Wabunge hawa wa CHADEMA ni mizigo isiyobebeka

Hoja yako ni ya msingi sana. kinachoikuta CHADEMA sasa ni matatizo ya kukua kwa chama. wakati wa bunge lililopita, CDM walikuwa wachache sana bungeni, na walileta changamoto kubwa sana kwa sababu karibu wote walikuwa wanajituma. kwa hiyo kutokana na kuwa na wabunge wengi zaidi bunge hili, tulitarajia makubwa zaidi kwa ulinganifu ule ule wa bunge lililopita, kwamba kama wabunge 4 wa CDM kila mmoja aliwakilisha 10 wa CCM, basi wabune 40 wa CDM watabeba 400 wa CCM. pengine haikuwa hivyo, ijapokuwa kuna majembe yameingia bunge hili ambapo bunge lililopita hayakuwepo, na yamefanya kazi kubwa sana. lakini kuna pia mambo ya msingi ya kuangalia:

1. Chama kiwe na programu ya kuhamasisha na kuwezesha wabunge na madiwani wake. hapa ni kupitia mafunzo, kuwapa feedback juu ya utendaji wao na kila baada ya kipindi fulani, kufuatilia ahadi zao, utekelezaji wao wa mikakati ya chama katika maeneo yao.

2. kutambua kwamba umuhimu wa kwanza ni kuwajibika jimboni, wala siyo bungeni. wabunge na madiwani wanatakiwa kuwatumikia wananchi kwa kutoa huduma ya hali ya juu. hapa wanahitaji msaada kutoka kwa wapambanaji mbalimbali. mimi binafsi nilikuwa tayari kutoa msaada huo kwa mbunge wangu wa CDM, na nilitamka hivyo alipotutembelea eneo letu. lakini niliishia kupewa simu ya msaidizi wake na pamoja na jitihada zangu, sikufanikiwa kupata nafasi ya kufanya chochote. inabidi ziwekwe taratibu zitakazoruhusu wanaopenda kujitolea kusaidia chama katika shughuli mbalimbali waweze kufanya hivyo.
 
Kweli umenena kumuita mzigo sio kumtendea haki kazi yake inaonekana. NI JEMBE LA UHAKIKA
 
Umeshajiulza pia ccm watabaki wangapi? Au kapten Komba, lusinde, maji marefu, Sophia simba, ongezea wengine kamanda

Acha kumtaja maji marefu. Unamjua vizuri wewe? Utajikuta umelala juu ya mti sasa hvi ukiwa uchi... We cheza na prof.
 
Mbona ndugu zangu mnaona mbunge kutokuwa mzigo ni kuwa anaongea sana bungeni. Kuna wabunge wanaongea sana ila majimboni kwao wana hali mbaya na sijui kama wataweza tetea hayo majimbo mwakani. Mfano ni mheshmiwa mnyika , mh. mbowe , na wengine. Na pia mbna umemsahau mzigo Lema??
 
Mh. Machemuli ni mzigo I concur...

Mimewahi kukaa naye meza moja kuna mtu alinitambulisha kwake...uwezo wake ni mdogo sana...Ana matatizo makubwa ya ki utu...anakera sana wapiga kura wake.. inafikia hatua anawakopa, kutumia ubunge wake...

Sidhani kama CDM watatweza kutetea jimbo la Uk!! I doubt...

huu mzigo lazima tuutue
 
Yule Chiku nani sijui si mbunge wa viti maalum yule....mbona yuko vizuri?
 
mkuu kura za maoni zitaamua lakini kila mtu anajua matokeo yake huyu jaffari akichukua fomu ameshashinda ni kama kule mbulu mikael aweda akichukua fomu kwenye kura za maoni lazima amgaragaze akonaay hata pale arumeru magharibi OLE Ikayo akichukua fomu tiyari ni mshindi hata kule Rombo ben saanane akichukua fomu atamgaragaza selasini
hii ni kwasababu wanao ushawishi mkubwa na wanakubalika

Ok hapo nimekupata uzuri mkuu.
 
Hoja yako ni ya msingi sana. kinachoikuta CHADEMA sasa ni matatizo ya kukua kwa chama. wakati wa bunge lililopita, CDM walikuwa wachache sana bungeni, na walileta changamoto kubwa sana kwa sababu karibu wote walikuwa wanajituma. kwa hiyo kutokana na kuwa na wabunge wengi zaidi bunge hili, tulitarajia makubwa zaidi kwa ulinganifu ule ule wa bunge lililopita, kwamba kama wabunge 4 wa CDM kila mmoja aliwakilisha 10 wa CCM, basi wabune 40 wa CDM watabeba 400 wa CCM. pengine haikuwa hivyo, ijapokuwa kuna majembe yameingia bunge hili ambapo bunge lililopita hayakuwepo, na yamefanya kazi kubwa sana. lakini kuna pia mambo ya msingi ya kuangalia:

1. Chama kiwe na programu ya kuhamasisha na kuwezesha wabunge na madiwani wake. hapa ni kupitia mafunzo, kuwapa feedback juu ya utendaji wao na kila baada ya kipindi fulani, kufuatilia ahadi zao, utekelezaji wao wa mikakati ya chama katika maeneo yao.

