Wabunge wa CHADEMA wanakatisha tamaa

Wabunge wa CHADEMA wanakatisha tamaa

Unajua idadi ya wabunge wanaopaswa kuwepo Bungeni au umeona chadema tu? Unakumbuka kuwa saa saba lilitolewa Tangazo kuwa wanakikao? angalia idadi ya wabunge wa ccm na CHADEMAwaliopo kwa asilimia ni akina nani watoro? Njoo na hoja yenye mashiko si kukurupuka

Wachangiaji wa namna hii ndo wanawapofusha Wabunge na viongozi wa CDM. Mwenzetu Mohamedi Mtoi anawachukulia CDM kama muhimili (reference pillar) wa mabadiliko na dola tarajiwa inayotegemewa ilete mageuzi ya kimfumo na kimuundo. Hivyo haitegemewi CDM wafanye kama CCM.

Na kwa muktadha huo ndo maana Mohamedi Mtoi anawashangaa na kuwakanya wajirekebishe. Lakini memba ambao wameifanya CDM na viongozi wa CDM kuwa Malaika hawataki daima chama na viongozi wao wakemewe wala kuguswa kwa makosa wanayofanya. Huku ni kupelekea akili na utashi wetu likizo.

Tunaanza kuzidiwa na wanyama wanaopambanua walau kidogo
 
Mimi nadhani headinp ya topic yako ingekuwa ni kuuliza wabunge wa CDM wako wapi kwa muda ule badala ya kulalamika. Walikuwa kwenye kikao
 
Mimi nadhani heading ya topic yako ingekuwa ni kuuliza wabunge wa CDM wako wapi kwa muda ule badala ya kulalamika. Walikuwa kwenye kikao
 
wabunge wengi tu watoro, co cdm wala ccm, wote ni walewale

Kwa hiyo mwanao akivuta bangi utamuacha tu endelee kuvuta kwa kuwa watoto wengi wa mtaani kwako nao wanavuta bangi? Umechemka hapa mkuu maana kosa halihalalishi kosa.
 
Tatizo kubwa la sisi watanzania ni kujengewa msingi ya unafiki na bado kuendeleza unafiki huohuo kwa kuifuata misingi hiyohiyo. Kwa nini utetee uwongo ili uonekane hulalamiki?!

Acha unafiki, tuache unafiki kuipenda chadema hakumaanishi kuto kukosoa wabunge au mwanachama mmoja mmoja ndani ya chadema. Kukosolewa ni moja ya nguzo kuu ya kujijenga.


don panic, wako kwenye vikao
 
Mtu atakayetaja tabia hata moja ya wabunge wa CCM ambayo haiigwi na wabunge wa CHADEMA nitampa zawadi.
Le Mutuz alituambia mpaka rushwa kwa wagombea wanachukua!

Sio mafisadi. Katika kashfa zote za ufisadi zilizoibuliwa, hawamo.
Mfano wa kashfa hizo za ufisadi ni:- EPA, Richmond, Kagoda, Dowans, Deep Green, TanGold, Kuuza NBC, mikataba mibovu ya madini, etc.
 
Kuna Chadema damu na chadema asilia hapa, kule kuna Chadema Slaa na Chadema Zitto mmmh haya
Acha uzushi wewe, sera za makundi ni za Magamba, kwetu M4C ni kazi tu ya kuikomboa tz kutoka kwenye makucha ya mafisadi "ccm" ZITO, SLAA wote ni majembe ya kung'olea visiki,.
 
Wewe kweli ni GT? Kwani tumewachagua watupe hela ya kula au kutuwakilisha kwa kutimiza majukumu yao mojawapo likiwa kuhudhuria vikao vya bunge bila utoro? Think or sink...

kuhudhuria vikao vyote ndio nini? Mawazo yao mengi yenye maslah kwa mwananch yanapuuzwa. Kuna haja gani ya kupoteza muda kwenye vikao ambavyo viongozi wa Bunge wanaviongoza kimagamba?
 
