Wachimbaji visima vya maji safi na salama

Wachimbaji visima vya maji safi na salama

Villanova tito

Senior Member
Joined
Dec 20, 2016
Posts
148
Reaction score
154
UTARATIBU WA KUCHIMBA KISIMA.

1. Ukitaka kuchimba kisima unatakiwa kufanya utafiti wa awali ili:-

● Kuangalia jiolojia ya eneo husika

● Kuangalia uwezekano wa kuwepo mikondo ya maji ardhini

● Historia ya eneo husika kuhusiana na suala la maji.

2. Gharama za kuchimba kisima/Visima hutegemea zaidi mambo yafuatayo:-

● Kipenyo na kina cha kisima pamoja na bomba zitakazotumika katika ujenzi.

● Aina ya mwamba utakaotakiwa kutobolewa.

● Umbali wa eneo la kuchimba kisima kutoka mahali ilipo mitambo yetu ya uchimbaji.

● Bei ya vifaa na mafuta (Dizeli) kwa wakati husika.

● Hali ya mazingira ya sehemu kitakapochimbwa kisima, mfano kama hakuna barabara, hivyo kuhitaji matengenezo ya njia ya kupitishia mitambo.

● Wingi wa vifaa vitakavyotakiwa kupelekwa eneo la uchimbaji kwa ajili ya shughuli hiyo mfano booster, compresor, mudpump, generator, welding plant, mobile workshop.

● Muda utakaotumika kupima uwezo wautoaji maji wa kisima husika.

● Kiasi na gharama za filtergravel, polymer bentonite, diesel, lubricants nk. vitakavyotumika katika uchimbaji.

Gharama zote zinaweza kuandaliwa baada ya kupata ripoti ya utafiti wa eneo husika.

Faida za kufanya utafiti kabla ya kuchimba kisima ni kama ifuatavyo:-

● Inapunguza gharamza zisizokuwa za lazima kwa eneo litakaloonekana halifai kuchimba.

● Inapunguza hasara zitokanazo na visima visivyokuwa na maji ambavyo vilichimbwa bila kupimwa.

● Mteja hufahamu gharama halisi kabla ya kuanza mradi.

● Hupunguza gharama zisizokuwa za msingi kwa kuchimba kisima kirefu sababu kina cha kisima huongeza gharama.

Mteja hupata kisima bora na kilichoondaliwa kitaalamu.

KARIBUNI SANA 0657710078
0769509666
DSC_0005.JPG
250513_155718_00016022.jpg
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom