Wabongo tunafeli wapi? tabia hii ya kuigana itakwisha lini?

Wabongo tunafeli wapi? tabia hii ya kuigana itakwisha lini?

kakamgeni

JF-Expert Member
Joined
Feb 1, 2018
Posts
241
Reaction score
201
Ahlan Wa Sahlan Members Wenzangu Wa JF,

Natumaini Kuwa Hamjambo Na Mnaendelea Vyema Na Mapumziko Ya Sikukuu Za Nanenane Sambamba Kabisa Na Eid.

Kwanza Kabisa Ningependa Kutoa Pole Kwa Watanzania Wenzangu Wote Na Wale Wenzetu Waliopoteza Ndugu, Jamaa Na Marafiki Katika Ajali Mbaya Ya Moto Iliyotokea Asubuhi Ya Leo Mkoani Morogoro.

Naungana Nanyi Katika Kipindi Hiki Kigumu...Nikimuomba Mwenye Mamlaka Kupitia Viumbe Wote Ulimwenguni Aweze Kuwatia Nguvu Na Faraja...Hakika Huu Ni Msiba Mkubwa Wa Taifa.

Basi Ningependa Kwenda Straight Kwenye Mada Niliyoileta Kwenu Katika Jukwaa La Habari Mchanganyiko...Kiukweli Hili Jambo Nimekuwa Nikisema Nitakuja Kulisema Kwa Muda Mrefu Ila Leo Nimeona Ngoja Nilitolee Uvivu.

Inapendeza Kuiga Jambo Au Kitu Kizuri Anachofanya Mtu Ambacho Kina Maslahi Ndani Yake...Ila Kabla Ya Kuiga Hilo Ni Vyema Kukifanyia Uchunguzi Ikiwemo Changamoto Zake Ndipo Uweze Kulifanya Kwa Ufanisi Zaidi.

Kumekuwa Na Kasumba Hasa Katika Miji Mikubwa Kwa Hapa Tanzania Ambayo Inamaendeleo Watu Kuigana Biashar a Na Mwisho Wa Siku Watu Kujikuta Wakiangukia Pua Na Hizo Biashara Kufa Kabisa...Nikianza Na Mifano Hai Kama Ifuatavyo ;

BIASHARA YA KUKU WA KISASA : Hii Biashara Wakati Inaanza Haikuwa Na Wafugaji Wengi...Lakini Baada Ya Muda Ikavamiwa Na Watu...Ilikuwa Kila Nyumba Ukipita Ni Kwiyokwiyo...Ukiuliza Watakwambia Ni Wafugaji...Hali Hii Ilipelekea Hadi Wake Wa Viongozi Wenye Nyadhifa Za Juu Kujikita Kwenye Biashara Hii...Ikaendaenda Baadae Wale Waliodandia Treni Kwa Mbele Ikawashinda Na Kuachana Na Hiyo Biashara.

MAYAI YA KWARE : Jamani Jamani Katika Biashara Za Uzushi Zilizowahi Ku-trend Basi Kamwe Hawezi Kuiacha Hii...Nakumbuka Niliwahi Kumnunulia Bi Mdanga Karibu Trey 4 Za Haya Mayai...Ukikutana Na Wauzaji Wenyewe Utasikia Haya Mayai Yanapunguza Pressure, Shinikizo La Damu Na Blah Blah Nyingi...Mwisho Wa Siku Ikapotea Hadi Leo Sijapata Kuisikia.

FOREVER LIVING : Huu Mtandao Uliwahi Kunikuta Mwaka 2009 Nakumbuka...Aiseee Hamasa Yake Ilikuwa Ni Kubwa Hata Nguvu Ya Soda Inasubiri...Ukifika Kwenye Ofisi Zao Hizo Sound Utakazoveshwa UnawezaKusema Kesho Unaamka Bilioni...Thubutuu!!!Anza Uone...Nakumbuka Kipindi Kile Hadi Profesa Juma Kapuya Na Kiongozi Wengine Waliingia Kwenye Mkumbo Huu...Watu Walisaga Soli Mwisho Wa Siku Wakaona Wakimbie Kwa Aibu...Kwa Sasa Speed Yake Ni 0.009Kps...

KILIMO CHA MATIKITI : Aiseee Kilimo Hiki Kilikuwa Kama Fashion Kwa Watu Mjini...Ukikutana Na Kijana Utasikia Nina Shamba Langu Hapo Vigwaza La Matikiti Nategemea Kuvuna...Watu Walivamia Kichwa Kichwa Kilimo Hiki Na Kujikuta Wakiangukia Pua...Huku Wakulima Wanaofuata Kanuni Wakiendeleza Libeneke...

DAGAA WA KIGOMA : Hawa Nakumbuka Kuna Jirani Yangu M1 Ni Mmama Mtu Wa Makamo Alikuwa Akinishawishi Kweli Niingie Kwenye Huu Mkenge...Mwisho Wa Siku Kilichomtokea Ni Kujikuta Akiingi Kwenye Madeni Na Kutapeliwa Na Wajanja wa Hizo Kazi...Wengine Ilifika Hatua Wakawa Wanapakia Kwenye Magari Yao Wanavizia Watu Wa Maofisini Kuwauzia...

UFUGAJI WA SAMAKI : Yaani Hapa Ndio Unaweza Ukavunjika Mbavu..Ukisema Sasa Hivi Ufanye Research Usishangae Ukakutana Na Mabwawa Mengi Yakiwa Yamekauka Hakuna Samaki Zaidi Zaidi Utakutana Na Nyavu Za Kuvulia...Watu Kimyaaaa Wamewaacha Wenye Fani Zao Wanaendelea Kupiga PESA...

