Wabunge wa UKAWA kuweni makini katika kujadili mahakama ya kadhi

Kalesya

JF-Expert Member
Dec 21, 2014
691
728
Kwa vyovyote vile ni ukweli ulio wazi kabisa kuwa ccm sasa wanatapatapa na ahadi yao ya kuwaletea waislamu mahakama ya Kadhi huku Tanganyika! Ili kuwatumia waislamu na kupata kura zao kwa wingi katika uchaguzi uliopita ccm walitoa ahadi hii huku wakijua hawakujiandaa kuitekeleza na hata hawakujua uendeshwaji wa mahakama hizo utakuwaje na kwa gharama za nani.

Hata katika katiba ya Chenge iliyopitishwa na ccm katika Bunge Maalumu la Katiba ya ccm chini ya Sitta bado ccm ilishindwa kutekekeza ahadi yao hiyo na hivyo kushindwa kuiweka mahakama ya Kadhi ktk Katiba hiyo. Kitendo hicho kiliamsha hasira na madai mapya ya Mahakama hiyo kwa waislamu! Hapo ndipo Waziri mkuu Pinda alipolazimika kuingilia kati mwishoni na kuwaahidi waislamu(waliokuwa BMK na walio nje) kuwa serikali ya ccm ingepeleka muswada bungeni wa mabadiliko ya sheria ili mahakama ya Kadhi iweze kutambulika kama muswada utapita ( na kwa jinsi maccm walivyo wengi bungeni basi wanao uwezo wa kuupitisha hata bila UKAWA kuupitisha).

Sasa angalizo lipo hapa:

1. Wabunge wa UKAWA kuweni makini wakati wa mjadala huo kwasababu ccm watataka nyie ndiyo mchangie sana ili muonekane kama nyie ndiyo mliokwamisha endapo mtaukataa ili kuichonganisha UKAWA na waislamu. Hili linategemewa sana baada ya zile propaganda za ccm kuwa CHADEMA ni chama cha wakristo kufeli, hasa wakati huu ambapo UKAWA umeundwa ikijumuisha watu wa dini zote.

2. Ccm wanajua tayari kuwa muswada huo wataupitisha au hawataupitisha kwa wingi wao, lakini wanachokitafuta hapo ni kuwaingiza katika mtego wabunge wa UKAWA. Hivyo basi ikiwezekana UKAWA wote wawe wa mwisho kabisa kusema neno kwenye huo muswada, ili kama ccm wataupitisha wapitishe na kama wataukwamisha waukwamishe wenyewe. UKAWA mje kumalizia tu mwisho kwa uamuzi ambao mtaona ni sahihi kulingana na ccm watakavyoamua. Hapo mtakuwa mmekwepa kuingizwa chaka na mafisadi.

3.Msiwape sababu ccm eti kwamba serikali yao sikivu (kama wanavyoiita wenyewe) kuwa ilipeleka muswada bungeni lakini UKAWA wakaupinga! Msikubali huo ujinga.

4. Muswada huo wa mahakama ya Kadhi kwa jinsi ulivyo ni bomu, ni feki na hautekelezeki kisheria!

Ni usanii mtupu kwasababu;
(a) Hauna tamko la kisheria la uanzishwaji wa mahakama hizo(Establishing Provision) kinachounda rasmi mahakama hiyo. Badala yake kuna tamko tu la kuitambua mahakama hiyo( huwezi kutambua kitu ambacho hakipo kisheria, hakijaanzishwa rasmi). Maamuzi yeyote ya mahakama hizi yaweza kuwa VOID kama hazitambuliki na sheria mama.
(b) Mahakama hizo hazijapewa muundo au ngazi za maamuzi eg ngazi ya awali ya shauri fulani, ngazi inayofuatia na ngazi ya mwisho.
(C) Mamlaka zake hazijaainishwa(jurisdiction) yake kijiografia wala kithamani. Kwamba ngazi hii inaanzia eneo lipi hadi wapi na kwa kesi za thamani ipi labda.
(d) Sifa za kuwa Kadhi hazijatajwa, hivyo unaweza kuwa na mahakama hii na bado ukawa na Kadhi asiye na vigezo kwa mujibu wa vigezo vya waislamu.
(e) Hakuna usalama wa ajira za Kadhi etc

HIVYO NASEMA UKAWA KAENI KIMYA KABISA KWENYE HUO MUSWADA, WAACHIENI CCM WAJIAMULIE AHADI YAO.. MAHAKAMA IJE AU ISIJE ITAJULIKANA MBELE YA SAFARI. MSIKUBALI KUTEGWA.
 
