Wizara ya Madini
Govt Institution
- Apr 12, 2025
- 47
- 19
Jukwaa hilo linafanyika jijini Mwanza katika Viwanja vya Malaika Beach Resort, limeanza leo Juni 16, 2025 na linatarajia kuhitimishwa Juni 18, 2025 ambalo linahusisha wadau wakiwemo kutoka kampuni za uchimbaji, watoa huduma migodini, taasisi za Umma, na wengine.
Katika jukwaa hilo linakwenda sambamba na maonesho ya madini, TGC ni miongoni mwa taasisi chini ya wizara zinazoshiriki ambapo kimepata wasaa wa kuelimisha kuhusu mafunzo na huduma mbalimbali zinazotolewa na kituoni hapo.
Mafunzo yanayotolewa na kituo hicho ni kuanzia ngazi ya cheti na diploma katika huduma za utambuzi madini ya vito, utengenezaji wa tuzo (trophy) za miamba na vito, ukataji madini ya vito, pamoja na utengenezaji bidhaa za usonara.
Wadau wanakaribishwa kutembelea banda laTGC, kujiunga na mafunzo hayo kwa kujaza fomu za maombi zinazopatikana katika banda la TGC na kwenye tovuti www.tgc.ac.tz. au kupitia namba +255 737 816 121.