Wabunge wote wapinge uteuzi wa Simbachawene

Wabunge wote wapinge uteuzi wa Simbachawene

Richard

Platinum Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
16,785
Reaction score
26,094
Kama ambavyo imekwishaelezwa na vyombo mbalimbali vya habari, rais Jakaya Kikwete alifanya mabadiliko kwenye bara za lake la mawaziri na moja ya mabadiliko hayo yanahusu wizara ngumu ya Madini na Nishati.

Rais amemteua mheshimwa George Simbachawene kuwa waziri kamili wa Wizara hiyo nyeti nchini Tanzania akiwa ni waziri wa nne kwenye serikali hii ya awamu ya nne.

Mheshimiwa Simbachawene kabla ya uteuzi huo alikuwa ni naibu waziri wa wizara hiyo kati ya mwaka 2012 na mwaka 2014 kabla ya kuhamishwa kwenda wizara ya ardhi nyumba na maendeleo ya makazi katikati ya mwaka 2014.

Ilipofunguliwa Akaunti ya Escrow na baadae kuamuliwa kwamba IPTL ifanyiwe utaratibu wa kufilisiwa ni George Simbachawene aliepewa jukumu la kusimamia kazi hiyo akiwa naibu waziri wa madini na Nishani na hata baadae kushirikiana na maofisa wa wizara ya Ardhi.

Isisahauliwe kwamba kuna baadhi ya viongozi wa wizara hizi mbili walokuwa chini ya Simbachwene wakishughulika na akaunti ya Escrow ambao leo hii wako mahakamani wakituhumiwa makosa yanayohusiana na hii akaunti ya Escrow.

Lakini tangu uteuzi huu ufanywe ni mashambulizi dhidi ya watu wengine ambayo ndio yanafanyika badala ya watanzania kukaa na kufikiri huu mchezo unaofanywa na serikali hii ya sasa.

George Simbachawene si mtu sahihi kuwekwa wizara nyeti ya Madini na Nishati kwani amekosa uadilifu.

Je Bunge letu linaona hali hiyo ni sawa pia?

Kama bunge linaona kuna kasoro katika uteuzi huu basi kuna budi kupiga kura ya kutokuwa na imani na uteuzi huu.

Sifahamu maoni ya wanachama wenzangu lakini mimi nimeona hio kasoro.
 
Simbachawene ana kosa gani? Waziri wake Tibaijuka ndiye mhalifu na fedha kala,kafukuzwa na Tra na mahakama wanamsubiri, hao watendaji wamechakachua nyaraka na wamekamatwa! Acha chuki binafsi.

Mkuu, unapotoa maoni kwenye masuala fulani fulani, unapaswa kutumia hoja katika kuwakilisha maoni yako, mimi nimeeleza kile nilichokiona katika uteuzi ulofanyika

Unafahamu hata mzee wetu Mkapa aliwahi kusema kwamba kuna watanzania ambao wanaendekeza uvivu wa kufikiri na hio sio lengo la mada yangu.

Ni maoni yangu huru kabisa kwamba iwaje wale ambao walikuwa wakiongoza wizara ya madini na nishati(Profesa Muhongo na Simbachawene) ionekane tu kwamba ni profesa Muhongo ndio tatizo na sio viongozi wote hawa wawili ambao wameshindwa kazi ya kuongoza wizara hiyo nyeti?

Jibu lilikuwa ni kutafuta waziri mwingine mpya kutoka eneo lingine ili aendeleze au kubadilisha sera za madini na nishati, likiwemo suala la kudhibiti malipo makubwa yanayofanywa kwa TANESCO kwa ajili ya usambazaji umeme.

Wewe kaa na usubiri utakuwa kuona mambo makubwa yanaibuka baadae kidogo.
 
Nchi yangu Tanzania !!!!!!!.

Watanzania sasa hivi wako kama watu waliochanganyikiwa .Mambo makubwa yanayotokea ,kuzusha mtafaruku na kutopatiwa majibu yameifanya jamii Ya watanzania kama watu waliochanganyikiwa. Serikali imeshindwa kuwakosha mioyo Yao pindi wanapokuwa na matarajio Fulani na yakatoka majibu completely opposite.