Hili suala halina cha kuridhisha kundi fulani sio rahisi hivyo. Ndio maana walio jaliwa hekima na mwenyezi Mungu huko nyuma waliliona hili na wakasema, "nchi hii haina dini period"

Mtahangaika sana lakini mwisho wa siku mtarudi kwenye ukweli huo hapo juu. Atakae pingana na ukweli huu basi ajue ana itafutia balaa nchi hii na wananchi wake na yeye akiwa mmoja wao.
 
Kwa hao akina mnyaa na waislamu ni ruksa kuitetea mahakama iletwe, mtego huu upo sana kwa wabunge wakristo na hasa wa Chadema. Ccm wanaiona point fulani kuwa wakristo na waislamu wanaweza kujikuta wanapingana kama wasipokuwa makini! Hivyo kuusambaratisha UKAWA ili Cuf na Chadema zitengane. Hivyo angalizo hili linawahusu sana Ukawa wakristo kutojiingiza kwenye kuipinga mahakama hii. WATEGAJI CCM TAYARI JIBU WANALO KAMA ITAPITA AU HAIPITI ILA WANATAKA KUGOMBANISHA WATU TU HAPO!
 
Kama ukawa watakuwa na hofu na uislam basi ni sababu tosha ya kuisambaratisha ukawa,wacha move iendeleee...
Hakuna UKAWA mwenye hofu na uislamu, pale kuna waislamu na wakristo. Hapa POINT ya msingi ni kuwa kuna mtego ccm wamewawekea UKAWA ili wakwaruzane katika huo muswada!
 
Viongozi wa UKAWA wanalijua hilo, hivyo kwa busara na hekima zao hiyo mikwaruzano ambayo Mainterahamwe wanataka itokee haitakuwepo.

Hakuna UKAWA mwenye hofu na uislamu, pale kuna waislamu na wakristo. Hapa POINT ya msingi ni kuwa kuna mtego ccm wamewawekea UKAWA ili wakwaruzane katika huo muswada!
 
Viongozi wa UKAWA wanalijua hilo, hivyo kwa busara na hekima zao hiyo mikwaruzano ambayo Mainterahamwe wanataka itokee haitakuwepo.
Tena UKAWA wangekuwa wajanja hawa, wange-take the chance/risk! Wange-take the chance/risk coz' sioni ni namna gani muswada huu unaweza kupita.... mbaya zaidi, CCM wakisema upite, utapita tu hata kama UKAWA wataukataa! Sasa busara kwa UKAWA hapa ni kuukubali coz' kuna uwezekano mkubwa CCM wakaukataa na hivyo CCM watakuwa wamejichongea wenyewe... lakini UKAWA wakiukataa na CCM wakaukubali, UKAWA, hususani Zanzibar watakuwa wamejichongea wakati inafahamika wazi kwamba hata wakiukataa CCM pekee yao wana uwezo wa kuupitisha wakiamua!

Hilo la mtego lipo wazi na haliepukiki na ndio maana busara hapa ni UKAWA (soma CHADEMA) ni kuukubali kwavile sioni ni namna gani CUF wanaweza kuukataa muswada huu! CHADEMA wanatakiwa kuukubali kwa hoja kwamba hawana cha kupoteza! Kama kweli kuna watu wanaoamini CHADEMA ni chama kwa ajili ya Wakristo, katu watu hao hawawezi kurudi CCM kwavile tu CHADEMA walikubali na CCM waliukataa. Binafsi siamini kama CHADEMA ni chama cha Kikristo ingawaje nakubali kwamba kuna mashabiki wa CHADEMA wana chuki mbaya dhidi ya imani nyingine.... na hawa ndio wanaoipaka sura mbaya CHADEMA hususani hapa JF.

Nikiongea kutoka moyoni kabisa, ni heri yako BAKI uliejitenga na upuuzi huu kwa sababu haileti picha mzuri kwa mtu anayesimama kidede kila siku kutetea chama fulani halafu mtu huyo huyo anaonekana kuwa na msimamo wa chuki za kijinga kabisa kwa imani zingine.
 
Last edited by a moderator:
Nimekusamehe kwa kuandika kitu usichokijua. Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza na kwa taarifa yako mimi sichukii mtu wa imani yoyote ile hata wale wasio na dini pia mapagani pia siwachukii, lakini pale ninapoona unafiki wa namna yoyote ile basi siogopi kuunyoshea kidole na kuukemea.

