Niliwahi kusema huko nyuma kwamba Huyu Jennister Mhagama angefaa kabisa kuwa Spika wa bunge.
Anaweza asiwe na elimu ya juu sana kwa maana ya VYETI lakini utendaji wake ni viwango vya juu kushinda hao wana-ccm wanaojiita wasomi. Kikao kilichopitaa aliongoza session na kwa kweli bunge lilionekana kuwa na hadhi. hata pale alipoona mbunge anakwenda kinyume na kanuni basi alimweleza mtoa hoja kwa style ya ustaarab na heshma.
Sasa tunamwona anavyopambana na madudu wizara ya kazi. Watanzania wanaofanya kazi kwenye viwanda vya wenzetu wenye asili ya India hapa tanzania wanaangamia. Kuna udhalilishaji wa hali ya kutisha. hawana utu kabisa hawa waajiri. Na cha kushangaza zaidi ni kuwa kwenye management ni Wahindi toka India. Sijui Wizara ya Mambo ya ndani na Wizara ya Kazi wametoa vibali vya watu toka India kwa sababu zipi? Hata kwenye maduka, car show rooms ni India, Pakistan.
Mawaziri vivuli LEMA na Regia Mtema angalieni hili kuna scandal za kutisha.