Wachina wanatorosha madini yetu

Sasa kuanzisha thread humu haitoshi,huko uliko kuna mamlaka husika ingefaa zaidi kama ungetoa taarifa .

Pili swala la kusafirisha mchanga au makinikia nje ya nchi bado tuu halijamalizwa na Serikali? Au wakati wanawaruhusu Barrick vipi kwa wachimbaji wengine?..

Waziri mhusika na watendaji wengine chukueni hatua.

Mwisho , nadhani kuna shida sana huko uhamiaji,hawawezi.ku track wageni wanaoingia Nchini?
 
safari imeanza,kwa nchi yetu hii hayo Mambo inabidi tuyazoee tu Sasa tutafanyaje!! maana ukifikiria Sana unaweza kuwehuka au kwenda kumzaba makofi mtu!!
Usiwe mjinga mkuu madini kutoroshwa imekuwa.hivyo mda mrefu imagine licha ya kujegwa ukuta na kuweka wanajeshi merelani Bado Madini yakiendelea kutoroshwa hadi Chief Hangaya akahoji maana has ya kujenga ukuta.

Licha ya kulinda bandari na wanajeshi Bado upigaji uko pale pale kwa hiyo haya mambo ni ishu za maadili zaidi kuliko mechanical means.

Tena kwa taarifa yako itoroshaji ni mkubwa sana hasa mikoa ya Ruvuma, Morogoro,Katavi na huko Kaskazini.

Tuangalie namba ya kufanya sokonla Madini ndani ya nchi liwe na tija zaidi maana wengi wanaenda kuuzia japo Kenya na Afrika Kusini.
 
Kutujulisha sisi unatutia hasira tu, bora hata ungepiga simu wizarani mbona namba zipo?
Humu hauko peke yako na hapa ni njia sahihi kabisa kutolea taarifa sensitive ambazo zina athiri kipato haramu cha watu hivyo kutoa taarifa kama hizi kwa uwazi ni kujiweka hatarini sana
Si tuliambiwa TISS wako kila mahali vipi hapo hawapo?
Hili swali huwa najiuliza sana hata mimi au pengine hayo sio sehemu ya majukumu yao.
 
Yupo sahihi sana kuanzisha uzi huku kwa kwa sababu za kiusalama huko mnako taka aende mnataka apotelee kusiko julikana maana huwezi jua nani yupo nyuma ya hawa wachina
 
Yupo sahihi sana kuanzisha uzi huku kwa kwa sababu za kiusalama huko mnako taka aende mnataka apotelee kusiko julikana maana huwezi jua nani yupo nyuma ya hawa wachina
Ni kweli mkuu! maana nitaharibu kipato cha watu!
 
Itafika muda, tutaanza kuchukua sheria mkononi. kulinda rasilimali zetu!
Inaumiza sana.
Lakini matumaini yangu ni kuwa haitatulazimu kufika huko. Tuendelee kuwapigia kelele hawa watu wanaoshiriki katika kulihujumu taifa lao. Hawa ndio maadui wakubwa zaidi tunaotakiwa kuwashughulikia kwa njia zote zinazowezekana.
 
inasikitisha sana kwa kweli
 
Kaka kazi za kuoperator excavator vipi huko zipo huko migodini mleta mada na yeyote anayejua
 
Hiyo ni kazi ya TISS ,
 
Suala sio kuamini kuna basis ipi ya kuyaamini.
Wewe unawezaje kuamini?
nishawai fanya kazi, na nikayaona mambo yanayofanana na hayo..

sema unakua huna pakureport,
mana ao jamaa wana connection aisee,
unaweza ishia kukosa kazi tuu
 
Kama ni kweli basi huu ni uzembe wa hali ya juu wa vyombo vinavyohusika. Hata wakiwa na vibali vyote ni lazima kuwe na monitoring ya kutosha bila hivyo tutaendelea kuwa shamba la bibi.
 
Taarifa ulizotoa ni za muhimu sana ila ungezipeleka kwa wahusika ungeokoa pesa nyingi za taifa hili

Tatizo hizi taarifa zikishapelekwa kwa watu unaofikiri wataleta suluhu, wao wanazigeuza mtaji na wanachofanya ni kuona namna gani watanufaika. Uzalendo tunauhubiri majukwaani lakini hali iko tofauti sana.

Ntwike, jengelyangulu, Shelui, Mgongo, Nkonkilangi nimeishi sana hayo maeneo miaka ya 88-94 nikiwa Primary.
Nakumbuka kulikua na maeneo yenye madini hasa hapo Sekenke ( Nkonkilangi).
 
Inauma sana! Nchi yetu imeshakuwa shamba la Bibi mpaka basi!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…