Tena UKAWA wangekuwa wajanja hawa, wange-take the chance/risk! Wange-take the chance/risk coz' sioni ni namna gani muswada huu unaweza kupita.... mbaya zaidi, CCM wakisema upite, utapita tu hata kama UKAWA wataukataa! Sasa busara kwa UKAWA hapa ni kuukubali coz' kuna uwezekano mkubwa CCM wakaukataa na hivyo CCM watakuwa wamejichongea wenyewe... lakini UKAWA wakiukataa na CCM wakaukubali, UKAWA, hususani Zanzibar watakuwa wamejichongea wakati inafahamika wazi kwamba hata wakiukataa CCM pekee yao wana uwezo wa kuupitisha wakiamua!

Hilo la mtego lipo wazi na haliepukiki na ndio maana busara hapa ni UKAWA (soma CHADEMA) ni kuukubali kwavile sioni ni namna gani CUF wanaweza kuukataa muswada huu! CHADEMA wanatakiwa kuukubali kwa hoja kwamba hawana cha kupoteza! Kama kweli kuna watu wanaoamini CHADEMA ni chama kwa ajili ya Wakristo, katu watu hao hawawezi kurudi CCM kwavile tu CHADEMA walikubali na CCM waliukataa. Binafsi siamini kama CHADEMA ni chama cha Kikristo ingawaje nakubali kwamba kuna mashabiki wa CHADEMA wana chuki mbaya dhidi ya imani nyingine.... na hawa ndio wanaoipaka sura mbaya CHADEMA hususani hapa JF.

Nikiongea kutoka moyoni kabisa, ni heri yako BAKI uliejitenga na upuuzi huu kwa sababu haileti picha mzuri kwa mtu anayesimama kidede kila siku kutetea chama fulani halafu mtu huyo huyo anaonekana kuwa na msimamo wa chuki za kijinga kabisa kwa imani zingine.
 
Nimekusamehe kwa kuandika kitu usichokijua. Jambo usilolijua ni kama usiku wa giza na kwa taarifa yako mimi sichukii mtu wa imani yoyote ile hata wale wasio na dini pia mapagani pia siwachukii, lakini pale ninapoona unafiki wa namna yoyote ile basi siogopi kuunyoshea kidole na kuukemea.
BAK, umenielewa nilichokisema au umeandika tu? Sasa umenisamehe ni nini nisichokijua wakati nimesema ni heri yako uliejitenga na upuuzi huu (wa udini)?
 
sisi kina gogo la shamba tumeisha wataadharisha ukawa kwa suala hili la Mahakama ya Kadhi wasichangii lolote kuanzia waislamu mpaka wakristo kwa sababu suala hili halina tatizo,mahaka ikiwepo au isiwepo,tatizo linakuja kwa kuwa viongozi wa ccm hawana busara ya utawala kwa sasa busara yao imebaki ya kubuni namna ya kujitajirisha tu, lakini tukipata viongozi wenye busara hili sio tatizo. ni wiki nzima sasa nasema maneno haya na nimeomba nijibiwe na Mh. Lema au Lisu lakini mpaka sasa sijasikia maoni yao,tafadhalini sana wabunge wa chadema msipuuze maoni yetu kama alivyopuuza Kikwete tulipomshahuri kwenye sakata la Escrow.bado naomba kupata mawazo ya Lema au Lisu
 
Nafikiri haya maneno yako pia yalinilenga mimi ndiyo maana nikajibu hivyo, labda kweli sikukuelewa, naomba ufafanuzi wako.

anayesimama kidede kila siku kutetea chama fulani halafu mtu huyo huyo anaonekana kuwa na msimamo wa chuki za kijinga kabisa kwa imani zingine.

BAK, umenielewa nilichokisema au umeandika tu? Sasa umenisamehe ni nini nisichokijua wakati nimesema ni heri yako uliejitenga na upuuzi huu (wa udini)?
 
Nafikiri haya maneno yako pia yalinilenga mimi ndiyo maana nikajibu hivyo, labda kweli sikukuelewa, naomba ufafanuzi wako.

anayesimama kidede kila siku kutetea chama fulani halafu mtu huyo huyo anaonekana kuwa na msimamo wa chuki za kijinga kabisa kwa imani zingine.
Sentensi yangu imeanza: ".... ni heri yako BAKI uliejitenga na upuuzi huu kwa sababu haileti picha mzuri kwa mtu anayesimama kidede kila siku kutetea chama fulani halafu mtu huyo huyo anaonekana kuwa na msimamo wa chuki za kijinga kabisa kwa imani zingine." Kwamba, kuna watu kila siku na kila wakati wanaonekana kuitetea CHADEMA kwa nguvu zote but at the same time wanakuwa na mihemuko ya kijinga kidini... na huo ndio msingi wa hapo kwenye BLUE kwamba haileti picha mzuri kwa mtu ambae kila wakati anatetea chama fulani lakini anakuwa ana mihemuko ya kidini in contrast na hapo kwenye RED, kwamba ikiwa mtu hawezi kujitenga na upuuzi wa chuki za kidini basi haipendezi kutetea chama kwa nguvu zote... sentensi yangu imeanza kwa kumtaja BAK kama ni aliyejitenga na upuuzi huu!
 
