Wabongo tunafeli wapi? tabia hii ya kuigana itakwisha lini?

Wabongo tunafeli wapi? tabia hii ya kuigana itakwisha lini?

Hii haikuanza leo, enzi hizo biashara ya kutengeneza batiki inaingia kila mtu anatengeneza batiki hadi zikashuka bei. Wakati zinaanza batiki moja ilikuwa Tsh. 13,000/- miaka hiyo...

Nikaachana na biashara ya kuungua na mishumaa halafu unauza batiki 6,000/-.
Heheh haya mambo sio ya leo kumbe??
 
Bongo watu hawataki kabisa kufikiri, ni mwendo wa KUSIKIA na KUIGA, magari mpk imekuwa sare sare mpk rangi jirani anaiga, mtaani kwetu kila mtu KLUGER nyeusi!
 
Bongo watu hawataki kabisa kufikiri, ni mwendo wa KUSIKIA na KUIGA, magari mpk imekuwa sare sare mpk rangi jirani anaiga, mtaani kwetu kila mtu KLUGER nyeusi!
Wewe ndio wa kwanza kununua?
 
Mkuu labda umeshinda kuielewa, ni jambo la kujipongeza kuwa watanzania wanaamka hamna biashara mpya duniani itakayofanywa na mtu mmoja muamko wa watu kujitafutia kipato cha ziada ni mkubwa na mji mdogo huu, so tegemea kuona hivyo hivyo na wewe roho isikuume fanya...pamoja na wingi wa watoa huduma na biashara bado hatujafikia kiasi cha kuoneana wivu, ama ulitaka Tanzania nzima forex afanye ontario tuu na uber umiliki peke yako?
 
Naongezea


Wauza mihogo mibichi kuongeza nguvu za kiume




Kunywa madafu kuongeza nguvu za kiume



Kulima mahindi kwaajili ya kuuza yakiwa mabichi almaarufu mahindi ya kuchoma



Kwa kweli mfumo wa shule wa kukariri ndio unatupelekea tusiwe na hata chembe ya kufikiri

Je mkuu hao watu hawajiingizii kipato cha kuendesha maisha yao, wewe unayefikiri sana sasa ivi unafanya nini cha tofauti na wengine?
 
Mkuu labda umeshinda kuielewa, ni jambo la kujipongeza kuwa watanzania wanaamka hamna biashara mpya duniani itakayofanywa na mtu mmoja muamko wa watu kujitafutia kipato cha ziada ni mkubwa na mji mdogo huu, so tegemea kuona hivyo hivyo na wewe roho isikuume fanya...pamoja na wingi wa watoa huduma na biashara bado hatujafikia kiasi cha kuoneana wivu, ama ulitaka Tanzania nzima forex afanye ontario tuu na uber umiliki peke yako?
Point of correction mtoa mada hajaongea vibaya ila anataka watu tufanye research kwanza tusikurupuke kuona mwenzako kafanya hv nawewe bila kufanya reseach unaingia mzimamzima utafirisika na kurudi nyuma.
 
Ha ha haaaa, eti kila nyumba kwiyokwiyo, ufugaji wa kuku unahtaj nidhamu, uvumilivu na innovation, ni baada ya kazi ngumu yenye hasara nyingi na kukatishs tamaa ndo unaweza ukatoboa, kilimo cha matikiti full kichekesho kila mtu atakwambia yalianza fresh kwenye kufikia kuiva yakaoza yote..ha ha haaaa, katika watu kumi wanaolima matikiti wanane lazima waje wanalia...
 
Point of correction mtoa mada hajaongea vibaya ila anataka watu tufanye research kwanza tusikurupuke kuona mwenzako kafanya hv nawewe bila kufanya reseach unaingia mzimamzima utafirisika na kurudi nyuma.

Mkuu hivi unafahamu biashara yoyote ina risk, mimi nashauri waingie wafanye, huwezi kumzuia mtoto asianze kunyanyuka na kutembea kisa anaweza kudondoka na kuumia, hizo changamoto zipo na kadiri mtu anapoanza biashara ina maana ana target zake hawezi kuingia kama zombie tuu hajielewi inapofeli inafeli unaamka tena hata hizo researched start up business 90+% zinafeli, dunia nzima sasa inaweza kuwa wewe ama mwingine akafeli, wil you take your chance or not, that’s up to you
 
Nafikiri cha kujadili hapa sio kuigana biashara.. maana ni biashara chache sana duniani zinazoanzishwa leo na kuonekana ni mpya.

Ishu hapa ni kuanzisha biashara na kuifanya kwa namna ile ile kama wafanyavyo wenzako waliokwisha kutangulia. Kinachotakiwa ni kuifanya hiyo biashara kwa namna tofauti ambayo ni gharama nafuu zaidi kuliko wenzako na wakati huo ukipata faida sawa au kuwazidi hao wenzako uliowaiga.

Mleta mada kama kila mtu angekuwa na mawazo kama haya yako basi leo hii tusingekuwa na makampuni kama Techno na Huwawei maana tayari walimkuta Nokia yuko sokoni kitambo.
 
Hivi wale Motivational speakers a.k.a MENTORS basi karibia kila MC alijifanya Motivational speaker. Unakuta jamaa hana hata kuku wawili wala bustani ya mbogamboga kwake halafu halafu anafundisha watu kilimo au ufugaji just kwa paper work tu.

Pia ufugaji wa sungura hapa napo wakenya na kampuni uchwara kama NAMAHINGO walitapeli sana wakulima, nakumbuka sungura mmoja walikuwa wanauza Dume Tshs. 60,000/= na Jike Tshs. 90,000/=
 
Kuiga biashara si dhambi wala si vibaya kwani hakuna biashara duniani iliyofanywa na mtu mmoja,kumbuka anaeiga biashara ya mtu mwingine analazimika kuwa na ubunifu zaidi ili aweze kuendelea kuwepo kwenye biashara hiyo. Ubunifu haupo kwenye kuanzisha biashara tu bali hata kuendelea kubaki kwenye biashara pia.
 
Kwanini kila neno unaanza na herufi kubwa? Huu uandishi wa wapi!
 
Siku hizi kuna

Kuuza juice ya miwa
Wachoma mishikaki ya mia mia
Kila kaya kuna genge.
 
Kuigusa Forex ni kuigusa Taasisi ya uraisi subiri kuumia
emoji23.png
 
Eti kuwainjika!!Umesahau kilimo cha vitunguu Ruaha Mbuyuni
 
Back
Top Bottom