Kama hawako kwenye orodha ya kuchangia waendelee kusinzia badala ya kwenda kutafiti kwa ajili ya hoja zijazo? Wabunge wanaisimamie serikali hivyo hawako pale kusikiliza michango ya wabunge wenzao ili kuikosoa; wao kazi yao ni kuikosoa serikali
 
Mtu atakayetaja tabia hata moja ya wabunge wa CCM ambayo haiigwi na wabunge wa CHADEMA nitampa zawadi.
Le Mutuz alituambia mpaka rushwa kwa wagombea wanachukua!

Hapo nina mashaka sana. Hivi serikali ya CCM ingewaachia tu jamaa wa Chadema wachukue rushwa huku inajua ??? Labda sio serikali hii tunayoifahamu sisi.
Serikali hii, jambo dogo sana likifanywa na Chadema litakuzwa saaana. Mpaka hoja za msingi zinapingwa kwa sababu tu zimetolewa na Chadema.
Hapo umechemka. Au labda huyo uliyemnukuu naye kachemka. Rushwa ni kosa kubwa sana, lisingeweza kuachiwa hivi hivi.
 
Naangalia bunge muda huu naona wabunge wengi wa chadema hawamo bungeni hii pia imejitokeza juma lililopita wabunge wengi hawakuwemo. Binafsi nakata sana tamaa na hili.

Wanakutana muda huu saa saba na robo mara baada ya kuahirisha shughuli za bunge. Tusiangalie kuwa eti mbona ccm wengi pia hawamo naongelea chadema, juma lililopita pia wengi hawakuwemo bungeni na viti vilikuwa wazi. Wao ndio tegemeo la wengi utoro wao unakera.

Tusiwe wepesi kutetea uozo kwenye chama chetu tutakuwa hatukisaidii chama wala wabunge wake. Wakienda hovyo tupaze sauti tuwaambie tusijenge mazingira ya kuwa na chama au wabunge wasio kosolewa au kusemwa.

Mwenyekiti Jenister Mhagama ametangaza kuwa kamati inakutana saa saba na robo mchana na si kweli kuwa kamati inayoenda kukutana ina wabunge wote wa chadema. Msitetee tu mapungufu jamani hamuwasaidii hao mnao tetea.

Wabunge wanafanya kazi ya chama kwanza nyie wananchi subirini kwanza.
 
Tatizo kubwa la sisi watanzania ni kujengewa msingi ya unafiki na bado kuendeleza unafiki huohuo kwa kuifuata misingi hiyohiyo. Kwa nini utetee uwongo ili uonekane hulalamiki?!

Acha unafiki, tuache unafiki kuipenda chadema hakumaanishi kuto kukosoa wabunge au mwanachama mmoja mmoja ndani ya chadema. Kukosolewa ni moja ya nguzo kuu ya kujijenga.


Nakubaliana na wewe Mohamedi, mahudhurio kwenye bunge letu bado ni tatizo, na hili ni kwa vyama vyote japo CCM wamekoleza. Ila vyema CHADEMA waoneshe kujali concerns za wananchi.

Hatat hivyo tuna tatizo kubwa zaidi na la kimsingi na hili linaangukia moja kwa moja kwenye meza ya Spika. Bunge letu bado linafanya kazi kwa msimu. Shughuli za kamati za bunge na hata swala zima la bunge kuisimamia serikali kwa niaba ya wananchi zinafanywa wakati wa vikao vya bunge! Mara bunge lilipoanza kamati za bunge nazo zikaanza kubadilisha ndege na hata wakati huu tunapoandika hapa wapo wabunge nje ya nchi wakifanya kazi za kamati.

Ni bahati mbaya sana kwamba mpaka sasa hivi hatujawa na Spika mbunifu wa kuweza kuongoza bunge mwaka mzima na kuweka utaratibu unaofaa kwa kamati za bunge kufanya kazi zake bila kuathiri mahudhurio ya bunge.
 
Usijal tuliza mzuka cdm wako 40 wakipungua tu ndio tunalalama ukiona kimya ujue watunga sheria
 
No research,no right to Speak.Wabunge hawa walitangaziwa kuwa kutakuwa na kikao chao kitaanza saa saba na robo mchana na hili alitangaza Spika Makinda saa nne asubuhi.
 
Kuna Wabunge wengi CDM ni mzigo kama wa CCM! Hawapo active kabisa! kila mbunge wa CDM angewajibika mambo mengi yangenyooka!
 
Kama hawako kwenye orodha ya kuchangia waendelee kusinzia badala ya kwenda kutafiti kwa ajili ya hoja zijazo? Wabunge wanaisimamie serikali hivyo hawako pale kusikiliza michango ya wabunge wenzao ili kuikosoa; wao kazi yao ni kuikosoa serikali

Kuweni makini wakuu! Utoro na kutokuwa makini ndio umechangia kupitisha sheria ya mifuko ya pensheni ambayo leo ndio bunge limegundua kuwa walichemka baada ya kelele za wananchi makini.

Jiulize, wabunge wa chadema ambao ni mahiri kwa kuibua hoja nzito na kusimamia maslahi ya wanyonge walikuwa wapi? Au ndio utetezi wenye makengeza kuwa walikuwa nje wanatafiti na kazi yao ni kuisimamia serikali?

Sheria ya mifuko ya pensheni ya mashirika ya umma inamgusa kila mlalahoi aliye ajiriwa kwa hiyo wabunge kutokuwemo ndani ya bunge na kuwa makini na mijadala athari yake ni kama hii ya kurudisha upya mjadala nakupoteza muda ambao ungetumika kujadili mambo mengine ya msingi yanayo tukabili.
 
Naangalia bunge muda huu naona wabunge wengi wa chadema hawamo bungeni hii pia imejitokeza juma lililopita wabunge wengi hawakuwemo. Binafsi nakata sana tamaa na hili.

Wanakutana muda huu saa saba na robo mara baada ya kuahirisha shughuli za bunge. Tusiangalie kuwa eti mbona ccm wengi pia hawamo naongelea chadema, juma lililopita pia wengi hawakuwemo bungeni na viti vilikuwa wazi. Wao ndio tegemeo la wengi utoro wao unakera.

Tusiwe wepesi kutetea uozo kwenye chama chetu tutakuwa hatukisaidii chama wala wabunge wake. Wakienda hovyo tupaze sauti tuwaambie tusijenge mazingira ya kuwa na chama au wabunge wasio kosolewa au kusemwa.

Mwenyekiti Jenister Mhagama ametangaza kuwa kamati inakutana saa saba na robo mchana na si kweli kuwa kamati inayoenda kukutana ina wabunge wote wa chadema. Msitetee tu mapungufu jamani hamuwasaidii hao mnao tetea.

Hiyo ni sahihi kabisa mkuu Tukitaka mazuri ni lazima hawa wabunge wetu waache Utoro vinginevyo mwisho wa siku tunasingizia hoja zinapita kwa uchache wa wabungu kumbe n Utoro mtupu.
 
Usikate tamaa wapo kutimiza majukumu mengine ya kukijenga chama,

Bora hata wasiwepo maana uwepo wao hauna tija kwani budget ingepitishwa tuu kwani wanafiki Ndio wengi kuliko wasio wanafiki, spika anakaba mpaka kivuli chake mwenyewe wewe unadhani uwepo wao unatija?

Ningewashauri walisusie ilo Bunge la vioja na kurudi majimboni mwao waimarishe chama ngazi za chini Kama mabalozi na wenyeviti pia ata watatue kero ndogondogo za wapiga kura wao ambazo hazihitaji mchango wa serikali kuu.

Nawasilisha ni mtazamo wangu sio mtu mngine wala wa chama cha siasa
 
Kama wanaangalia kusaini posho na kuondoka nachelea kusema kuwa wanaiga tabia za magamba ambazo zinachukiza wengi.
Kama kila kitu kinapigwa nyundo hamna haja ya kuwepo bungeni! Mkuu unafikiri siku hizi kuna bunge? hicho ni kijiwe cha ccm
 
Back
Top Bottom