2. kutambua kwamba umuhimu wa kwanza ni kuwajibika jimboni, wala siyo bungeni. wabunge na madiwani wanatakiwa kuwatumikia wananchi kwa kutoa huduma ya hali ya juu. hapa wanahitaji msaada kutoka kwa wapambanaji mbalimbali. mimi binafsi nilikuwa tayari kutoa msaada huo kwa mbunge wangu wa CDM, na nilitamka hivyo alipotutembelea eneo letu. lakini niliishia kupewa simu ya msaidizi wake na pamoja na jitihada zangu, sikufanikiwa kupata nafasi ya kufanya chochote. inabidi ziwekwe taratibu zitakazoruhusu wanaopenda kujitolea kusaidia chama katika shughuli mbalimbali waweze kufanya hivyo.

mkuu shikamoo..nimependa sana uchambuzi wako
 
wakuu

Salaam

Kwanza nianze kwa kusema mimi ni mwanachama hai wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA tena inaweza kuwa nimejiunga siku nyingi kuliko wewe lakini ngoja lro niseme ukweli mtupu.

Kumekuwa na hili neno "mzigo" linalotumika sana kwenye siasa na niukweli usiopingika kuwa viongozi wa chama cha mapinduzi wengi (almost all) ni mizigo tena mizigo mikubwa sana lakini hata sisi wapinzani tuna mizigo yetu.

kwa upande wangu mimi na kwa chama changu cha CHADEMA mizigo hiyo ni

1) John Shibuda
Huyu kila mtu anajua alivyo tatizo ndani ya chama chetu na sijui ni kwanini tulikubali kupokea huu mzigo uliowashinda CCM .

Kitu anachokiweza ni mipasho na misemo yake bungeni hana la ziada
fani aliyobobea ni kuhama vyama na kuanzisha malumbano yasiyo na tija ndani ya vyama

2) Mh. prof. Kahigi
huyu mzee nadhani alishinda ubunge kwasababu ya tittle yake ya "uprof"ndicho kigezo alichotumia kuwahadaa wananchi wakampa ubunge lakini kujenga hoja hawezi kabisa nilitegemea angeleta michango muhimu kwenye kambi ya upinzani kama msomi lakini wapi.

3)Mh.machemli
huyu mimi sijawai hata kumuona akiongea bungeni japo mimi ni mfuatiliaji mzuri wa vikao vya bunge kwanza sidhani hata bungeni kama anaendaga muulize mwanachama yeyote wa CHADEMA kama alishawai kusikia kama kuna mtu anaitwa machemli wewe mwanachama wa CHADEMA unamjua huyu mtu japo kwa sura tu?

4)Mh. Opulukwa
Huu tena ni mzigo mwingine usiobebeka hata sihitaji kufafanua kila mtu analielewa hili.

5)mh. Kiwia Highness
Huyu labda kwa sababu ya ugonjwa wake kila mara analazwa nje ya nchi kidogo siwezi nikamuongelea lakini kama tunataka hili jimbo liendelee kubaki kwetu tumtute kamanda mwingine tusonge mbele

6) Mh. Selasini
Kiukweli huyu mzee hawezi chochote sio jimboni bungeni wala kwenye chama ni mzigo mkubwa tusipoangalia hili jimbo tutalikosa.

7) mustapha akonaay
CHADEMA bado inaushawishi kwenye jimbo la mbulu lakini tusipokuwa makini tukausimamisha mzigo huu jimbo tutalipoteza

8) Wabunge wote wa viti maalum

Kiukweli sijaona mbunge yeyote wa viti maalum chadema ambaye sio mzigo wote ni "empty set". Nilitegemea kuona wabunge wa viti maalum wenye kaliba ya Mdee wa bunge la tisa akiwa mbunge wa viti maalum lakini wapi hawa wote ni mizigo mitupu.

Hakuna kazi wanayofanya sio ndani ya bunge wala nje ya bunge wala kazi za chama. Nijuavyo mimi ubunge wa viti maalum ni kwaajili ya kuwajengea uwezo na platform ili wawe wabunge wa majimbo kabisa (mfano Mdee) lakini hawa hawana uelekeo wowote.

Embu jiulize CHADEMA ina wabunge zaidi ya ishirini wa viti maalum wewe unawajua wangapi ?wanafika watano ...!! yupi mwenye uwezo wa kuwa mbunge wa jimbo!

Nakishauri chama changu kuwapiga chini hii "MIZIGO" yote uchaguzi ujao.

