Wabunge hawa wa CHADEMA wanatukera sana

Wabunge hawa wa CHADEMA wanatukera sana

Wamekuwa kero kwelikweli kwetu. Wanaheshimiwa kuliko waheshimiwa wa chama na Serikali. Tunawajadili,hawajadiliki.Mipango dhidi yao tunaipanga,inapanguka. Kwakweli,ni kero hasa. Wanawaaminisha watanzania kuwa chama chao kinaweza kuwa na viongozi bora na wasemaji wazuri. Wanaanza kueleweka. Ni hawa:

Freeman Aikaeli Mbowe-Hai, Philemon Ndesamburo-Moshi Mjini,John John Mnyika-Ubungo, Vincent Nyerere-Musoma Mjini, Mchungaji Peter Msigwa-Iringa Mjini, Halima Mdee-Kawe, Godbless Jonathan Lema-Arusha Mjini, Joshua Nassari-Arumeru Mashariki, Tundu Lissu-Singida Mshariki, Ezekiel Wenje- Nyamagana, Joseph Mbilinyi-Mbeya Mjini, mwanangu Silinde wa Mbozi Magharibi na Joseph Selasini wa Rombo.

Amini nawaambia,Wabunge hawa ni kero kuu kwetu CCM na ni mtaji mkubwa wa CHADEMA kama sehemu ya UKAWA. Wana mizizi migumu majimboni mwao. Kuwang'oa yatubidi kuongeza nguvu. Ili wasimwage sumu yao Tanzania nzima.

Mapambano yanaendelea lakini!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Mkuu ilibaki kidogo nianze kuporomosha matusi, asante sana kwa kuona ukweli.
 
Hadi sasa matokeo yaliyokusanywa ni kutoka katika vijiji 9,047 na mitaa 3,078.
Matokeo hayo yanaonesha kuwa Chama Cha Mapinduzi CCM kimeongoza uchaguzi huo kwa kujinyakulia vijiji 7,290 sawa na 80.58% na mitaa 2,116 sawa na asilimia 68.7% huku chama kikuu cha upinzani CHADEMA kikijinyakulia vijiji 1,248 sawa na 13.8% na mitaa 753 sawa na 24.5%.
Ikumbukwe ushindi wa 80.58% wa CCM ni pamoja na wagombea waliopita bila ya kupingwa kutokana na mapingamizi au Upinzani kushindwa kusimamisha wagombea ambao ni 33%. Hivyo kwa maeneo ambayo uchaguzi umefanyika utaona jinsi ushindani ulivyokuwa mkubwa. CCM wameshinda kwa 47% tu.

Chama cha Wananchi CUF kimeibuka nafasi ya Tatu kwa kujinyakulia vijiji 382 na mitaa 235 wakati NCCR Mageuzi kikipata mitaa 8, ACT mitaa 9, TLP mtaa 1 na vijiji 2, UDP Vijiji 4 na NLD vijiji 2.
Kata 120 zinatarajiwa kufanya Uchaguzi wiki hii.
 
Poleni mzee Tupatupa. Kwa nini hamjishughulishi na mpasuko wa chama chenu mnabaki kuweweseka na wabunge wa Chadema? Na mbona mnamruhusu Nape anaendelea kuwapotosha wanachama kuwa chama kimefanya vizuri uchaguzi huu ilihali pamoja na kupita kwa viti vingi kwa mapingamizi magumashi na kutumia mbinu chafu bado wamedrop sana?
Huku sio kuua chama kwa kutoa habari za kuwafanya wabweteke hali wanaangamia?

tunashuhurika kwanza na huo mpasuko wa hapo nyuma kwako tukisha maliza ndo tutaendelea na mambo mengine
 
hii hadithi yako inatufundisha nini?
maana naona porojo tu humu.

Wamekuwa kero kwelikweli kwetu. Wanaheshimiwa kuliko waheshimiwa wa chama na Serikali. Tunawajadili,hawajadiliki.Mipango dhidi yao tunaipanga,inapanguka. Kwakweli,ni kero hasa. Wanawaaminisha watanzania kuwa chama chao kinaweza kuwa na viongozi bora na wasemaji wazuri. Wanaanza kueleweka. Ni hawa:

Freeman Aikaeli Mbowe-Hai, Philemon Ndesamburo-Moshi Mjini,John John Mnyika-Ubungo, Vincent Nyerere-Musoma Mjini, Mchungaji Peter Msigwa-Iringa Mjini, Halima Mdee-Kawe, Godbless Jonathan Lema-Arusha Mjini, Joshua Nassari-Arumeru Mashariki, Tundu Lissu-Singida Mshariki, Ezekiel Wenje- Nyamagana, Joseph Mbilinyi-Mbeya Mjini, mwanangu Silinde wa Mbozi Magharibi na Joseph Selasini wa Rombo.

Amini nawaambia,Wabunge hawa ni kero kuu kwetu CCM na ni mtaji mkubwa wa CHADEMA kama sehemu ya UKAWA. Wana mizizi migumu majimboni mwao. Kuwang'oa yatubidi kuongeza nguvu. Ili wasimwage sumu yao Tanzania nzima.

Mapambano yanaendelea lakini!

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
tunashuhurika kwanza na huo mpasuko wa hapo nyuma kwako tukisha maliza ndo tutaendelea na mambo mengine
tunashuhulika ndio neno gani tena hilo? Kijana sii ungeenda shule kwanza haya mambo ya JF sii utayakuta tuu baadae? Kuandika hujui, kiswahili nacho pia majanga! Ila nyie vilaza ndio tumaini na turufu ya mwisho ya Magamba.
Hilo neno linaandikwa hivi tunashughulika.
 
Mzee VUTA-NKUVUTE namkubali sana!!!


Sent from my iPhone using JamiiForums app
 
Last edited by a moderator:
Wanabumburua dili zetu....mimi mama Anna Tibaijuka wabunge wengi wa CDM wanaweza kuwa wanangu wa kuwazaa ila wale watoto hawana hata haya kuninyoshea kidole mtu mzima kama mimi....ndio nimechota lakini hamkutakiwa kuniumbua mtu mzima namna ile
 
Back
Top Bottom