Wabomoa kaburi na kumwibia marehemu nguo

Wabomoa kaburi na kumwibia marehemu nguo

Mphamvu

JF-Expert Member
Joined
Jan 28, 2011
Posts
10,702
Reaction score
3,345
10407889_671782362927835_1081478994251468696_n.jpg



Watu wasiojulikana, wamebomoa kaburi na kisha kumvua nguo marehemu na kuiba vitu kadhaa alivyozikwa navyo yakiwemo mabegi mawili, pamoja na Vito kadhaa vya thamani na kisha kutoweka huko Kibaha, mkoani Pwani.

Kwa mujibu wa watu wa karibu na eneo hilo, walisema kuwa baada ya mazishi hayo kufanyika, ndugu waliweka mlinzi maalum wa kulilinda kaburi hilo kwa muda wa wiki 3, na baada ya muda huo kwisha na kisha mlinzi huyo kuondoka, ndipo lilipotokea tukio hilo lililowaacha watu wengi kutoamini kilichotokea.

Chanzo: Kado Cool
 
Mrehemu alizikwa na mabegi na vito? vya nini?
 
  • Thanks
Reactions: BAK
hayo mabegi yalikuwa ya kazi gani!!? au ni safari!!?
 
Hiyo ushawahi kutokea miaka ya nyuma Ktk makaburi ya mwananyamala, kuna bahari mmoja alizikwa na dhahabu, usiku wahuni wakamfukua
Kuchukua dhahabu zile alizovaa
 
walivyo mzika na mabegi na vito walitegemea nini na kwa nini wamemzika na mabegi au huko aendako akabadili nguo au akafanye biashara mambo mengine hayahitaji akili za kuambiwa kabisa yaani
 
Hao wezi wanastahili kupongezwa
ni ujinga mno kumzika mtu na vitu vya thamani..
ujinga kabisa

ha ha ha mkuu umechukia kweli ah ha ha alizikwa navyo akafanye biashara huko aendako labda na waliwaza nini
 
Makaburi ya kinondoni watu mpka leo wanaiba mishumaa na madhara ya mama, sasa wakiskia mtu kazikwa na vitu vya thamani unafikiri watakuacha, watakufukua tu masela
 
Ni tamaduni ya kabila husika au dini yake ndio iliyawasukuma kumzika marehemu na vitu vyake?...inashangaza...
 
Kwa hapa ndipo napo ona Imani ya ndugu zangu waislam haina mbwembwe kwenye suala la mazishi sasa mtu mnamzika na vito vya thamani vya nini sasa? Hata ningekuwa ni mimi ningefukua tu maana nitakuwasina dhambi kwa sababu niliyemuibia hana kauli.
 
Walimzika na vitu vya thamani ili akavithainishaje huko kaburini? jamaa alikuwa anapenda anasa duniani na kaburini anajinaksi amfurahishe nani? wacha vichukuliwe kwa sababu ni mali ya dunia.
 
Safi sana vijana ni kawaida kabisa vito vya thamani kufukuliwa chini na nyie mmevitoa chini hongereni sana kama mngevichukua akiwa juu mngekuwa mmeiba...nawapongeza kwa kazi nzuri
 
Mimi napita tu wadau maana haya mambo ni magumu!!

Kweli haya mambo ni magumu sana..nakumbuka mwaka juzi kuna jamaa angu alifiwa na Mama ake pale kibaha mailmoja..siku ya kuzika walishusha na mabegi yake ya nguo..nikashangaa sana..baadae nikauliza imekuwaje..jamaa wakasema Maza wao alikuwa ni mshirikina na inasemekana hata bro wao wa kwanza alifariki kwenye mazingira ya kishirokina so kama familia wakaona isiwe kesi..kila kitu chake wakifukie..nikachoka..!!
 
duuuuu!!! watu wanapataga wapi ujasiri wa kucheza na maiti??
 
Wanafamilia kwa umoja wao wamedhihilisha kuwa, kuwa tajili hakumaanishi kustaaribika Hata much. Aliyeendesha ibada ya mazishi ni mchumia tumbo tu.
 
Back
Top Bottom