NB: Nitajitolea fedha za fomu na kampeni kwa kijana yoyote atakayeonesha nia kwenye majimbo tajwa hapo juu.

kilaza

kweli kabisa ila viti maalum wapo wafuatao wako poa
1. chiku abwao kiboko ya Lukuvi
2. suzan kiwanga kiboko ya celina kombani
3. Rachel mashishanga kiboko ya stiven masele
4. ester matiko kiboko ya nyambari nyangwine
5. cecilia daniel pareso
 
kweli kabisa ila viti maalum wapo wafuatao wako poa
1. chiku abwao kiboko ya Lukuvi
2. suzan kiwanga kiboko ya celina kombani
3. Rachel mashishanga kiboko ya stiven masele
4. ester matiko kiboko ya nyambari nyangwine
5. cecilia daniel pareso

wote uliowataja sijaona impact yao kivileeeee wapowapo tu
 
Paulina Gekul ni wa ukweli, huwa nasafiri Babati na kushuhudia sarakasi zake nyingi jimboni, anaweza kushika jimbo yule!
 
ukiacha shibuda , wengine wote umewaona mizigo kwa michango ya bungeni tu , hukuangalia majimbo wanayotoka , fanya utafiti .
 
Shibuda kwa kuwa anaweza sana misemo,nahau,methali tumpugie pande akafundishe somo la kiswahili Maswa Sekondari
 
wakuu

Salaam

Kwanza nianze kwa kusema mimi ni mwanachama hai wa chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA tena inaweza kuwa nimejiunga siku nyingi kuliko wewe lakini ngoja lro niseme ukweli mtupu.

Kumekuwa na hili neno "mzigo" linalotumika sana kwenye siasa na niukweli usiopingika kuwa viongozi wa chama cha mapinduzi wengi (almost all) ni mizigo tena mizigo mikubwa sana lakini hata sisi wapinzani tuna mizigo yetu.

kwa upande wangu mimi na kwa chama changu cha CHADEMA mizigo hiyo ni

1) John Shibuda
Huyu kila mtu anajua alivyo tatizo ndani ya chama chetu na sijui ni kwanini tulikubali kupokea huu mzigo uliowashinda CCM .

Kitu anachokiweza ni mipasho na misemo yake bungeni hana la ziada
fani aliyobobea ni kuhama vyama na kuanzisha malumbano yasiyo na tija ndani ya vyama

2) Mh. prof. Kahigi
huyu mzee nadhani alishinda ubunge kwasababu ya tittle yake ya "uprof"ndicho kigezo alichotumia kuwahadaa wananchi wakampa ubunge lakini kujenga hoja hawezi kabisa nilitegemea angeleta michango muhimu kwenye kambi ya upinzani kama msomi lakini wapi.

3)Mh.machemli
huyu mimi sijawai hata kumuona akiongea bungeni japo mimi ni mfuatiliaji mzuri wa vikao vya bunge kwanza sidhani hata bungeni kama anaendaga muulize mwanachama yeyote wa CHADEMA kama alishawai kusikia kama kuna mtu anaitwa machemli wewe mwanachama wa CHADEMA unamjua huyu mtu japo kwa sura tu?

4)Mh. Opulukwa
Huu tena ni mzigo mwingine usiobebeka hata sihitaji kufafanua kila mtu analielewa hili.

5)mh. Kiwia Highness
Huyu labda kwa sababu ya ugonjwa wake kila mara analazwa nje ya nchi kidogo siwezi nikamuongelea lakini kama tunataka hili jimbo liendelee kubaki kwetu tumtute kamanda mwingine tusonge mbele

6) Mh. Selasini
Kiukweli huyu mzee hawezi chochote sio jimboni bungeni wala kwenye chama ni mzigo mkubwa tusipoangalia hili jimbo tutalikosa.

7) mustapha akonaay
CHADEMA bado inaushawishi kwenye jimbo la mbulu lakini tusipokuwa makini tukausimamisha mzigo huu jimbo tutalipoteza

8) Wabunge wote wa viti maalum

Kiukweli sijaona mbunge yeyote wa viti maalum chadema ambaye sio mzigo wote ni "empty set". Nilitegemea kuona wabunge wa viti maalum wenye kaliba ya Mdee wa bunge la tisa akiwa mbunge wa viti maalum lakini wapi hawa wote ni mizigo mitupu.

Hakuna kazi wanayofanya sio ndani ya bunge wala nje ya bunge wala kazi za chama. Nijuavyo mimi ubunge wa viti maalum ni kwaajili ya kuwajengea uwezo na platform ili wawe wabunge wa majimbo kabisa (mfano Mdee) lakini hawa hawana uelekeo wowote.

Embu jiulize CHADEMA ina wabunge zaidi ya ishirini wa viti maalum wewe unawajua wangapi ?wanafika watano ...!! yupi mwenye uwezo wa kuwa mbunge wa jimbo!

Nakishauri chama changu kuwapiga chini hii "MIZIGO" yote uchaguzi ujao.

NB: Nitajitolea fedha za fomu na kampeni kwa kijana yoyote atakayeonesha nia kwenye majimbo tajwa hapo juu.

kilaza

We igogo na wewe mwakani nenda kagombee kwenu RORYA
 
Back
Top Bottom