Wadanganyika dini yao ya pili ni "ubinafsi"!

Wadanganyika dini yao ya pili ni "ubinafsi"!

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
52,144
Reaction score
162,541
Hivi ndivyo ninavyoweza kusema kuhusu wadanganyika kwani ni watu ambao ubinafsi umewatawala kwa kiwango kikubwa ambapo karibu kila mtu anaangalia masilahi yake bila kujali ni watu wangapi waanathirika au kuumia na jambo fulani ambalo yeye analitetea au kuliunga mkono kisa tu yeye anafaidika hata kama maelfu, mamia au makumi ya wanaomzunguka wanaathirika na jambo hilo.

Kwa hiyo, no wonder mtu anapigwa risasi hadharani wako watu wanatetea na kusema huyo si wa kwanza na kwamba hilo ni jambo la kawaida tu

Similarly, no wonder wakati watumishi wanalilia nyongeza ya mishahara n.k kuna watumishi wenzao wanawebeza na kuwaambia kama mishahara haitoshi waache kazi au kuwaambia zama zimebadilika na maneno mengine kama hayo kisa tu ndugu yake ni kada, mjomba wake kapata uteuzi, n.k.

Wengine wakipewa vyeo au wakiwa kwenye system, ama wanachagua kukaa kimya au kuwabeza wanaopinga au kulalamikia hali ngumu ya maisha ila wakitoka, nao wanaanza kulalama utadhani sio wale waliokuwa wamechagua kukaa kimya au kubeza wengine.

Hiyo ni mifano michache miongoni mwa mingi kuwahusu wadanganyika inayothibitisha kuwa dini yao ya pili ni ubinafsi na ndio maana wako tofauti sana na watu wa mataifa mengine katika kupigania haki zao.

Badilikeni na si kusubiri mpaka kila mtu yamkute ndio muungane kupigania haki zenu.
 
Hongera bwashee kwa kuchangia 10m.....hii imedhihirisha wewe ni mtu wa watu!
 
Ubinafsi kwa binadamu upo tangu enzi na enzi sio kwa watanzania tu. Wewe kwanza wengine baadae sio wao kwanza afu wewe baadae haipo hiyo ndugu tusidanganyane ila tu useme tumetofautiana katika hali ya kujali ya wengine (matatizo) ila sio ubinafsi huo upo kwa kila mtu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom