Nadhani Hii ni katika kujaribu kuleta Usawa katika Ugawaji wa muda katika kuongea----Tunakubaliana kwamba Wabunge wanapoongea,ndio tunaona jinsi wanavyotutetea ama wasivyoweza kutututetea.
Huwa mnaona kwamba michango mingi ya wabunge,hutolewa kwa maandishi,Lakini kwa sababu watanzania tunafuata sana emotions zetu na si uhalisia wa mambo,basi wale wabunge ambao wanatoa michnago yao kwa maandishi sisi hatuwaoni kama wanafanya lolote.Ikumbukwe kwamba wakisema kila mbunge kule bungeni aongee,basi itabidi bunge liwe la miaka miwili mizima kuweza kumaliza kipindi bunge moja la bajeti.
Na kila mbunge,ana haki ya kusema yeye ndiye achaguliwe kuongea LIVE kile anachochangia.
Sasa je,nani aseme na nani asiseme LIVE?
Kumbuka kuonekana LIVE,watanzania wanakuona na kukuthaminisha(hasa wengi wao wanachukulia ndio muda wa kueleweka kwamba wanafaa)
Katika Siasa za Vyama vingi,inakuwa vigumu zaidi kuweza kupanga nani ataongea na nani asiongee.
Kila mmoja atataka aongee
Sasa cha kufanya ni nini hapa?Inatafutwa njia ambayo ni "Objective" ili kuwapa wabunge wengi zaidi muda wa kuongea LIVE
Na kwa sababu hivi ni vyama vingi,basi kila chama lazima wabunge wake wanafanana katika "nini cha kusema",ingawaje si mara zote.
Hivyo,kama ndivyo,basi kwa sababu kuna wabunge 300 kutoka vyama A,B,C na D,na Idadi ya wabunge katika vyama hivyo ni 200,50,40,10,respectively,then wape uwiano wa muda hivyo hivyo,kwa mfano katika saa moja la LIVE bunge talk,watapata katika uwiano wa 40mins(muda kwa ajili ya wabunge hao 200 kutokea chama A wanaotaka kuongea),10mins(muda kwa ajili ya hao wabunge 50kutokea chama C wanaotaka kuongea),7mins( muda kwa ajili ya wabunge hao 40 kutokea chama C wanaotaka kuongea) and 3mins(muda kwa ajili ya wabunge hao 10 kutokea chama D wanaotaka kuongea).....Objectively,utaona kwamba kila mbunge wa bunge amepewa hapo dakika 60/300=0.02
Hapo kumbuka kila Mbunge analalamika kwamba mbona mie sipewi muda?ama Chama kimoja kinasema mbona sie hatupewi muda?-----na suluhisho la kweli linakuwa hilo lililofanyika.
Kwa hiyo,kama nilivyotangulia kusema wabunge kutoka chama kimoja ni lazima kwa kiasi kikubwa wanakuwa wanashabihiana misimamo yao,na hivyo hata cha kuongea wanakuwa wanashabihiana,na kutofautiana ni kidogo,pia kukubaliana ni rahisi---hivyo basi,kila chama inatakiwa wajipange kuweza kuona ni namna gani watatumia muda wao ili kuweza kuwakilisha kile wanachotaka kuongea
Sasa nadhani wabunge wengi zaidi watakuwa wanaongea.
Lakini nadhani bado kila chama kitakuwa kinachagua nani wa kumpandisha chati kwa muda gani,ili apewe muda mrefu zaidi (kutoka kwenye ule muda wao wanaopewa)----Kumbuka wabunge wote mashuhuri wametokana na kuongea sana bungeni(watanzania tunapenda watu wanaoongea jamaniiiiiii...chaaaaaa!mburaaaaa)