Wabunge wa CHADEMA wanakatisha tamaa

Wabunge wa CHADEMA wanakatisha tamaa

Joined
Dec 11, 2010
Posts
3,321
Reaction score
6,331
Naangalia bunge muda huu naona wabunge wengi wa chadema hawamo bungeni hii pia imejitokeza juma lililopita wabunge wengi hawakuwemo. Binafsi nakata sana tamaa na hili.

Wanakutana muda huu saa saba na robo mara baada ya kuahirisha shughuli za bunge. Tusiangalie kuwa eti mbona ccm wengi pia hawamo naongelea chadema, juma lililopita pia wengi hawakuwemo bungeni na viti vilikuwa wazi. Wao ndio tegemeo la wengi utoro wao unakera.

Tusiwe wepesi kutetea uozo kwenye chama chetu tutakuwa hatukisaidii chama wala wabunge wake. Wakienda hovyo tupaze sauti tuwaambie tusijenge mazingira ya kuwa na chama au wabunge wasio kosolewa au kusemwa.

Mwenyekiti Jenister Mhagama ametangaza kuwa kamati inakutana saa saba na robo mchana na si kweli kuwa kamati inayoenda kukutana ina wabunge wote wa chadema. Msitetee tu mapungufu jamani hamuwasaidii hao mnao tetea.
 
Unajua idadi ya wabunge wanaopaswa kuwepo Bungeni au umeona chadema tu? Unakumbuka kuwa saa saba lilitolewa Tangazo kuwa wanakikao? angalia idadi ya wabunge wa ccm na chadema waliopo kwa asilimia ni akina nani watoro?
Njoo na hoja yenye mashiko si kukurupuka
 
wabunge wengi tu watoro, co cdm wala ccm, wote ni walewale
 
Mkuu Mohamedi Mtoi usijali sana watakuwa wameshasaini posho.

Naangalia bunge muda huu naona wabunge wengi wa chadema hawamo bungeni hii pia imejitokeza juma lililopita wabunge wengi hawakuwemo. Binafsi nakata sana tamaa na hili.
 
Last edited by a moderator:
Kuna Chadema damu na chadema asilia hapa, kule kuna Chadema Slaa na Chadema Zitto mmmh haya
 
Kama wanaangalia kusaini posho na kuondoka nachelea kusema kuwa wanaiga tabia za magamba ambazo zinachukiza wengi.
 
Usikate tamaa wapo kutimiza majukumu mengine ya kukijenga chama,
Naangalia bunge muda huu naona wabunge wengi wa chadema hawamo bungeni hii pia imejitokeza juma lililopita wabunge wengi hawakuwemo. Binafsi nakata sana tamaa na hili.
 
Kosa halihalalishi kosa, kutukuwepo wabunge wa ccm sio tiketi ya wa cdm kutokuwepo. Wewe ndio pumba kweli.
 
Hakuna mtu aliyezaliwa kuishi maisha ya mwingine. Fight for your daily bread na usitegemee lolote toka kwa mwana siasa...kila mtu yuko kwa maslahi yake pale. Huyo JOHN Mnyika kila siku ni miongozo na taarifa lakini ubungo yote haina maji.
 
wafanye nn? serikali inapinga kila linalochangiwa na upizani,
 
We unafkiri wamegombea kukusaidia! kudadek, ww cheza pool ukitegemea cdm itakutoa. Hiyo inaitwa yarabbi nafsi. Wao kwanza madebe baadae
 
Mtu atakayetaja tabia hata moja ya wabunge wa CCM ambayo haiigwi na wabunge wa CHADEMA nitampa zawadi.
Le Mutuz alituambia mpaka rushwa kwa wagombea wanachukua!
 
Naona una lalamika tuu

Tatizo kubwa la sisi watanzania ni kujengewa msingi ya unafiki na bado kuendeleza unafiki huohuo kwa kuifuata misingi hiyohiyo. Kwa nini utetee uwongo ili uonekane hulalamiki?!

Acha unafiki, tuache unafiki kuipenda chadema hakumaanishi kuto kukosoa wabunge au mwanachama mmoja mmoja ndani ya chadema. Kukosolewa ni moja ya nguzo kuu ya kujijenga.
 
Wakihuduria vikao vyote huwa wanakuletea hela ya kula

Wewe kweli ni GT? Kwani tumewachagua watupe hela ya kula au kutuwakilisha kwa kutimiza majukumu yao mojawapo likiwa kuhudhuria vikao vya bunge bila utoro? Think or sink...
 
subiri miswada ya tume ya katiba, masuala ya tume ya uchaguzi au mengine yenye maslah nao binafsi.
 
Back
Top Bottom