Wadogo zangu mmh!

Wadogo zangu mmh!

kuntubaby

Senior Member
Joined
Dec 29, 2016
Posts
187
Reaction score
202
Habari wakuu,
Hivi mtt wa kiume hadeki choo au bafu? kuna ubaya mtt wa kiume akijifundisha kazi ndogo ndogo za nyumban eti?. Huyu mdg wangu wa kiume yupo likizo, kutwaa anashika simu ana groups za whatsapp zaid 20, yes zaid ya 20 yani namshangaa ad nachoka kushangaa. Ukimuelekeza kitu yy haoni tabu kukujb sitaki au fanya mwenyewe yan ana kejeli kama zote tu.
Huyu wa kike sasa, kamaliza chuo juzi karud na mimbaa, ss jmn mwenye mimba hawezi hata kuosha vyomba? Vikaz vdg dg kufanya haruhusiwi?. Nikimuelekeza nae utasikia (hujui uzito nnaousikia, omba Mungu akujalie asipokujalia basi hautoexperience mimba) arghh! nmewachoka . Mm sishindi na wao, naenda mishe mishe narud usiku na nikirud nalala tu sitak kelele na mtu, lkn ukirudi unakuta hamna jipyaa, nyumba chafu na tangu arudi huyu wa kiume ndo imezidii kwasabb yy ndo anashndaa home muda mwingi, huyu wa kiume yupo miguu juu kashika simu (na nmempa mimi hapa nawaza kuchukua simu yangu tu) huyu wa kike nae yupo busy na Sultan, ataamka Mama we flani tupikie ugali......... M nikiamka asbh hufagia na kuosha vyombo vya usiku (nafanya kupunguza kaz kdg maana huyu mjamzito eti hajiwez so kumuachia kazi bimkubwa alone naona sio vzr). Ss haya mambo Mpaka lini? Kama leo chakula cha night ugali na mlenda ndo unapikwa ss hivi, tena Mama umekuja kuniamsha nipike, sio kwamba nimegoma nmejiulza tangu saa12 ad sasa hv kimefanyika nini kikubwaaa kias mkose kula mapema mle sasa hv au ndo housegal nilkua nasubiriwa.............???Najua Mama una mahaba na hawa wanao lkn mimi ni dada yao, silazimishi waniheshimu but Respect ni Muhimu!
 
Mambo yangu hayaja nyooka bado,

Then inabidi uvumilie hayo majukum kama bado huna uwezo wa kuondoka hapo...waswahili wanakwambia ukubwa jalala subiri na huyo mdogo wako ajifungue ndio upate akili
 
Japo sishauri tabia yake ya kushinda na simu kutwa, ila swala la mwanaume kudeki chooni au kuosha vyombo wakati wanawake wapo siafiki!

Mwanaume ni mwanaume tu hata awe na umri wa miaka 5
 
hujui kushika kiboko! hivi umesema ndo unapiga ugali au ndo unapost kwanza uzi hapa oke Nimekumbuka mungu atakujalia upate nawe ka mimba mdogo wako kasema hivyo etiii
 
Je alipokuwa hana mimba alikuwa hvyo hvyo.???

Huyo wa kiume dawa ni ndogo sana, Chukua simu yako then kitendo cha yeye hadi apate simu kwa hela yake atakuwa amesha nyooka na kujifunza kitu..

BTW acha kulalamika, utakuja kuolewa halafu mmeo alete ukoo mzima na wewe ndio unapiga kazi home (inatokeaga likizo ndgu wote wakaja kwenu)
 
Japo sishauri tabia yake ya kushinda na simu kutwa, ila swala la mwanaume kudeki chooni au kuosha vyombo wakati wanawake wapo siafiki!

Mwanaume ni mwanaume tu hata awe na umri wa miaka 5
mkuu huo mfumo dume kizamani, mie hadi namaliza kidato cha 6 naonsha vyombo, napika, nadeki na kufua. sio mimi tu familia nzima na hapo dada wa kazi yupo wakati mwingine anaona tv ww unafanya kazi.

bi mkubwa anakwambia :huyu dada nimemleta anisaidia kazi mimi sio nyie" ratiba zenu ziko pale pale.

leo naona faida yake kazi zote twende, sema hasara yake pia ipo naona hakuna wa kufanya kazi kama navyo taka mimi hata kufuliwa huwa staki
 
Back
Top Bottom