Wiki iliyópita imenibidi nimrudishe kwao kwa kumshtukiza yaani bila kuwambia maana nliona kwa miez 8 tuliekaa nae alikuwa amebadilika sana. Alianza kuonyesha kachuki na kiburi kwa mke wangu huku akionekana kunichangamkia kuliko kawaida na vituko vya kunitega vya hapa na pale. Ilinkera sana, nikakubaliana na mke wangu tumwondoe kwa sabcu ya kiburi na dharau japo sikumwambia vitimbwi kadhaa nlivofanyiwa kwa hofu ya kisasi kutoka kwa mke wangu kwa binti yule. Angalizo: akina baba tuwe makini na wadada wa ndani kwani usipo chukua hatua mapema waweza kuliswa limbwata na kuharibu familia yako .