Last edited by a moderator:
sisi kina gogo la shamba tumeisha wataadharisha ukawa kwa suala hili la Mahakama ya Kadhi wasichangii lolote kuanzia waislamu mpaka wakristo kwa sababu suala hili halina tatizo,mahaka ikiwepo au isiwepo,tatizo linakuja kwa kuwa viongozi wa ccm hawana busara ya utawala kwa sasa busara yao imebaki ya kubuni namna ya kujitajirisha tu, lakini tukipata viongozi wenye busara hili sio tatizo. ni wiki nzima sasa nasema maneno haya na nimeomba nijibiwe na Mh. Lema au Lisu lakini mpaka sasa sijasikia maoni yao,tafadhalini sana wabunge wa chadema msipuuze maoni yetu kama alivyopuuza Kikwete tulipomshahuri kwenye sakata la Escrow.bado naomba kupata mawazo ya Lema au Lisu
Hili la kutochangia chochote inaweza kuwa ni busara kubwa zaidi lakini CUF walivyo na mihemuko, I doubt kama wanaweza kuvumilia hasa ukizingatia kwamba suala lenyewe linaingia kwenye katiba JMT. Kuna wengine, dini kwanza, siasa/nchi baadae!
 
Shukrani Mkuu NasDaz kwa ufafanuzi wako, nchi yetu haihitaji hili la kupandikiza mbegu za kupitia udini. Tunayaona yanayotokea Nigeria ya kuuana wenyewe kwa wenyewe kupitia udini, hili likitokea kwetu basi umwagaji damu wake utakuwa ni mkubwa sana na wa kutisha. Tulipige vita hili la udini kwa nguvu zetu zote.
 
Last edited by a moderator:
hapa kazi ipo mana nmeshawackia watu kadhaa ambao ni wakristo wakisema iwapo chadema wataunga mkono hoja ya kukubali mahakama ya kadhi bac wanahama chadema
 
Shukrani Mkuu NasDaz kwa ufafanuzi wako, nchi yetu haihitaji hili la kupandikiza mbegu za kupitia udini. Tunayaona yanayotokea Nigeria ya kuuana wenyewe kwa wenyewe kupitia udini, hili likitokea kwetu basi umwagaji damu wake utakuwa ni mkubwa sana na wa kutisha. Tulipige vita hili la udini kwa nguvu zetu zote.
Na suala la udini halijapata kumsaidia yeyote zaidi ya kupandikiza chuki zisizo na msingi! Wengine sisi huwa hatuogopi kusema... nimeshawahi kuwaambia wale tunao-share imani kwamba ni upumbavu uliopita mipaka ya upumbavu kudhani dunia ya leo unaweza kumsilimisha mtu kwa kutumia nguvu na nikasema wazi kwamba labda leo hii Uislamu ungekuwa na wafuasi wengi zaidi kuliko ilionao sasa (tena kutoka kwa watu wa imani nyingine) endapo kusingekuwa na matumizi ya nguvu kwa kuwa watu wanajiunga kwenye dini fulani kutafuta peace of soul, and nothing else sasa ni mpumbavu tu ambae baada ya kuvurugwa huko alikotoka anaamua kwenda msikitini akasilimu/kuomba msaada wa kiroho halafu anakuta vipaza sauti vinahubiri shari halafu bado akawa na hamu ile ile ya kutaka kuingia na kuomba msaada wa kiroho! Hapa tulikuwa tunajadili suala la matumizi ya nguvu lakini tusiliendeleze hapa lisije likachafua mjadala.
 
Kwa kuwa ccm wana uwezo wa kupitisha au kutopitisha,na wanajua nia yao ovu!,basi mi naishauri ukawa wakubali maamuzi yao then km utapitishwa na raia hatujaridhika tutaenda mahakamani kama kenya kuupinga!, ukawa wasiingie majaribuni kwa mtego mchache ivi,
Logic
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom