Wachawi bado wananiandama

Wachawi bado wananiandama

sasa kama wamefikia kukuvua nguo huko kwingine wanakoelekea sio kuzuri kabisa, washindwe!
 
Mzizi mkavu, mwenzio kuvuliwa nguo siku tu, teyari umeshamwita bibie. Aisee!
 
Baada ya kufiwa na mwanangu mwenye umri wa siku mbili katika mazingira ya utata, takribani wiki 3 zilizopita,niliamua kukaa karibu na Mungu ili nisije kuanza kuwatwanga risasi watu wote ninao wahisi kuwa wachawi ktk eneo hili la Maswa, maombi ya nguvu nikishirikisha watumishi mbali mbali wa Mungu yalianza.

Wiki moja baadae asubuhi nikakuta nyayo kubwa kama ngumi ya mtu mzima za fisi ama simba zikiwa zimeizunguka nyumba yangu na katika dirisha la chumba changu nje palikuwa pamekwaruzwa kwa nyayo zile sambamba na alama za raba za mtu aliyekuwa kasimama dirishani.

Kabla ya kufiwa na mwanangu wakati mke wangu akiwa mjamzito nilikuta alfajiri saa 12 kinyesi cha binadamu mlangoni kwangu,Leo hii alfajiri saa 11 nimeshtuka na kujikuta nikiwa uchi kitandani wakati nililala na nguo,nilianza kusali na kuzizingira nguo hizo kwa damu ya Yesu,dk 5 baada ya kumaliza maombi paka akaanza kulia nje ya dirisha la chumba changu kwa sauti hafifu sana,nikamkea na kisha akatoweka ghafla.

Ole wenu wachawi nitawashinda ktk ulimwengu wa roho.

Gonga bia tu, hawtakusumbua tena.
 
Kazana na maombi mkuu!!!
Baada ya kufiwa na mwanangu mwenye umri wa siku mbili katika mazingira ya utata, takribani wiki 3 zilizopita,niliamua kukaa karibu na Mungu ili nisije kuanza kuwatwanga risasi watu wote ninao wahisi kuwa wachawi ktk eneo hili la Maswa, maombi ya nguvu nikishirikisha watumishi mbali mbali wa Mungu yalianza.

Wiki moja baadae asubuhi nikakuta nyayo kubwa kama ngumi ya mtu mzima za fisi ama simba zikiwa zimeizunguka nyumba yangu na katika dirisha la chumba changu nje palikuwa pamekwaruzwa kwa nyayo zile sambamba na alama za raba za mtu aliyekuwa kasimama dirishani.

Kabla ya kufiwa na mwanangu wakati mke wangu akiwa mjamzito nilikuta alfajiri saa 12 kinyesi cha binadamu mlangoni kwangu,Leo hii alfajiri saa 11 nimeshtuka na kujikuta nikiwa uchi kitandani wakati nililala na nguo,nilianza kusali na kuzizingira nguo hizo kwa damu ya Yesu,dk 5 baada ya kumaliza maombi paka akaanza kulia nje ya dirisha la chumba changu kwa sauti hafifu sana,nikamkea na kisha akatoweka ghafla.

Ole wenu wachawi nitawashinda ktk ulimwengu wa roho.
 
Pole ndg mleta mada kama umeamua kupambana kiRoho unatakiwa umaanishe cz Vita ya kiRoho ni ngumu sana.....Kwa sababu wanakujua watapambana lkn Tambua YESU hashindwi cha muhimu kujua Kanuni za kuomba manake MUNGU hasikilizi Maombi labda MTU unamwaga machozi unapoomba NO..kingine Tafuta mafundisho yanayohusu ASILI yakuzaliwa kwako....Pengine kwenye Familia yenu kuna MTU anakufanyia majanga Take care Lkn nakutahadhalisha VITA ya kiROHO kuna nyakati inakatisha Tamaa.....lkn wee Komaa utatoka
 
Vita ya kiroho ni ngumu sana na unatakiwa uwe moto kweli kweli yaani uwe umesimama kabisa na Mungu, kama unabip bip hao wachawi hutawaweza, bora ukatafute mitishamba kwa wataalamu, ila kama unaweza kusimama ujue kabisa utapitia changamoto nyingi na maranyingi Mungu anachelewa kujibu ili kukupima imani yako kwasababu watu wengi tukiwa na changamoto ndo tunakumbuka kuomba
 
Ukitaka uwe na nguvu za kuwashinda hao wachawi lazima pia ufunge na sio kuomba peke yake. Bwana Yesu alisema kuna matatizo ambayo hayatoki bila kufunga
 
kuna jamaa alimpata bingwa alimuosha mchawi kila kitu bila kujua sijui yupo wapi
 
Nimevutiwa kwa jinsi unavyoifahamu Zaburi vizuri! Wanaojiita wakristo hata hawajui matumizi yake!
Mimi ni Mtaalamu tofautisha na hao wanaojiita Wakristo wanaokwenda kila siku ya jumapili kusali na kuimba mimi ninaichambuwa kwa ndani zaidi hiyo Biblia usicheze na mimi MziziMkavu Hauchimbwi Dawa Mkuu sunshine1 mimi ni Moto wa kuotea mbali.
 
Last edited by a moderator:
Pole mkuu. Dr Manyau-nyau angekuja kuokoa jahazi, unfortunately mtaalamu huyo leo hii kapelekwa ngome kunyea debe!
 
Back
Top Bottom