Wabaya wa CHADEMA wavurugana!

Wabaya wa CHADEMA wavurugana!

Tanzania Daima ili ni gazeti pendwa la udaku.
 
Hapa ndipo ninapowapendea wana - CHADEMA wa JF! Anaanza mmoja anakuja kudondosha bonge la porojo jukwaani! Kisha,wanatokea wengine kiasi cha kumi hivi au hata kumi na tano kisha wanashikana mikono na kuizunguka porojo husika na kuanza kuimbishana "Ukuti! Ukuti! Wa Nazi, wa nazi! Ukuti, ukuti; wa nazi, wa nazi; Ukija upepo; wapepea ! ukija upepo, wapepea!!" Mwenye wowowo anazungusha wowowo, mwenye kitambi anazungusha kitambi;akina sie tunaishia kutikisa machogo tu;kutahamaki, kumbe kuepepea kwa ukuti si kudondoka kwa mnazi!!

hivi ndivyo wanavyofanya akina utaifa kwanza, marcopolo nk. tukirudi kwenye mada nimependa hili gazeti kuanza kufuatilia nyenendo za saumu ili kuweza kuthibitisha madai ya Lissu. sasa tunategemea kujua saumu alikuwa anawasiliana nabosi yupi! mwigulu au? je, akifahamika huyo atatueleza huo unga unawekwa na askari gani? saumu anatakiwa akamatwe na polisi kwa mahojiano. tunatarajia ccm wanaweza fanya kitu kwa saumu ili kupoteza ushahidi.
 
Mwigulu nchemba hizo siasa za kitoto anazoendesha zitammaliza kisiasa ndani ya ccm na nje ya ccm.Na aelewe hakuna siri chini ya jua siku si nyingi kila kitu kitakuwa wazi,huo mchezo watu wenye busara wa ccm wamekaa pembeni kwa kuwa wanajua mwisho wake ni mbaya kuliko mwigulu anavyofikiri.na hii njia anayotumia ili cdm ifutwe aelewe itasababisha vurugu maandamo na uasi mpaka kwenye vyombo vya ulinzi na usalama.


Mwisho wake utakuwa kama sera yao ya udini ilivyowatokea sasa. Maana 2005 sera iliyowaingiza Ikulu ni kuwa waliahidi kuanzisha mahakama ya kadhi. Leo hii wanasema serikali haipendelei dini yeyote. Sasa wana sera ya Ukanda mwisho wake utakuwa mbaya zaidi maana hata Rais atachaguliwa kwa ukanda
 
Wakiongozwa na Yuda Iskariyote, aka Ludovick. Hawa jamaa hawana akili, na ndo kusema shetani huwa hana mwisho mzuri, hayupo smart. Hivi unafanya dili la kuiba hela kwenye account ya mtu kwa kuhamisha kwa TT? hahaaa
 
Mwisho wake utakuwa kama sera yao ya udini ilivyowatokea sasa. Maana 2005 sera iliyowaingiza Ikulu ni kuwa waliahidi kuanzisha mahakama ya kadhi. Leo hii wanasema serikali haipendelei dini yeyote. Sasa wana sera ya Ukanda mwisho wake utakuwa mbaya zaidi maana hata Rais atachaguliwa kwa ukanda

Umesahau na kontena la visu ya CUF.
 
Chanzo Tanzania Daima ha ha ha yaani ukiisoma hiyo habari ni sawa wameandikiwa wale machizi wa Mirembe ha ha ha Chadema kama ndio style zenu za kupambana na ukweli ki-dizaini hii basi RIP
umesema kweli mkuu. Si wange iga Gazeti la UHURU?
 
Jaman naomba mnielezee maana ya cdm

Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums


Join Date : 26th July 2012Posts : 3
Rep Power : 0

Likes Received:2
Likes Given :0

Hii inaonyesha jinsi gani ulivyo MBWIGA, kama siku zote hizi toka umejiunga humu status yako iko hivi, unategemea hata ukiambiwa maana ya CHADEMA utaelewa???
 
Bado wanahangaika na CDM inayolindwa si na watu bali na malaika wote wa mbinguni ..watajane na wapeane sumu wote
 
Teh tehe teh teh teh...
Weitaaa... Niongezee heinekein 3 za bararidi...
 
Tanzania Daima ili ni gazeti pendwa la udaku.

Hahahaaa

Weita muongezee na Ritz viroba vinne...
Mkuu juzi nikuja hapo maeneo ya Lumumba kuchukua kagari kangu kwa wakala anaitwa Deoo... kapanga hapo kwenye jengo lenu...
Siku nyingine nikija ntakucheki...
 
Sio chadema,ni ufisadi na udhaifu ndio umefanya wananchi waichukie ccm
 
ccm si muwatumikie wananchi? Mbona mnateseka sana kukabiliana na chadema? Ccm naifananisha na enzi zile tulipokuwa boarding school, mwanafunzi mmoja ilikuwa ana mtindo wa kwenda kulia chakula bwenini japo uongozi ulikuwa unakemea sana. Yeye atafanya lolote hata kama ni baada ya saa zima ili mradi achenge walimu na viranja kisa akalie bwenini na alijiona mjanja kwenye hilo, kumbe ulimbukeni tu. Hao ndio ccm.
 
Dar es Salaam ni kijiji kikbwa cha majungi. Mara nyingi katika Tanzania mambo mengi huanza kama majungu,udaku au tetesi na hatimaye yanakuwa kweli. Mfano Richmond ilisemekana kuwa ni tetesi au udaku wa kwenye mtandao na hatimaye ikawa kweli. Ni kama drama, ni kama video. Je Mwigulu aliposema kuwa ana CD za CDM wakipanga mauwaji ya watu nchini yalikuwa ni majungu ya kisiasa au ilikuwa kweli? Tuone episode ya mwisho itakuwaje! Shooting bado inaendelea na wahusika wanakariri scripts zao. Je mtengeneza filamu ataweza kuweka stori zake vizuri? Au itaishia kwenye suspense kama ile ya Dr, Ukimboka? Tutayarishe popcorn na soda za kutosha maana yaelekea hii picha itakuwa ndefu kidogo
 
Vyama vya siasa vya Tanzania vinafanya makosa makubwa kutumia vijana wenye tamaa, wahuni, malaya n.k kuendesha siasa nyakati hizi.
Hata hivyo haya ni matokeo ya ufisadi uliojikita katika siasa kuazia miaka ya nyuma kidogo.
Kuna haja ya kuangalia upya sheria zinazohusika hata ikibidi vijana ambao wanataka kujiingiza katika siasa wawe wamefanya shughuli nyingine za kujiingizia kipato katika jamii kwa muda ili waijue jamii vizuri na hata wao wafahamike uadilifu wao.
Tutegemee madhara makubwa kwa taifa katika siku za usoni kama tutaendelea na siasa hizi.
Kurekebisha hali hiyo, itabidi kufanya mapinduzi ya nguvu ili kurejesha UTAIFA na UADILIFU!
 
Back
Top Bottom