Wamebaki kushikia Bango mambo yasiyo na tija huku wakiacha mambo Ya msingi Kabisa. Nakubaliana na wewe Kabisa asilimia Mia Kuwa hatukutarajia huu uteuzi. Hii wizara unatakiwa kichwa kwani si Ya mchezo mchezo Ina mikataba mikubwa sana ambayo kuna aina ya wasomi wanaweza japo kujaribu kuimudu. Yes ni mwanasiasa lakini Kwenye sector nyeti kama hiyo Kwa CV ya simbachewene naona kama tunacheza na maisha.

Kwa mwakyembe ndo si comment Kabisa kwani sidhani kama hapo panahitaji IQ ya ziada kujua umuhimu wake. Yanayotokea ni Kama Mh Magufuli alivyowahi kuondolewa wizara yake.
 
Je,tunajua rais Kikwete ni kwa sababu zipi zilimfanya ampe uwaziri wa madini Simbachawene ?
1.Wanajuana
2.Mtetezie
3....
 
Muhongo alituhumiwa tu kwa kumkaribisha mwekezaji (Singh) ofisini kwake jambo ambalo siyo kosa. Kwa hilo kawajibika. Simbachawene hakuwa mtuhumiwa na Rais namsifu kwa kuona Simbachawene anahitajika kuendeleza kazi nzuri ya Muhonngo akamtoa Ardhi na kumrudisha Nishati na kumpandisha cheo! Kwa hoja hizi sijaona awajibike kwa lipi?
 
Simbachawene ndiye waziri wa nishati na madini atakayeboronga au kufeli kuliko mawaziri wote waliomtangulia wizara hii !
 
Muhongo alituhumiwa tu kwa kumkaribisha mwekezaji (Singh) ofisini kwake jambo ambalo siyo kosa. Kwa hilo kawajibika. Simbachawene hakuwa mtuhumiwa na Rais namsifu kwa kuona Simbachawene anahitajika kuendeleza kazi nzuri ya Muhonngo akamtoa Ardhi na kumrudisha Nishati na kumpandisha cheo! Kwa hoja hizi sijaona awajibike kwa lipi?

Inawezekana lakini ni moja ya vikosa vidogo,

Kosa kubwa la Muhongo ni kulidanganya bunge na watanzania kwamba pesa iliyowekwa kwenye akaunti ya Escrow haikuwa ya umma wakti sio kweli.

Ni kosa hilo tu na kamati ya Zitto ikamulika jambo hilo na baadae waheshimiwa John Mnyika na David Kafulila wakatishia kumwajibisha waziri mku kwa kushindwa kutekelza maazimio ya kamati ya PAC.
 
Kwa habari ya usafi wa Muhongo na wengine,tusubiri taarifa ya PCCB,iwe hadharani ndio mtu amtetee anayempa ndigwa aishi.
 
Wakuu ! Kama macho hayakuona vizuri ni kwamba mawaziri karibu wote walioapishwa na rais walikuwa watetezi wa ESCROW au ?
 
Simbachawene ndiye waziri wa nishati na madini atakayeboronga au kufeli kuliko mawaziri wote waliomtangulia wizara hii !

Yuko na mtaalamu Mhe Mwaijage kwa hiyo tuwape moyo vijana wanaweza kufanya vizuri zaidi baada kuona kilichowapata watangulizi wao.
 
Yuko na mtaalamu Mhe Mwaijage kwa hiyo tuwape moyo vijana wanaweza kufanya vizuri zaidi baada kuona kilichowapata watangulizi wao.

Ndio hii mambo unaambiwa "who the cap fit. . . . . . . . ." mtaalamu afanye na wataalamu wenzie sio kuweka kundi la ndio na sio pamoja!!!
 
Simbachawene ana kosa gani? Waziri wake Tibaijuka ndiye mhalifu na fedha kala,kafukuzwa na Tra na mahakama wanamsubiri, hao watendaji wamechakachua nyaraka na wamekamatwa! Acha chuki binafsi.

Wewe ndie mtoto wa simbachawene nini? Mbona mapovu yakumwaika?
 
Yuko na mtaalamu Mhe Mwaijage kwa hiyo tuwape moyo vijana wanaweza kufanya vizuri zaidi baada kuona kilichowapata watangulizi wao.

Mwijage ana utaalamu gani wakati yeye na Asumta Mshama ndio walikuwa watetezi wa hiyo kashfa?
 
Acheni kuwa wapinzani wa kila kitu, rais ana washauri waliobobea, so tuwape nafac, achen kufikiria kama mtu aliyeko toilet, think big
 
Back
Top Bottom