MBEGU ZA MABOGA : Sasa Hivi Imekuwa Mpaka Kero...Ukikaa Bar Au Kwenye Migahawa Utakuta Wamama Tena Hata Vaa Zao Huwa Zinafanana...Utakuta Wanakutolea Pakti Ya Maboga Wanakwambia Wanauza Inasaidia Nguvu Za Kiume Na Mambo Kibao...

UBUYU WA ZANZIBAR/ONLINE SHOPING : Hii Imekuwa Kama Fashion Hasa Mitandaoni Kila Mtu Anauza Ubuyu Na Hasa Wanafunzi Wa Vyuo Unakuta Wanamiliki Page Zao Za Online Shopping...Baada Ya Watu Kulialia Kutapeliwa Naona Walau Kidogo Imepungua...Shughuli Imehamia Kwenye Kuuza iPhone Na Saa Za Mkononi...Naona Nao Wanakuja Kasi Ka Kimbunga Cha Katrina...

UDALALI WA MAGARI NA UBER : Sasa Hivi Ukiingia Katika Ofisi Basi Usishangae Ukakutana Na Dalali Wa Magari...Wengine Wanajiita Walengaji...Kwa Hakika Udalali Wa Magari Umevamiwa...Hata Ukiangalia Kwenye Groups Za Kuuza Na Kununua Magari Mtandaoni Ni Vurugu Tupu...Haya Hapa Kwa Uber Ndio Hata Sitaki Kuzungumza Zaidi...Wapo Waliochukua Mikopo Hadi Kwenye Mabenki Wakanunua Magari Mengi Kwa Mkupuo Na Kuyafanya Uber Ila Cha Moto Walikiona...Kingine Baadhi Ya Madereva Wengine Wa Uber Hata Driving Yao Haiko Poa Na Hata Kujali Vyombo Vyao Ni Mtihani...Chunguza Utakuja Kuniambia.

FOREX/BITCOIN : Hawa Naweza Kuwaita Wajomba Zake ONTARIO Bingwa Wa Kuandika Magazeti Ya Kuwainjika Wenzie..Hahahhaaaa...Navyoongea Hapa Kuna Mtu Ukimwambia Au Ukimtajia Neno Forex Anaweza Akazimia Au Mshipa Wa Kichwa Ukamcheza...

Rai Yangu kwa Watanzania Wenzangu Kuiga Kitu Hakuna Ubaya Ila Kabla Ya Kuamua Kufuata Mkumbo Ebu Tafuta Muda Wa Kufanya Research Hata Ikikuchukua Mwaka Haiko Mbaya Maana Wajua Unachoenda Kukifanya...Overrr!!!
 
Hii haikuanza leo, enzi hizo biashara ya kutengeneza batiki inaingia kila mtu anatengeneza batiki hadi zikashuka bei. Wakati zinaanza batiki moja ilikuwa Tsh. 13,000/- miaka hiyo...

Nikaachana na biashara ya kuungua na mishumaa halafu unauza batiki 6,000/-.
 
Umeniacha mbavu sina. Tunapenda sana mtelemko ndio maana tunakwama. I have gone long way baada ya kumaliza kusoma. Nina hakika kabisa, bila kubadilika sitafika. tena nibadilike kweli kweli. Nikiangalia wale walichosoma sawa na mimi wanachofanya wakafanikiwa, sina budi kubadilika.
Hela rahisi zipo Forever Living na Bitcon tu
 
Watanzania wengi tunafeli kwasababu ya
a)Kufanya biashara ambazo watu fulani wamefanikiwa nazo au
b)Wingi wa watu katika biashara hiyo
Wengi wetu hatufanyi biashara ambazo tunazipenda, tunazijua na tuna maarifa nazo.
Na ukiuliza majibu yetu huwa;
1.Umemuona yule kipapi usimuone vile sikuhz mambo yake super anafanya biashara fulani yule.
2.Sikuhizi ujanja kufanya biashara fulani, kila mtu mjini ndio mishe zake wewe unangoja nini!
 
Una deserve kuitwa great thinker, umenigusa kwenye Forex, ni mwaka na zaidi sasa naisoma online.. kiukweli ukiwa mwepesi wa kupelekeshwa na upepo maisha yatakuwia magumu na majuto mengi
 
Hakuna hela rahisi, futa huo usemi kabla hujaanza chochote.. kama sio kutumia nguvu basi akili
Umeniacha mbavu sina. Tunapenda sana mtelemko ndio maana tunakwama. I have gone long way baada ya kumaliza kusoma. Nina hakika kabisa, bila kubadilika sitafika. tena nibadilike kweli kweli. Nikiangalia wale walichosoma sawa na mimi wanachofanya wakafanikiwa, sina budi kubadilika.
Hela rahisi zipo Forever Living na Bitcon tu
 
Changamoto ni hatufanyi tafiti za production tokea mbegu mpaka kuvuna mpaka kuhifadhi. Zaidi sana ni kusikiliza stories tu katika vikao, vijiwe na WhatsApp Groups.

Hatujui wala hatuhoji kuhusiana na soko siki bidhaa ikiiva. Na hapa wanaumia zaidi wale wa perishable goods ambao hawakujipanga juu ya utunzaji, wale wa mitaji ya mikopo waliotoa ahadi ya marejesho ya mapema nao wanaangukia hapa.

Vitu vyote vinawezekana, sababu vyote vina walaji. Fanya utafiti, jipange kisha tenda
 
Naongezea

Wauza mihogo mibichi kuongeza nguvu za kiume

Kunywa madafu kuongeza nguvu za kiume

Kulima mahindi kwaajili ya kuuza yakiwa mabichi almaarufu mahindi ya kuchoma

Kwa kweli mfumo wa shule wa kukariri ndio unatupelekea tusiwe na hata chembe ya kufikiri
 
Back
Top Bottom