana anakutengenezea mazingira mapema sana siku ukitaka kumfukuza unaona kabisa unakosea unaamua kuendelea kukumbatia bomu kwa upendo mkuu..

Kuna kipindi nilikuja kugundua kuwa ukienda ugenini ili ukae pale kwa muda mrefu sana kwanza mtu wa kujenga uhusiano mzuri ni mtoto au watoto wa pale kisha mama yao kwa upande wa baba mwenye nyumba huyo hata mkiwa hamuelewani ni sawa tu utakaa muda unao utaka wewe iwapo una maelewano mazuri na watoto na mama mwenye nyumba, hii ni aina ya manipulation.

Kuna msichana niliwahi kumpenda sana lakini kadri siku zilivyokuwa zinaenda nikawa naona kabisa ameanza kuingiwa na tamaa nikaanza kutengeneza mazingira ya kunikosea yaani kitu kidogo tu ila akisema anifokee mimi simjibu halafu baadae anakuja ananiomba msamaha yeye mwenyewe na wakkati hana kosa.

Na hawa manipulators wengi ndio huwa ni playboys na playgirls.. Yaani anaplay victim kudai kuwa anakupenda mpaka unahisi huyu sasa nikisema nimuache anajiua halafu ukimuacha ana moveon..

Na uwezo wa kufanya haya yote nadhani huwa ni uwezo wa kuzaliwa nao sio kila mtu anaweza kufanya hivyo.
 
Kila mtu anacheza drama katika game of life.
Hata mchungaji hucheza ili apate wafuasi
Everything you see is Fake.
Watu, maisha, nguo, kazi yaani kila kitu unachokiona ni Fake.
Kitu pekee ambacho ni halisi ni wewe mwenyewe lakini kila kitu kilichobaki ni Fake!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom